Maandamano ya kupinga fujo za Mbowe, Mwanza

Maandamano ya kupinga fujo za Mbowe, Mwanza

hii ni mara ya tatu anatuletea fujo, mara ya kwanza kahamisha msiba kutoka geita na kuuleta mwanza bila sababu za maana nayo ikaleta taharuki kweli, mara ya pili kaja kwenye kesi ya wenje wakati anajua kabisa huyo jamaa yake alishindwa uchaguzi bado akatuletea jam mjini, kaja tena! hapana uvumilivu umetushinda.

Ujue panapotokea kurupushani za kisiasa tunaoumia wa kwanza ni wafanyabiashara, maduka yanavunjwa bidhaa zinaporwa wateja wetu wanakimbia kwa hofu na mauzo yanadorora wakati huo huo marejesho ya bank yako palepale, kodi zinatusubiri wafanyakazi wetu wanataka mishahara na makanisani tunatakiwa tuwakilishe zaka. sasa mji wetu wakati wa amani tu tumebanana bado mjinga mwingine atuletee jam za kipumbavu, kaacha kujadili budget anakuja kutuletea jam mjini.

Dah! Nimekuelewa mkuu changamoto mlionayo ila kuwa mpole na mvumilivu ili sheria na katiba ''tuliyojiwekea'' kupitia Bunge ichukue mkondo wake kupitia tafsiri sahihi itakayotolewa na waheshimiwa ma-Jaji wa Mahakama Kuu jijini Mwanza itakayotupa mwelekeo wa kesho kwa Tanzania nzima .
 
Ndo hivyo tena katiba yetu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inatoa nafasi mtanzania kufungua kesi ya kikatiba katika Mahakama Kuu popote ndani ya mipaka ya Tanzania Bara.

Labda Bunge lifanye marekebisho ya sheria kwa hati ya dharura kwa kutumia wingi wa wa-Bunge wa CCM bungeni lakini katika hali ilivyo sasa hakuna jinsi kesi imefunguliwa Mahakama Kuu jijini Mwanza na imetimiza mahitaji yote kisheria na kikatiba kusikilizwa katika mji wenu wa Mwanza.
hakuna cha katiba hapa anatetea pesa kutoka chama cha centre party cha Norway kupitia TDC, anafanya show apeleke clip kwa wafadhili apate mpunga, safari hii huyo mwakili wao lazima tumkamate airport anajifanya kutumia passport ya Tanzania.
 
Dah! Nimekuelewa mkuu changamoto mlionayo ila kuwa mpole na mvumulivu ili sheria na katiba ''tuliyojiwekea'' kupitia Bunge ichukue mkondo wake kupitia tafsiri sahihi itakayotolewa na waheshimiwa ma-Jaji wa Mahakama Kuu itakayotupa mwelekeo wa kesho .
Jumatatu tunapeleka shauri mahakama ihamishie shauri lao Bariadi kwa sababu za kiusalama wakakae huko na majaji wao watuache tufanye biashara.
 
Jumatatu tunapeleka shauri mahakama ihamishie shauri lao Bariadi kwa sababu za kiusalama wakakae huko na majaji wao watuache tufanye biashara.

Hiyo sasa ndiyo hatua sahihi tunayotakiwa kujijengea utamaduni wa kwenda katika vyombo vya Mahakama au Polisi ili kupata haki ya amani na utulivu si kwa Mwanza tu bali hata kama changamoto hii ikitokea eneo jingine la Tanzania yetu.
 
. Kuna haja gan ya kutumia vurugu na watu kama mtaji wa kisiasa? Mbona kwenye maandamano huwa haibebi familia yake? Kwanini huwa anawachonganisha wananchi (wafuasi wake) dhidi ya Jeshi la Polisi kwa kufanya mambo ambayo ni kinyume cha sheria za nchi. Mnawadanganya wananchi budget ni mbaya itaongeza umasikini na wakati huo huo mliwahi kuipongeza kwa kusema ni ya kihistoria kwa sababu miradi ya maendeleo imechukua 40% ya budget yote. WAPINZANI UCHWARA WA NCHI HII HAMUELEWEKI NEVER!!
 
