mablogers njooni mtupe maujuzi

mablogers njooni mtupe maujuzi

Oxpower

JF-Expert Member
Joined
Jan 15, 2012
Posts
2,181
Reaction score
3,115
habari za kazi waungwana

twende moja kwa moja kwenye topic.
siku za hivi karibuni biashara ya blog imekua ikikua kwa kasi sana hapa nchini kwetu.na vijana wengi wamekua wakitamani sana kuitumia hiyo fursa lakini tatizo ni elimu juu ya hiyo kitu,wengine hawajui hata pakuanzia,na wengine wamefanikiwa kufungua lakin zimeishia kufungwa na pia kutowalipa hata tsh 10.

hivyo basi nmeleta huu uzi ili wataalamu watujuze namna nzuri ya kuanzisha na kuendesha ili iweze kutoa manufaa,kwa mfano tunaweza kujuzana kuhusu
1;jinsi ya kuanzisha,yani kufungua je wapi na nani anaweza kukutengenezea na kwa gharama nafuu
2.aina ya blog,yan ni aina ipi nzuri kufungua ambayo inaweza kukulipa kirahis
3;namna ya kuchagua jina kulingana na lengo la blog yako
4;blog inakulipaje
5;njia bora yakuchukulia pesa yako ambayo haina makato makubwa
6;ongezea mambo mengine...........................
 
Nawasubil waje wataalam maana na mm nahitaji kujua kiundani juu ya hilo
 
Nichangie Kidogo Kwa kile ninachojua..

Kwanza unapaswa kujua Lengo (maudhui) lako kubwa la kuanzisha blog ni nin asa
mfano we unataka kwa ajili ya kutangaza biashara yako au kwa ajili ya kutoa Elimu juu ya jambo flan mfano Afya, Tech, au Dini. Au unaweza ukawa unataka kuanzisha kwa ajili ya Habari.

Pili unatakiwa kujua walengwa wa blog yako au wasomaji wako watakuwa watu wa aina gani hii itakusaidi kujua ni wapi paku wapata watembeleaji au wasomaji wa blog yako.

Tatu Jina la Blog yako... hapa ndipo wanapo chemsha.... Unapaswa kuwa na jina linaloendana na blog...
Mfano blog yako inahusiana na makala za michezo inakupasa kuchagua jina ambalo lina maudhui ya kimichezo na si vinginevyo.... Hii itakusaidia hata kupatikana kiurahisi kwenye search engine kubwa kama Google.. Pia unashauriwa kuchagua jina fupi na linalo tamkika kirahisi.... hii itasaidia kukumbukwa kwa urahisi na kuwa na Unique visitors.

La nne ni Template au Design.. Hakikisha blog yako ina mwonekano mzuri, wa kipekee na wa Kuvutia.. Blog kuwa na mwonekano mzuri humfanya mtembeleaji kuipenda na kurudi mara kwa mara kusoma habari zako... Kingine inapaswa kuwa mobile friendly, asilimia kubwa ya watu kwa sasa ni watumiaji wa internet na wengi wakiwa wanatumia simu Janja hivyo hata watembeleaji wengi wa blogs hutumia simu kuperuzi.

Tano ni Uandishi: Wengi wana blog nzuri na zenye sifa karibu zote ila linapokuja swala la uandishi ndipo tunaposhindwa.... Jaribu kuwa wakipekee... Andika habari nzuri na kwa mpangilio mzuri epuka ku copy na Kupest pia andika vitu vitakavyomfanya mtembeleaji kurudi tena kesho.......

