Mabomu ya machozi yanarindima Ifakara sasa hivi

Mabomu ya machozi yanarindima Ifakara sasa hivi

Vyamavingi

JF-Expert Member
Joined
Oct 3, 2014
Posts
6,044
Reaction score
5,920
Nipo Ifakara, stendi ya Mlimba, polisi wanapiga mabomu ya machozi baada ya makundi ya vijana 'kuvamia' kituo kikuu cha polisi kushinikiza kuachiwa Diwani wa Kata ya Ifakara (Chadema).

Chanzo cha kukamatwa kwa Diwani sijakifahamu.

Source: Mimi mwenyewe.

Vv
 
Nipo Ifakara, stendi ya Mlimba, polisi wanapiga mabomu ya machozi baada ya makundi ya vijana 'kuvamia' kituo kikuu cha polisi kushinikiza kuachiwa Diwani wa Kata ya Ifakara (Chadema).

Chanzo cha kukamatwa kwa Diwani sijakifahamu.

Source: Mimi mwenyewe.

Vv


Duh hii nchi tusipochapana hatutaheshimiana,Diwani anawekwa ndani lakini mafisadi wameiweka serikali mfukoni
 
Elezea vizuri! kwani alikosa dhamana na kafanya nini mpaka akamatwe?
 
Nipo Ifakara, stendi ya Mlimba, polisi wanapiga mabomu ya machozi baada ya makundi ya vijana 'kuvamia' kituo kikuu cha polisi kushinikiza kuachiwa Diwani wa Kata ya Ifakara (Chadema).

Chanzo cha kukamatwa kwa Diwani sijakifahamu.

Source: Mimi mwenyewe.

Vv

kiongozi kama uko hapo ihi toka nje utuletee habari kamili
 
Risasi pia zinarindima.

Sababu ya haya yote ni Uchaguzi wa serikali za mitaa. Diwani inasemekana amegomea baadhi ya mambo na wakamkamata na kumchapa makofi na kumpeleka polisi.

Kasheshe inaendelea...
Vv
 
Nadhani huyu ni yule diwani aliyebambikizwa kesi ikidaiwa kwamba amemzuia karani wa uandikishaji chaguzi za serikali za mitaa kufanya kazi yake?
 
Nadhani huyu ni yule diwani aliyebambikizwa kesi ikidaiwa kwamba amemzuia karani wa uandikishaji chaguzi za serikali za mitaa kufanya kazi yake?

nipo hapa ifakara kwa sasa, kilichotokea ni kwamba Jana baada ya kufungwa kituo kimojawapo katika kata hii, Leo asubuhi ikaonekana idadi ya watu waliokuwa wsmejiandikisha mpaka Jana jioni imeongezeka tofauti na walivyo funga kituo. Diwani wetu ambaye no jembe kweli kweli alipokwenda kuhoji likatokea zogo na kupelekea diwani kukamatwa na polisi. RAIA wenye hasira Kali walivamia kituo cha polisi kwa lengo LA kumtoa diwani.....hivi ninavyo andika of is I ya mtendaji inawaka moto. hali sio swari
 
Kwa sasa hali imetulia baada ya Diwani kuachiwa.

Nawalaumu Polisi, wanatumia maguvu mahali pasipohitaji ubabe.

Uongozi na dhamana,na kiongozi hajiweki, anawekwa na watu; kiongozi wa Upinzani ili ashinde, ni lzm awe na watu wengi nyuma yake, tena waliodhamiria, hivyo ni vema kutumia busara.

Polisi wamesababisha hasara kubwa kwa mali za watu.

Nadhani Polisi walitaka kuhua kama Diwani Lijualikali bado anaungwa mkono baada ya vurugu za uchaguzi mdogo mwaka jana.

Ni vema polisi waangalie upepo wa kisiasa unavumaje kuliko kutumia ubabe kila mahali.

Watanzania ni kama vile wamechoka na wana stress, suala dogo tu tena ambalo halina uzito mkubwa, linawafanya wa-react kwa namna ya kushangaza.

Vv
 
.......to b honest sikuwahi kuona nguvu ya umma kabla. Leo ndio nimeona. polisi wamemaliza mabomu yote ya machozi mwishoe diwani kaachiwa. UMMA ukiamua unaweza.
 
.......to b honest sikuwahi kuona nguvu ya umma kabla. Leo ndio nimeona. polisi wamemaliza mabomu yote ya machozi mwishoe diwani kaachiwa. UMMA ukiamua unaweza.

Safi sana mdogo mdogo tu kitaeleweka hiyo ndiyo nguvu ya umma.
 
nguvu ya umma hairudi nyuma hata muwapige mitama daima itasimama,CHADEMA MOTO JUU!
 
Back
Top Bottom