Maandamano ya CCM Moshi Mjini

Maandamano ya CCM Moshi Mjini

Eberi M. Manya

JF-Expert Member
Joined
Jun 29, 2011
Posts
743
Reaction score
280
Kuna Maandamano fake yanafanywa na CCM hapa Moshi mjini leo kuelekea kwa Mkuu wa Mkoa Amos Makalla.

10985934_525703864251695_7461679398022605224_n.jpg


Maandamano hayo yaliratibiwa na Davis Mosha mgombea ubunge wa chama hicho pamoja na wafuasi wake huku wakilalamika kwamba wanaonewa na kufanyiwa vurugu na chadema. Hali hii imewastua wananchi wote wa Moshi maana wanaofanya vurugu Moshi mjini ni Davis Mosha na wafuasi wake baada ya kubaini kushindwa uchaguzi siku ya tarehe 25 Jumapili hii.

Lengo kubwa la Davis Mosha na wafuasi wake ni kuvuruga amani ya Moshi na kuleta vurugu na kupandikiza chuki na kesi mbalimbali kwa wapinzani wao chadema ili uchaguzi uahirishwe siku hiyo.

Jambo linaloshangaza watu wengi hapo Moshi ni kwamba vurugu hizo za Davis Mosha na wafuasi wake wa CCM zimekuwa zikifanyika mbele ya jeshi la polisi pasipo jeshi hilo kuchukua hatua yeyote na kuonesha wazi kuwa wanamwuunga mkono Davis Mosha.

Kama uchaguzi huo utavurugika na kujawa na fujo na mivutano mikubwa, basii jeshi la polisi watakuwa ni wa kulaumiwa maana hawachukui hatua yeyote dhidi ya Davis Mosha. Inaoonekana polisi wapo pamoja na Davis Mosha na wafuasi wa CCM kuvuruga uchaguzi huu.

Pia Mkuu mpya wa mkoa Kilimanjaro Amos Makalla naye ameonesha kumwuunga mkono Davis Mosha pasipo kuangalia pande zote mbili. Mkuu huyo wa Mkoa ni kada aliyekubuhu wa CCM asiyejua mipaka ya mamlaka yake hasa wakati huu wa uchaguzi.

Davis Mosha amekuwa akiingilia mikutano za kampeni za Chadema na kuwapiga wafuasi wa chadema na hata kuzichana bendera zao mbele ya jeshi la polisi pasipo jeshi hilo kumchukulia hatua yeyote.

Wafuasi wa Chadema wameionya polisi na mkuu wa mkoa wasipochukua hatua madhubuti ili kuzuia vurugu hizo watajibu mapigo haraka iwezekanavyo, na kuwa wakijibu mapigo Moshi hakutakalika tena.

Wakazi wote wa msnispaa ya Moshi wanataka uchaguzi wa amani na utulivu ili haki ya kidemokrasia ichukue mkondo wake. Davis Mosha, Wafuasi wa CCM, Mkuu wa mkoa na viongozi wa CCM wasiwe sehemu ya kuvuruga mwenendo wa uchaguzi na kuleta fujo na adha zote hapa Moshi mjini. Tunawaomba waheshimu sheria na taratibu za uchaguzi.
 
Wakuu amani na iwe kwenu,

Naomba niweke wazi dukuduku langu hapa na sio kule kwenye complaints kwa sababu inaendana na Uchaguzi mkuu.
Kwa kweli kipindi hiki naona kila tukiweka mada zinazohusiana na haya mambo ya uchaguzi especially ukiwa unasapoti UKAWA, ni baada ya dk chache tu mada inahamishwa ama kufutwa kabisa, lakini za uongo na udhalilishaji za kuihusu ukawa zinaachwa bila kufanyiwa chochote..

Jf imenunuliwa?
Hata kama mmenunuliwa mtambue ya kuwa mnatuumiza sana.


Bila shaka hukumsikia mkurugenzi wa jF alipohojiwa na kusema Ccm wame invest sana kweny habari. Akasema mwanzni UKAWA wlaikuwa mbele sana hapa JF lakini sas Ccm wanaongoza.


