Mutta
Senior Member
- Mar 24, 2011
- 101
- 11
Hivi juzi yalitokea mafuriko jijini Dar na Serikali imejitahidi kuwatafutia viwanja MABWEPANDE ili wanaokaa mabondeni wakae sehemu salama.Lakini watu waliobomokewa nyumba wakati wa MABOMU YA GONGOLAMBOTO mpaka sasa viwanja havijapatikana na nyumba hawajajengewa kama Serikali ilivyoahidi ikidai eneo lililo patikana lina mgogoro(je mabwepande haikuwepo?).Kibaya zaidi hata wale waliosababishiwa VILEMA serikali haijawafidia kama ilivyoahidi wengine wanaishi maisha ya shida kwani Walivunjika MIKONO,MIGUU ,MIGONGO nk. hawana mahitaji yao ya kila siku.Serikali yetu inashangaza sana hasa inapochelewesha kulipa watu wakati pesa nyingi ilichangwa na taasisi mbali mbali.Wana jf tufanyeje ili serikali iwalipe watu wa GONGOLAMBOTO?