Mabeberu wameanza fyokofyoko DR Congo

Mabeberu wameanza fyokofyoko DR Congo

Mabeberu wa Afrika ni waafrika wenyewe.
Wazungu walishatoka Afrika miaka mingi.

Aliyepewa ushindi ni Mkongo na Mwafrika mwenzetu.

Kuna baadhi ya dini zinaweka mbele maslahi ya mabeberu duniani na si vinginevyo.

Nadhani kwanza tungempongeza Kabila kwa kuthubutu kuendesha Uchaguzi Kwenye eneo hilo .
Nadhania ilikua ni mwanzo mzuri wa Demokrasia. Wapinzani wangekubaliana na matokeo mana Demokrasia Afrika ni changa sana. Inabidi tumpongeze mtu anayeweza kusimamia uchaguzi na chama chake kikashindwa.

Tanzania CCM hakiwezi kwa namna yoyote hata uchaguzi mdogo kabisa wa udiwani bado kinatumia hila kishinde kwa 99%.

Joseph Kabila ni Rais atakayekumbukwa sana kwenye ukanda huo wa walevi wa madaraka na wabinafsi.
Ukanda wenye mabeberu weusi.

Siungi mkono harakati zozote za kidini huko Kongo.
Dini na siasa ndizo zinazovuruga Demokrasia ukanda huu wa Mashariki na kati.

Hata nchi za jirani na Kongo kuna udini udini ndio maana akitawala wa dini tofauti na mabeberu anapigwa vita sana hata kama anatenda haki na kukuza Demokrasia.

Kongo Rais ameshapatikana nafikiri Kabila angekua mtata angetakua amefuta kifungu cha kuhoji matokeo mahakama.

Simuungi Mkono Martini Fayulu mana ni chaguo la Mabeberu.
Bora Chaguo la Kabila mwafrika na Mkongo lakini sio huyo Martini chaguo la Ufaransa amboa ama kwa hakika wanaiona Kongo kuna shamba lao la bibi.

Cha msingi waunde serikali ya ummoja wa kitaifa ili kumaliza migogoro ya miaka mingi. Kongo irejee kwenye amani.
Kanisa Kirumi libaki kusimamia haki za watu wake chini ya Rais mteule.

Ninawasiwasi kuwa Mabeberu walitengeneza matokeo yao kwa malengo yao Kabila akawashtukia.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Huku dunia ikisubiri kwa tahadhari uamuzi wa mahakama ya kikatiba juu ya ni nani mshindi wa kura za urais huko Kongo, kumeibuka data zilizovujishwa kutoka ndani ya database ya tume ya uchaguzi inayohusisha asilimia 86 ya kura zote zilizopigwa. Data hizi ambazo zimechambuliwa na kuripotiwa na gazeti la financial times zinaonyesha kuwa mgombea Martin Fayulu alishinda uchaguzi wa December 2018 kwa asilimia 59.4 (59.4%), akifuatiwa kwa mbali na Felix Tshisekedi aliyepata asilimia 19 (19%)- Congo voting data reveal huge fraud in poll to replace Kabila. Pamoja na juhudi za Kabila kujaribu kuendesha uchaguzi kwa kuzuia usimamizi wa uchaguzi kwa vyombo kutoka nje, yaonekana wazi kuwa kuna wazalendo waliowezesha kukushanya hizo taarifa sahihi na kuzivujisha.

Taarifa hizi mpya, zinakaribiana sana na zile zilizotolewa na kanisa katoliki zilizokusanywa kwenye vituo zaidi ya elfu 40 zilizoonyesha kuwa Bw. Fayulu alishinda kura za urais kwa zaidi ya asilimia 60. Pamoja na hayo, waratibu wa kampeni ya Bw. Fayulu, wanadai kuweza kukusanya sampuli za matokeo yanayoonyesha ushindi wa zaidi ya asilimia 61. Takwimu hizi, zimeongeza hisia za watu wengi ndani na nje ya Kongo kuwa Kabila aliingia makubaliano ya kushirikiana madaraka na Bw. Tshisekedi, baada ya kudhihirisha kuwa asingeweza kumtangaza mgombea wa chama chake Bw. Shadari aliyeshindwa vibaya mno kwenye uchaguzi huo.

Kutokana na taarifa hizo, dunia imeanza kuimulika Kongo. Jumuiya ya SADC ambayo Kongo ni mwanachama, imeitisha kikao cha dharura kuijadilli huko Addis Ababa, Ethipia - SADC calls for emergency meeting over DRC poll. Pia SADC ambayo kupitia waangalizi wake kwenye huu uchaguzi katika hatua za awali ilitoa maoni kuwa ulienda vizuri na kasoro ndogondogo, imegeuka msimamo wake wa awali na kuitaka tume ya uchaguzi ya Kongo (CENI) ihesabu kura upya African nations call for recount in DRC election. Mataifa yenye ushawishi Kongo, mfano Ubelgiji, Ufaransa na Marekani, wote kuanzia awali waliyatilia shaka matokeo ya uchaguzi, wakisema yalipinduliwa.
Wana jisumbua tu mijizi hiyo walahi
 
Nyie si mlichukulia poa tu na mkaridhika na hali yenu..??
Na hako ka-Jecha mkakaona ka malaika fulani!!
Maalimi Alifika mpaka uingereza... wakamzuga zuga tu... Au hukuwa na taarifa kuwa maalimi alienda kushtaki uko?
 