Sita na Mwisho kwa leo ni Kuitangaza.
Hii ni muhimu sana kwani blogs kwa sasa zipo nyingi sana kwa hapa tuu tanzania zinaweza zikawa zinafika hata 1000+.... Tumia mitandao ya kijamii kuitangaza kwa kutengeneza funpage kama Facebook, Instagram, Twitter, Whatsapp, Snapchat nk. Hakikisha unapo andika habari mpya una share kwenye hiyo mitandao ya kijamii... Pia unaweza kutumia matangazo ya kulipia kama Facebook +Instagram hapo unaweza tangaza hata kwa $2 pia kuna Google adwords unaweza kutangaza pia kupitia Email marketing mfano mzur MailChimp wanakupa free acount
YOTE HII NI KUIFANYA BLOG YAKO KUJULIKANA NA KUWA NA WASOMAJI WENGI.
Naomba niishie hapo kwa leo japo Yapo mengi ya kuandika kuhusu tasnia hii ya bloger nadhani wengine nao wata changia.
 
Nichangie Kidogo Kwa kile ninachojua..

Kwanza unapaswa kujua Lengo (maudhui) lako kubwa la kuanzisha blog ni nin asa
mfano we unataka kwa ajili ya kutangaza biashara yako au kwa ajili ya kutoa Elimu juu ya jambo flan mfano Afya, Tech, au Dini. Au unaweza ukawa unataka kuanzisha kwa ajili ya Habari.

Pili unatakiwa kujua walengwa wa blog yako au wasomaji wako watakuwa watu wa aina gani hii itakusaidi kujua ni wapi paku wapata watembeleaji au wasomaji wa blog yako.

Tatu Jina la Blog yako... hapa ndipo wanapo chemsha.... Unapaswa kuwa na jina linaloendana na blog...
Mfano blog yako inahusiana na makala za michezo inakupasa kuchagua jina ambalo lina maudhui ya kimichezo na si vinginevyo.... Hii itakusaidia hata kupatikana kiurahisi kwenye search engine kubwa kama Google.. Pia unashauriwa kuchagua jina fupi na linalo tamkika kirahisi.... hii itasaidia kukumbukwa kwa urahisi na kuwa na Unique visitors.

La nne ni Template au Design.. Hakikisha blog yako ina mwonekano mzuri, wa kipekee na wa Kuvutia.. Blog kuwa na mwonekano mzuri humfanya mtembeleaji kuipenda na kurudi mara kwa mara kusoma habari zako... Kingine inapaswa kuwa mobile friendly, asilimia kubwa ya watu kwa sasa ni watumiaji wa internet na wengi wakiwa wanatumia simu Janja hivyo hata watembeleaji wengi wa blogs hutumia simu kuperuzi.

Tano ni Uandishi: Wengi wana blog nzuri na zenye sifa karibu zote ila linapokuja swala la uandishi ndipo tunaposhindwa.... Jaribu kuwa wakipekee... Andika habari nzuri na kwa mpangilio mzuri epuka ku copy na Kupest pia andika vitu vitakavyomfanya mtembeleaji kurudi tena kesho.......

Sita na Mwisho kwa leo ni Kuitangaza.
Hii ni muhimu sana kwani blogs kwa sasa zipo nyingi sana kwa hapa tuu tanzania zinaweza zikawa zinafika hata 1000+.... Tumia mitandao ya kijamii kuitangaza kwa kutengeneza funpage kama Facebook, Instagram, Twitter, Whatsapp, Snapchat nk. Hakikisha unapo andika habari mpya una share kwenye hiyo mitandao ya kijamii... Pia unaweza kutumia matangazo ya kulipia kama Facebook +Instagram hapo unaweza tangaza hata kwa $2 pia kuna Google adwords unaweza kutangaza pia kupitia Email marketing mfano mzur MailChimp wanakupa free acount
YOTE HII NI KUIFANYA BLOG YAKO KUJULIKANA NA KUWA NA WASOMAJI WENGI.
Naomba niishie hapo kwa leo japo Yapo mengi ya kuandika kuhusu tasnia hii ya bloger nadhani wengine nao wata changia.

shukrani sana mkuu,walau tumepata mwanga na natamani uendelee kutupa elimu zaid kadri upatapo muda
 
Back
Top Bottom