Jamaa umekomaa kweli, sasa ni hivi, hakuna mtu wa kuacha shughuli zake afanye maandamano.
Aulizwe tu ataandamana vipi wakati Polisi wamepiga marufuku mikutano na maandamano nchi nzima?

Au kwa kuwa anajua kwa kuwa tuna policcm, kwa hiyo wanaweza ruhusu maandamano hayo kwa kuwa tu yatakuwa yanawapinga wapinzani?!
 
Kuanzia Ijumaa kutakuwa na Maandamano ya kupinga mwenyekiti wa chadema kuendesha kesi Mwanza kwa sababu za kiusalama. Yeye anamatatizo yake na polisi kule kahama hajaenda kufungua kesi Tabora kaja kufungulia mwanza kama sio kuleta fujo za kijinga. Tutaandamana kuhakikisha anaondoka hatukubari kutuharibia mji wetu.

Watu waachwe wafanye biashara zao na shughuli za kujipatia kipato, siaende moshi arusha na dar aliko na wafuasi wengi, siakafungue kesi shinyanga mjini, kinachomleta mwanza ni nini kama sio kuleta fujo za hovyo tu, hapana. Sasa tutaandamana na kufurumusha wafuasi wake hadi nyashishi. Hatutaki ujuha.
Mtu ana haki ya kufungulia kesi popote anapoona inafaa!
Madai ya CHADEMA sio kuzuiwa mkutano wa kahama Bali mikutano yao yote kwa tishio la usalama!
Sasa wapi wakafungue kesi hiyo inatokana na convenience yao!
Na suala la mahakama halina maandamano hivyo kama cdm hawakubaliki Mwanza hamna haja ya kuwa na hofu, watakuwa wenyewe tu, nyie kaeni ndani ili hata wakianzisha vurugu wawe peke yao!
 
Ni Fujo Gani Mbowe alifanya Mwanza? Kwa Hiyo Maandamano ya Propaganda za Magufuli ni sawa Lakini ya Vyama Vingine ni haramu?. Mi Nasema Kuwa Kuna Rafiki yangu Mmoja amemsifia sana Magufuli akasisitiza apewe Uwenyekiti wa CCM. Ni haki yake kusema Hivyo, Ila Tunatofautiana, Mimi Niliamini Katika Mabadiliko Tanzania, Mabadiliko ya Kuboresha Huduma za Jamii, Mabadiliko ya Kuimarisha haki, Uhuru na Demokrasia, Kwa Mtazamo wangu Magufuli hana Uwezo wa Kuwa Rais, hana Hekima ya Ustahimilifu wa Kufikiri kwa Makini Kubeba Mzigo mzito wa Maamuzi magumu ya Nchi kwa Kutenda haki. Mimi Nilimpenda sana, Lakini Nilikuwa Chongo, Pamoja na Kuwa Magufuli ni Mchapakazi, asiyependa mchezo, Urais haumfai, anapenda sifa, anakurupuka na Ni dictator. CCM Walikosea Kumpa Tikiti, lakini Watakuwa Wametenda dhambi ya Mauti Kumpa Umwenyekiti. Lazima awepo wa Kumdhibiti huyo Mh.
 
Mbowe kama amefungua kesi Mwanza hakuna wa kumzuia kwa kuwa ni mtanzania. CCM Oyeee!
 
nani kakwambia mbowe ni mwananzengo wa mwanza? hatumtaki na wenje wake tumeshamtupa kule sijui anatutafutia nini huyu baba? hiyo kesi yake akaifungulie mahakama ya mwanzo ibinzamata, safari hii lazima ziumane tu tumechoka sasa.
Mwenye hekima hunyamaza akiwa hana la kusema
 
Taarifa Hujapata wewe kua Marufuku maandamano na mikutano. Kama unahamu ya kuandamana si usubiri huyo Mbowe akutetee huko mahakamani kwanza ili uruhusiwe! Au unataka kushindana na vyombo vya dola! Mikurupuko mengine hatari!
 
