Tokea Kardinali Pengo atoe kauli ya kupinga mapendekezo ya Maaskofu juu kura ya hapana kwa katiba inayopendekezwa,amekuwa akiitwa msaliti hata kufikia kutukanwa na akina Gwajima, lakini nionavyo mimi wasaliti ni maaskofu.
1. Wameusaliti wito wao wa kuutangaza Ufalme wa Mungu badala yake wamekaa wakipoteza muda kuujadili ufalme wa duniani Luka 9:2 Yohana 18:36 labda watuambie wameongozwa na andiko gani
2. Wamesaliti umoja wa Taifa la Tanzania maana unapotoa tamko la wakristo kupiga kura ya hapana unawaambia nini watu wa imani nyingine?je na wao wakikutana kupiga kura ya ndio,mustakabari wa Taifa utakuwaje?
3. Je huu sio mwanzo wa kutumia umoja huu kufanya kampeni za viongozi wanaoona wao wanafaa kuongoza kipindi cha uchaguzi?
4. Makanisa yanahusisha watu kutoka makundi mbalimbali, wapo wanaoipinga katiba inayopendekezwa na wapo wanaoikubali,je huu sio mwanzo wa kukaribisha migogoro ya kiitikadi ndani ya makanisa.
Mungu atusaidie...