Filipo
JF-Expert Member
- Jan 6, 2011
- 9,347
- 5,555
Jiji la Arusha litapata mtikisiko wa maandamano asubuhi hii yatakayoanzia Majengo, kuzunguka viunga mbalimbali vya jiji, hatimae kuishia uwanja wa Sheikh Amri Abeid Kaluta. Maandamano hayo yameandaliwa na umoja wa waongoza watalii, Tato, na yataongozwa na Waziri Nyalandu. Lengo lake ni kupinga mauaji ya Tembo nchini.
Itakumbukwa kwamba mauaji ya tembo yamekuwa ni janga hapa nchini tangu uongozi mpya wa Chama cha mapinduzi uingie madarakani na licha ya watuhumiwa mbalimbali kutajwa, akiwemo Katibu mkuu wa chama hicho, bado takwimu zinaonesha Tembo mmoja anauawa kila siku nchini na itakapofika mwaka 2025 Tembo watakuwa historia hapa nchini.
Nawasihi wakazi wa Arusha na maeneo ya jirani kujitokeza kwa wingi kushiriki maandamano haya na kulaani kwa nguvu zote mauaji ya Tembo wetu!
Itakumbukwa kwamba mauaji ya tembo yamekuwa ni janga hapa nchini tangu uongozi mpya wa Chama cha mapinduzi uingie madarakani na licha ya watuhumiwa mbalimbali kutajwa, akiwemo Katibu mkuu wa chama hicho, bado takwimu zinaonesha Tembo mmoja anauawa kila siku nchini na itakapofika mwaka 2025 Tembo watakuwa historia hapa nchini.
Nawasihi wakazi wa Arusha na maeneo ya jirani kujitokeza kwa wingi kushiriki maandamano haya na kulaani kwa nguvu zote mauaji ya Tembo wetu!