Kabisa huyu mtu anataka kuhalibu mji wa mwanza ...naunga mkono hoja

Kibwenzi,
Unaunga mkono baadhi ya wana Mwanza siku ya ijumaa wavunje ''amri halali'' ya polisi kupiga marufuku maandamano/shughuli zote zenye dalili za kisiasa nchi nzima au jiji la Mwanza halipo Tanzania?

Kumbuka CHADEMA ipo Mahakama Kuu jijini Mwanza kutafuta tafsiri ya Kikatiba kwa waheshimiwa Majaji wa Mahakama Kuu.

Ina maana hutambui mamlaka waliyonayo Mahakama Kuu kikatiba kusikiliza maombi ya watanzania wenzako au hata hutaki wasipate haki ya kujua tafsiri zenye utata?

Na kama waheshimiwa majaji wakikubaliana na CHADEMA kuwa wanahaki kikatiba ya kufanya shughuli za kisiasa bado mtapinga.
 
Ni Fujo Gani Mbowe alifanya Mwanza? Kwa Hiyo Maandamano ya Propaganda za Magufuli ni sawa Lakini ya Vyama Vingine ni haramu?. Mi Nasema Kuwa Kuna Rafiki yangu Mmoja amemsifia sana Magufuli akasisitiza apewe Uwenyekiti wa CCM. Ni haki yake kusema Hivyo, Ila Tunatofautiana, Mimi Niliamini Katika Mabadiliko Tanzania, Mabadiliko ya Kuboresha Huduma za Jamii, Mabadiliko ya Kuimarisha haki, Uhuru na Demokrasia, Kwa Mtazamo wangu Magufuli hana Uwezo wa Kuwa Rais, hana Hekima ya Ustahimilifu wa Kufikiri kwa Makini Kubeba Mzigo mzito wa Maamuzi magumu ya Nchi kwa Kutenda haki. Mimi Nilimpenda sana, Lakini Nilikuwa Chongo, Pamoja na Kuwa Magufuli ni Mchapakazi, asiyependa mchezo, Urais haumfai, anapenda sifa, anakurupuka na Ni dictator. CCM Walikosea Kumpa Tikiti, lakini Watakuwa Wametenda dhambi ya Mauti Kumpa Umwenyekiti. Lazima awepo wa Kumdhibiti huyo Mh.
Mistari yote hiyo hakuna hata neno Ufisadi...chadema hampingi tena ufisadi,ufisadi mmeupa mgongo....chadema mmekuwa chanda na pete na ufisadi...chadema nyinyi Mungu anawaona
 
Kweli kabisa naungana na mleta mada. Nimeungana naye kwasababu ameitetea hoja yake kwa point. Ama nyie bavicha jiheshimuni. Si kila jambo mnawahi kuhamaki na kuanza kutukana. Ivi ukitoa tu Maelezo bila kutukana unadhani hautoeleweka
 
usukuma unatoka wapi hapa? wacha kuhamisha hoja ya msingi? nani kakwambia wakazi wa mwanza ni wasukuma pekee, wenje mjaluo tulimpa ubunge kiwia mchagga tulimpa ubunge, huyu anayekuja kutuvunjia vioo vya magari hata kama ni mnyantuzu hapana, ujinga huo apeleke hukoo!
Gari lako aina gani? Kwanini usipeleke hoja hiyo mahakamani kama Kahama jiografia yake ya kimahakama ni Tabora? Hebu anzisha hayo maandamano yako ya kwenye keyboard tuone!
 
nani kakwambia mbowe ni mwananzengo wa mwanza? hatumtaki na wenje wake tumeshamtupa kule sijui anatutafutia nini huyu baba? hiyo kesi yake akaifungulie mahakama ya mwanzo ibinzamata, safari hii lazima ziumane tu tumechoka sasa.
naona unapalilia ukabila hapa. mwanza sio mji wako wewe binafasi bali wa watanzania wote.
 
haaa haaa natamani na wafuasi wa CHADEMA mwanza nao waanzishe maandamano ya kuunga mkono kesi hiyo ifanyike mwanza tuone faida ya kupinga kila kinachofanywa na wapinzani na hawa maccm. kumbukeni kama mnahaki ya kumpinga mbowe hata wafuasi wake wana haki ya kuwapinga nyinyi.
 
Back
Top Bottom