Mabeberu wa Afrika ni waafrika wenyewe.
Wazungu walishatoka Afrika miaka mingi.

Aliyepewa ushindi ni Mkongo na Mwafrika mwenzetu.

Kuna baadhi ya dini zinaweka mbele maslahi ya mabeberu duniani na si vinginevyo.

Nadhani kwanza tungempongeza Kabila kwa kuthubutu kuendesha Uchaguzi Kwenye eneo hilo .
Nadhania ilikua ni mwanzo mzuri wa Demokrasia. Wapinzani wangekubaliana na matokeo mana Demokrasia Afrika ni changa sana. Inabidi tumpongeze mtu anayeweza kusimamia uchaguzi na chama chake kikashindwa.

Tanzania CCM hakiwezi kwa namna yoyote hata uchaguzi mdogo kabisa wa udiwani bado kinatumia hila kishinde kwa 99%.

Joseph Kabila ni Rais atakayekumbukwa sana kwenye ukanda huo wa walevi wa madaraka na wabinafsi.
Ukanda wenye mabeberu weusi.

Siungi mkono harakati zozote za kidini huko Kongo.
Dini na siasa ndizo zinazovuruga Demokrasia ukanda huu wa Mashariki na kati.

Hata nchi za jirani na Kongo kuna udini udini ndio maana akitawala wa dini tofauti na mabeberu anapigwa vita sana hata kama anatenda haki na kukuza Demokrasia.

Kongo Rais ameshapatikana nafikiri Kabila angekua mtata angetakua amefuta kifungu cha kuhoji matokeo mahakama.

Simuungi Mkono Martini Fayulu mana ni chaguo la Mabeberu.
Bora Chaguo la Kabila mwafrika na Mkongo lakini sio huyo Martini chaguo la Ufaransa amboa ama kwa hakika wanaiona Kongo kuna shamba lao la bibi.

Cha msingi waunde serikali ya ummoja wa kitaifa ili kumaliza migogoro ya miaka mingi. Kongo irejee kwenye amani.
Kanisa Kirumi libaki kusimamia haki za watu wake chini ya Rais mteule.

Ninawasiwasi kuwa Mabeberu walitengeneza matokeo yao kwa malengo yao Kabila akawashtukia.


Sent using Jamii Forums mobile app
Mawazo mazuri. Ila ni afadhali wangekubaliana kuundwe serikali ya Bw, Tshisekedi ya mpito kisha uchaguzi uitishwe upya ndani ya mwaka mmoja bila Kabila. Ikiwezekana Kabila na baadhi ya wafuasi wake wawekwe kizuizini ili wasije wakaingilia mpangilio mpya wa serikali ya mpito.
 
Walioitisha kikao cha dharura SADC nao ni mabeberu kumbe
Naona neno "Ubeberu na Mabeberu" limeshika kasi sana. Ila mimi binafsi linanipa kichefuchefu. Ina maana kama hao ni mabeberu, sisi ni mbuzi jike? Tuache utani bwana, ni afadhali mtu kukitwa beberu kuliko mbuzi jike. Beberu likikutana na mbuzi jike tunajua kitakachoendelea. Watanzania tuache kujidhalilisha wajameni.
 
Afrika wamezidi ujinga wa kuibaiba kura na dawa pekee inayowafaa ni kuwekewa vikwazo vikali vya kiuchumi ili iwe fundisho kwa wengine.

Watawala wanaojifanya watemi kama alivyokuwa Mugabe, Gaddafi au Sanchez hawafai na udikteta wao ndio chanzo cha nchi zao kuporomoka kiuchumi. Mahakama ya Congo DR itende haki kwa kutii matakwa ya wakongomani kwa kuthibitisha ushindi wa Bw. Martin Fayulu.
 
Nadhani hujitambui jinsia yako wewe!
Hao "MABEBERU" ndio wamekupatia "Tanganyika" na baadaye Tanzania. Huko Berlin.
Kwaiyo iyo ndo sababu inayofanya mwendelee kuwalamba nyao. Sasa endeleeni kuwalamba lakini mkirudi tz sisi tutawaonyesha kazi kwamba tz ni ya kwetu na sisi ndo watawala na kuwafundisha uzalendo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sasa kusipokalika unamkomoa Nani?

Wewe unadhan kati ya Mwananchi wa kawaida Na Nkurunzinza Nani anateseka zaid kwa ukosefu wa Amani Burundi?

Ahahahahah unajua tunaongelea nchi gani..?? Au unataka uposti uwahi kupata buku 7??
 
Aisee! Mie ningepitia jeshini ningeshaasi,huwa sikubali kuonewa kizembekizembe na mtu wa aina yoyote ile! Awe na cheo au asiwe na cheo,ningeshawanyoosha wengi tu
Nalog off
 
Back
Top Bottom