Wana jf, leo nilikuwa nasikiliza RADIO FIVE ya Arusha wananchi wenyewe bila kiongozi wa chama chochote wameazimia kuandamana hadi kwa Mkuu wa Mkoa wa Arusha kwa tarehe tajwa. Lengo la maandamano hayo ni kudai UMEME. Kwa mujibu wa wananchi walioohojiwa, maandamano hayo hayatahusisha chama chochote ili kuepuka kile kinachoitwa lawama kwa baadhi ya vyama hasa vya upinzani. Maandalizi yanafanyika kwa kutafuta kibali na hata kibali kisipopatikana wataandamana hata damu ikamwagika. Nafikiri ni kusubiri tuone.