Kwa hiyo kufutwa kwa threads za ukawa ni kuifaya ccm ionekane inaongoza kwa kuwa imetumia fedha nyingi kwenye vyombo vya habari.

Na kwa mantki hii, ninaona JF inakwenda kufa baada ya uchaguzi kwa sababu ya udhalilishaji ambao JF imeamua kuwafanyia wanaopingana na ccm.

Lakini haya yote si Ccm yetu asilia ni hii ccm ya kisasa. Inaua kila kiltu.

Hata hivyo tunakwenda kushndwa uchaguzi. Mimi ni Ccm na hili nimeliona kwamba tunazidi kuudhi wapiga kura kila siku, na kwamba hatuna uwzo wa kushinda uchaguzi huu. Hivyo tutakaa kando tujipange upya. Lakini hata wale wanaotufuata matakwa yetu, kama hapa JF, wasanii na vyombo vingine kama Star TV, wajiandae kukaa pembeni pamoja na sisi wakijipanga upya kwa sababu wamebeba nuksi zetu na tunawakokota kwenda tusikokujua.

Hawasalii salama hawa. Wala usiwe na hofu.
 
Huyo makalla na mosha ni marafiki walioshibana
 
Uwongo dhambi mashabiki wa ukwa wanafujo mno.
Anaye pinga ajitokeze kwa hoja.
 
Nilikua hapo kwenye mnara wa saa yakipita hayo maandamano, cha kushangaza raiya wote walioko pemben ya bara bara wanaonyehs alama ya chadema,
swali la kujiuliza, hivyo vipigo wanavyosema CCM kuwa wanapigwa vyote vinatokea kwenye mikutano yao na Polisi wakiwepo, RPC ameshindwa kazi?? mkuu wa mkoa hawezi kazi??
haya maandamano ni ya kumshtaki RPC na mkuu wa mkoa kitu ambacho ni kichekesho kwakuwa Mosha anaanzisha vurugu zote mbele ya askari na raiya wanajibu mapigo mbele ya hao-hao askari.

Juzi maeneo ya Rau Madukani nilishuhudia kada wa CCM akipatiwa kichapo mbele ya askari kwakuwa alikua anatoa bendera ya chadema mbele ya hao askari.
Jeshi la polisi linafumbia macho maovu ya ccm na kupelekea wafuasi wa upinzani kulipa kisasi mbele ya hao askari.
 
Kusanya evidence zithibitishe ni sahihi na kweli peleka kwa wakubwa wa mkoa.HATUTAKI MACHAFUKO...TUNATAKA AMANI NA UTULIVU.kama wakubwa hawatafanyia kazi ikifika mambo ya ICC itasaidia.
 
kazi ya wakuu wa mikoa ni kulinda maslahi ya CCM
 
Mosha kampeni zimemshinda, arudi nyumbani kwake Dar es salaam.


Jaffary hana mpinzani hapo Mo town.
 
Video za ccm wakichana bendera za ukawa zipo ni ushahidi
 
Kitu nilichokigundua watu wengi wa humu ndani wanatokea amma wa asili ya Arusha na KLM/Moshi
 
Video za ccm wakichana bendera za ukawa zipo ni ushahidi




14-300x194.jpg





[h=1]Tangazo Muhimu kuhusu upigaji kura[/h] Written by Abdul Zakinthos // 22/10/2015 // Ujumbe maalum // Hakuna maoni




Kuna taarifa kuwa,huenda kukawa na karatasi za kupiga kura feki,sasa sijui hili litasaidia vipi Chama tawala,lakini ni muhimu kukumbushana.


Unapoingia kwenye Chumba cha Kura,tafadhali weka kura yako juu kwenye muangaza kuangalia kama kutakua kuna nembo ya Tume ndani,kama haipo ,omba kura nyengine,itakuwa ni feki..
sambaza ujumbe kwa kila mtu
Ahsanteni
 
DAvis Mosha anaanza ku count loss na haoni kama kampeni zinalipa na ana opt kufanya mambo ya kitoto. Yeye avumilie asubiri kunyolewa bila maji siku ya Jumapili
 
Back
Top Bottom