Nyendo
JF-Expert Member
- Jun 4, 2017
- 1,359
- 4,814
Ghasia zimeibuka tena katika mji mkuu wa Lebanon, Beirut, ambapo vikosi vya usalama vimetumia gesi ya kutoa machozi na mizinga ya maji dhidi ya waandamanaji ambao walikuwa wakirusha chupa na mabomu ya kienyeji karibu na jengo la bunge.
Idadi kubwa wa watu walijeruhiwa katika kadhia hiyo ya Jumapili. Hali hii ya maandamano ya kulipinga kundi la wanasiasa walio katika hatamu ya uongozi imekuwa ikiendelea tangu katikati mwa mwezi Oktoba.
Safari hii waandamanaji wanapinga waziri mkuu aliyejizulu Saad Hariri akirejea tena katika serikali itakayoundwa. Wanataka kiongozi huru kabisa ambaye hana muingiliano na vyama vya kisiasa nchini humo.
Chanzo: DW Swahili
Idadi kubwa wa watu walijeruhiwa katika kadhia hiyo ya Jumapili. Hali hii ya maandamano ya kulipinga kundi la wanasiasa walio katika hatamu ya uongozi imekuwa ikiendelea tangu katikati mwa mwezi Oktoba.
Safari hii waandamanaji wanapinga waziri mkuu aliyejizulu Saad Hariri akirejea tena katika serikali itakayoundwa. Wanataka kiongozi huru kabisa ambaye hana muingiliano na vyama vya kisiasa nchini humo.