Mkuu,
Wazo lako ni zuri, zuri sana!
Nani ata-coordinate maandamano hayo?
Nategemea jawabu ya, wote wanaochukia ubadhirifu wa mali za umma na ufisadi
Ugumu wa kulitekeleza wazo lako.(Kama nilivyosema ni wazo zuri,mimi naliunga mkono)
Katika Tanzania ya leo, nakusudia nchi ambayo wananchi wake wengi hawana elimu ya uraia(civic education) na hakuna juhudi za makusudi zinazofanywa ili kurekebisha udhaifu huu.kuwafanya watu watambue haki zao na wajibu wao kwa taifa.
Kwenye nchi ambayo muamko wa wananchi juu ya haki zao katika taifa ni mdogo sana.
Kwenye nchi ambayo kila mmoja wetu anasubiri mwenzake afanye, aanzishe jambo la kuwanufaisha wananchi wote.
Kwenye nchi ambayo serikali iliyopo madarakani kwa miongo zaidi ya minne inachukulia udhaifu huo nilioutaja hapo juu kama mtaji wa kukinufaisha kikundi kidogo cha jamii kumiliki, kuharibu, kujitwalia kila kitu,kurubuni mlalahoi wakati wa kura, vyombo pekee ambavyo tungetegemea vingefanikisha wazo lako ni Asasi za kiraia, vyama vya wafanyakazi, jumuia za wananchi, na vyama vya siasa.
Hapa sitaji,vyama vya wasomi na wanasheria kwani hivi kazi yao nikuitisha makongamano, warsha waalikwa ni wavaa tai na suti, si mlalahoi, kuandika magazetini, au kusubiri kuhojiwa watoe mawazo yao halafu wanakwenda zao bar kupata bia na kiti moto au soda na chipskuku, siku inakuwa imepita!
Asasi nyingi zinaanzishwa sio kwa lengo la kumnufaisha mwananchi. Mwananchi mlalahoi hutumiwa tu kama kisingizio cha kuombea fedha kutoka kwa mfadhili,wafadhili ili watu wamege donge nono,watunishe mifuko yao na fedha kidogo humfikia mlengwa na huwa geresha tu.
Sina nia ya kusema kuwa ni asasi zote ila majority ziko hivyo. Kwa hiyo asasi hizi hazitajibebesha jukumu hili la kuandaa maandamano ya amani kwa nchi nzima. Hali kadhalika jumuiya za wananchi na vyama vya wafanyakazi havina ubavu huo, ziko weak sana.
Kimbilio pekee ni vyama vya siasa vya upinzani. Vyama hivi vikiamua,vikiweka manunguniko ya wananchi na maslahi ya taifa mbele vinaweza kuthubutu kuitisha maandamano kwa nchi nzima. Ni bahati mbaya kuwa havijitambui kuwa maslahi ya taifa ni superior kuliko kujitangaza kichama. Kukosekana kwa ujasiri na utashi kwa vyama hivi kuwa na sauti ya pamoja katika kuiwajibisha serikali inayokumbatia uoza,ufisadi,ubadhirifu wa mali ya umma ni ufinyu wa mawazo wa viongozi wa vyama hivyo.
Tusitegemee CCM kuitisha maandamano ya nchi nzima kuitaka serikali iwajibike kwa wananchi.
Lakini hili la vyama vya upinzani kushindwa kufanya hili ni uwendawazimu. Kama lugha hii ni kali basi niseme viongozi wa vyama vya upinzani wana muono finyu kama vyama vya siasa.
Wao wanapokuja kuomba kura hutuambia tuwachague ili wakatutumikie, wakatuwekee mambo sawa, ok, siku ya kushika hatamu haijafika lakini wanataka tuamini kuwa hata ku-coordinate na ku-organise maandamano ya wananchi kwa nchi nzima kunawashinda ?
Ubinafsi wa kila chama kuwa kinataka kionekane kuwa ndio chama dume,chama kikuu cha upinzani kisiwe kikwazo cha kushirikiana katika mambo, au jambo linalowaunganisha wananchi wote.
Mkuu, mchango wangu katika kuunga mkono wazo lako, ni kuwaomba wanaJF ambao wanaweza kupata sikio la hawa viongozi wa vyama vya upinzani wawapitishie ujumbe huu. Halafu baada ya miezi mitatu tuone kama watapata utashi na ujasiri wa kuja pamoja kama nguvu moja itakayowakilishia vilio vya wanyonge.
Kama wao watashindwa, kwa mazingira ya Tanzani yalivyo hii leo, basi kuitisha maandamano ya nchi nzima itabaki kuwa ni ndoto. Hatuko tayari, bado jamii inapiga mbonji ! na kukoroma.