Mabati ya ALAF yako overated sana

Mabati ya ALAF yako overated sana

Mukulu wa Bakulu

JF-Expert Member
Joined
Aug 12, 2014
Posts
4,050
Reaction score
12,966
Kwa utafiti wangu mdogo nimeona watanzania tunapigwa na wauza mabati ya ALAF kwa kuaminishwa kua yako special sana kuliko mabati mengine.

Haya mabati tunapigwa, hayana ubora wa kipekee kuliko mabati mengine, hayana utofauti wowote.

Kwa kweli sijaona chochote cha ziada kwenye hayo mabati. Usiwe draged na majority, hayana upekee wowote.
 
Si kweli ndugu angalia mabati ya kampuni zingine yanavyo pauka paa linakuwa na mabakamabaka ndani ya mwaka mmoja tu.

Mikoani wanaumizwa sana. Wanauziwa mchanganyiko wa mpauko au kutu na mapya. Pita Ruvuma Mbimga etc. Sheeda
 
Mabati mengine kama yapi ili twende sawa katika mjadala mkuu
 
Utafiti wako umegundua nini?yanapata kutu au nini mbona umeleta habari kama ya kichuki bila hata kujipanga
 
Mkuu nadhani hujafanya utafiti kidogo tembea kwenye nyumba walizoezeka bati za Alaf-Simba dumu na bati zingine waulize tu zina miaka mingapi harafu angalia ubora wake harafu urudi hapa kutupa mrejesho
 
we!!we!!! labda hujawahi kujenga, na kama hujawahi kujenga hujatembelea kwenye majengo ya watu ukaona jinsi mabati ya kampuni nyingine yalivyopauka kama ngozi ya kenge? asikudanganye mtu kwa bongo bati ni ALAF tu
Yeah nilichogundua ni hiko kwa mleta mada hajawahi kujenga ina maana hayajui vizuri hayo mabati,pamoja na kwamba wana promotion kubwa hata mabati yao ni mazuri mno huwezi linganisha na mengine hapa Tz
 
Yeah nilichogundua ni hiko kwa mleta mada hajawahi kujenga ina maana hayajui vizuri hayo mabati,pamoja na kwamba wana promotion kubwa hata mabati yao ni mazuri mno huwezi linganisha na mengine hapa Tz
Ni sahihi kabisa, unaweza kutumia garama kubwa kununua mabati ya rangi tena yale yaliyokunjwa kama vigae (versetile) ambayo kibongobongo tunaita msauz hata kama ni wachina wametengenezea hapo kariakoo na kupaka marangi ya hovyo ,mwisho wa siku yakianza kukauka nyumba inakuwa mbaya kuliko yule aliyeezekea mabati ya bei nafuu yanayoitwa ya nyumba za waalimu
 
Ni sahihi kabisa, unaweza kutumia garama kubwa kununua mabati ya rangi tena yale yaliyokunjwa kama vigae (versetile) ambayo kibongobongo tunaita msauz hata kama ni wachina wametengenezea hapo kariakoo na kupaka marangi ya hovyo ,mwisho wa siku yakianza kukauka nyumba inakuwa mbaya kuliko yule aliyeezekea mabati ya bei nafuu yanayoitwa ya nyumba za waalimu
Hawa vijana hawajajenga ndio maana wakianza ujenzi wataelewa tu
 
Vitu vingi mkuu vipo over rated yaan mpaka unashangaa sifa zote zile kumbe hali halisi ndio hii? Papuchi ipo over rated Simba SC ipo over rate n.k n.k
 
Back
Top Bottom