Maaskofu ndio wasaliti

Maaskofu ndio wasaliti

Kweli umeamua kushikilia msimamo wako,lakini unapaswa ujue kanisani sio sehemu sahihi kwa hiyo mijadala,hayo jadilini mitaani kwenu.Kanisa ni Universal institution, sio taasisi ya kitaifa,ndio maana aihitaji kuwa raia ili uwe mshirika kama ilivyo kwa vyama vya siasa
viongozi wa kanisa wana wajibu wa kuwaelimisha waumini wao kimwili na kiroho...ndo maana makanisa yaliyokamilika yanajenga na mashule na mahospital pia, vinginevo yangejikita kujenga makanisa tu yasingepata mafanikio yalionayo kiroho. sioni shida kwa viongozi wetu kutupa mwanga katika tusiyoyajua
 
Walikwepo Mjengoni walijadili mwanzo mwisho, sasa kulikoni. WTZ inatupasa kuelewa Bin Adam ye yote siyo Maaika. Makundi yalijadili mapendekezo ikaja katiba inayopendekezwa, sasa tuisome kwanza ndipo tuamuwe, pole sanaaaa wewe unataka kubebewa Akili na maamuzi.
 
Eti Roman Catholic!......ni kati ya maneno magumu mno kuyatamka ikiwa kwa kujitambulisha au chochote kile, as a matter of fact nilishafuta kwenye akili yangu hii kitu,watu weusi tuna shida kubwa sana ambayo sijui kama tutakuja kujitambua...!!
 
Hii ni imependekezwa, haijalitishwa. Kwa kura ngapi imepitishwa. Tusikurupuke tuisome kwanza tielewe nzuri lipj, baya lipj, ukisha ifahamu toa maamuzi yako. Usikubali kubebewa Akili KTK Uamuzi wako,
 
Mimi ni Roman Catholic lakini hawa maaskofu wamenifanya niufikirie mara mbili mbili huu ukatoliki wangu.

Kwanini hawa maaskofu watudharau kwa kiasi hiki? Yani wametuona sisi ni ma-Robot tusioelewa chochote hadi tuelekezwe cha kufanya?

Hawa maaskofu kwa akili zao wanadhani Mungu alishindwa kutufanya ma-Robot tufanye anayoyataka yeye tuepukane na haya mateso ya hii Dunia?

Wamenikera sana hao maaskofu.

Mbona Viongozi wa Serikali walitoa wito tupige kura za NDIO? Hao hawajakukera?
 
Jibu unalo, Waserikali sio Wading!!!!!!! Pia kumbuka makundi yaliyo shiriki kupendekeza katiba, Wanasiasa wa Ukawa ndo waliona maslahi yao yatakuwa madogo wakasusa sasa Viongozi wamakanisa wanatoka kundi gani? Na wao CDM? NCCR CUF nk wasijifiche.
TANZANIA AMANI KWANZA, TANZANIA KWANZA, UMOJA KWANZA, UPENDO KWANZA, MSHIKAMANO KWANZA.
 
Kama ndio hivyo wewe huna haja ya kwenda kanisani kwa sababu unajua kila kitu na huna haja ya kuongozwa!

Mimi ni Roman Catholic lakini hawa maaskofu wamenifanya niufikirie mara mbili mbili huu ukatoliki wangu.

Kwanini hawa maaskofu watudharau kwa kiasi hiki? Yani wametuona sisi ni ma-Robot tusioelewa chochote hadi tuelekezwe cha kufanya?

Hawa maaskofu kwa akili zao wanadhani Mungu alishindwa kutufanya ma-Robot tufanye anayoyataka yeye tuepukane na haya mateso ya hii Dunia?

Wamenikera sana hao maaskofu.
 
Tatizo Lako Mkuu Bado Hujamuelewa Vizur MUSAMI Kwa Ufupi ilitakiwa Maaskofu Wakae Pamoja Na Mashekhe
:shocked:
Wajadil Msimamo Wao Ndo Wautoe Hadharani. Lakin Kusema Maadhimio Ya Maaskofu Tz Ni ... Juu Ya Katiba. Swali, Je Masheikh Nao Wakija Na Msimamo Wao Kinyume Na Maaskofu Huoni Kama Itatokea Balaa Kubwa?.

Mbona Viongozi wa Serikali walitoa wito tupige kura za NDIO? Hao hawajakukera?

Wewe kweli kiazi.. ni vigumu kuelewa.. swali gani hilo!?
 
Kwa hiyo wewe unakubali serikali inavyoipigia debe katiba? Serikali yenyewe ina ajenda gani inapowaambia watu wapige kura ya NDIYO? Kwa nini serikali wasitoe tu uhamasishaji wa kusoma katiba wakawaacha watu kuamua wenyewe? Mifano halisi ninayo. Waziri Mh Mary Nagu juzi kati alikuwa na wamasai akawaambia hii katiba ni nzuri wapige kura ya NDIYO (Hiyo ni kampeni ya serikali) Makamu wa pili wa rais kule Zanzibar naye hivi majuzi kule Zanzibar aliwaambia wananchi kuwa wapige kura ya NDIYO. (Pia hiyo ni kampeni ya serikali)

Sasa inakuwaje vibaya Maaskofu kuwaambia waumini wao wapige kura ya HAPANA wanapoona inatakiwa kuwa hivyo? Jamii forum ni ya watu wenye akili wanaoweza kuchambua mambo lakini nasikitika kuona watu wengi wanashindwa kuielewa vizuri hii nchi yetu. Tukubaline hapa kama Maaskofu wamekosea basi na serikali ishakosea zamani na hakuna wa kumlaumu mwenzie..

Serikali ndio inayokusanya kodi na kupanga matumizi yake, walipanga kutumia kiasi cha pesa kilichotumika kwenye mchakato wa katiba mpaka kukamilika kwake, itakuwa ni kitu cha ajabu serikali kusema pigieni kura ya hapana katiba pendekezwa, ni sawa na kusema baba amenunua mboga ili watoto wake wapate kula, anafika nyumbani anaamua kuimwaga mboga eti kwa kuhofia watoto hawata kula, hivyo mzazi ataingia gharama ya kununua mboga nyingine, hapo utakuwa hujawaumiza watoto unajiumiza wewe mwenyewe mzazi ambayo ndiyo serikali
 
Sawa kujenga jengo la gharama halafu anakuja mtu anawaambia watu bomoweni, wewe na watu wako mtaonekana vp?
 
Back
Top Bottom