Maandamano maandamano maandamno

Maandamano maandamano maandamno

Mchaga 25

JF-Expert Member
Joined
Oct 29, 2011
Posts
464
Reaction score
114
Hakika muda ukifika hakuna kurudi nyuma, wadau wana wataifa wapenda maendeleo, wapendahaki, wanaharakati, wanaJF, WANAFACEBOOK, WANACCM, WANACHADEMA, WANANCCR, WANACUF, wanamapinduzi wake kwa waume tujitokeze ijumaa saa 3 asubuhi katika maeneo haya mlimani city, ubungo mataa, tazara, magomeni, sayansi, mbagala mwisho, mtoni kwa azizi ally, kimara mwisho kupinga ufedhuli na ubazazi wa nchi hii mimi na mwanangu tutakuwepo, hakika sina cha kupoteza kwani baba na babu wamepoteza miaka 50 iliyopita ni waktai wa kuandika historia mpya.

Ukoloni mamboleo hauna nafasi Tanzania.
 
tuweke wazi maana na mimi nina safari ya kuja huko kama ni sababu ya msingi nitajiunga nanyi....msiliweke pembeni swala la posho za wabunge na mgomo wa madr
 
Wananchi wa tanzania wana upungufu wa akili mwilini! Mbunge analipwa 330 a day?mpo mmenyamaza?umeme mmepandishiwa mpo mmenyamaza?viongozi wanakula nchi mmpo mmenyamaza?dah hii shida kweli na kamwe hamuezinkwenda mahala, mtakuwa watu wa kuachwa kila sector!
 
huyu katoka usingizini au kaamuka nazo, c unajua siku hizi komputer zetu ni simu
 
Mi naona maandamano yafanyike siku ya jumapili ili watu wa intelligensia wasiseme eti watu watabughudhiwa makazini na kuhatarisha amani. Tuvaeni magwanda twende vitani kwanza wanachi tuko wengi kuwashinda hao mffu kila mtu awe chupa ya maji mkononi tuone kama hayo mabomu ya machozi yatafanya kazi
 
Wewe ni nani unataka Watanzania waandamane?
Niulize mimi ni nani ninayetaka kuandamana, raia wa nchi, ninayeteseka kwa kulipa kodi na sioni matunda yake, ninaye pinga nchi yangu kugeuzwa shamba la bibi, ninayepinga kuongezwa posho za wabunge, malipo ya dowans, kupanda kwa umeme, ninayepinga wizi wa kiwira, ninayepinga kujazana kwa watoto wa vigogo serikalini, ninayepinga taxi holiday kwenye mahotel, ninayepinga kuchelewesha mikopo kwa wanafunzi, ninayepinga huduma mbaya za elimu, afya na maji, ninayepinga safari nyingi za JK, ninayeunga mkono migomo ya wafanyakazi, ninayepambana na mchuzi bata kama wewe! Je wewe ni nani ambaye usiye taka tuandamane
 
tuweke wazi maana na mimi nina safari ya kuja huko kama ni sababu ya msingi nitajiunga nanyi....msiliweke pembeni swala la posho za wabunge na mgomo wa madr
Mkuu kama kweli una uchungu na hii nchi utahudhuria
 
Yaani Madakitari wamefanikiwa kuitisha mgomo wa nji nzima; na sisi wananji tungelikuwa na mshikamano maandamano nji nzima sidhani kama kuna bomu la machozi litakaloruka.

mbona Serikali walishindwa kurusha mabomu au kutumia nguvu katika Mgomo wa madreva wa malori uliofanyika Mwezi October 2011 na huu wa mwezi january 2012???

mwezi october Kule Tunduma Polisi walikimbia pamoja na gari lao la maji washa na mabomu yao, wakawatishia waandishi wa habari wasitoe habari hiyo pia na picha zilizoonyesha polisi wakitoa mbio zisiwekwe katika magazeti. lakini madreva walikuwa na ushirikiano.

TUKIAMUA TUNAWEZA KUMUONDOA ADUI HUYU MNYANYASAJI NA MUUAJI WA RAIA!!!!!

MIZAMBWA
INANIUMA SANA!!!
 
wewe ni nani unataka watanzania waandamane?

kasafishe meno ndo maana na maneno unayotoa ni machafu!upeo wako wa mambo mchafu yani kila kitu kichafu!kipato cha mtanzania ni 770,000.00 kwa mwaka mbunge anapata 660,000.00 kwa siku mbili!hizi akili matope!amkeni nyie vipofu na viziwi! Mnafikiri kutumia nini?
 
Niulize mimi ni nani ninayetaka kuandamana, raia wa nchi, ninayeteseka kwa kulipa kodi na sioni matunda yake, ninaye pinga nchi yangu kugeuzwa shamba la bibi, ninayepinga kuongezwa posho za wabunge, malipo ya dowans, kupanda kwa umeme, ninayepinga wizi wa kiwira, ninayepinga kujazana kwa watoto wa vigogo serikalini, ninayepinga taxi holiday kwenye mahotel, ninayepinga kuchelewesha mikopo kwa wanafunzi, ninayepinga huduma mbaya za elimu, afya na maji, ninayepinga safari nyingi za JK, ninayeunga mkono migomo ya wafanyakazi, ninayepambana na mchuzi bata kama wewe! Je wewe ni nani ambaye usiye taka tuandamane

Nimeuliza wewe ni nani unaetaka Watanzania waandamame? Sijakuambia wewe usiandamane! Sasa uoni kama unatwanga maji kwenye kinu, watu hawakujui wewe ambae ndio kiongozi wa maandamano unaandika huku umejificha kwenye Laptop. Jitokeze watu wakujue mkuu.
 
Nimeuliza wewe ni nani unaetaka Watanzania waandamame? Sijakuambia wewe usiandamane! Sasa uoni kama unatwanga maji kwenye kinu, watu hawakujui wewe ambae ndio kiongozi wa maandamano unaandika huku umejificha kwenye Laptop. Jitokeze watu wakujue mkuu.
majibu : raia wa nchi, ninayeteseka kwa kulipa kodi na sioni matunda yake, ninaye pinga nchi yangu kugeuzwa shamba la bibi, ninayepinga kuongezwa posho za wabunge, malipo ya dowans, kupanda kwa umeme, ninayepinga wizi wa kiwira, ninayepinga kujazana kwa watoto wa vigogo serikalini, ninayepinga taxi holiday kwenye mahotel, ninayepinga kuchelewesha mikopo kwa wanafunzi, ninayepinga huduma mbaya za elimu, afya na maji, ninayepinga safari nyingi za JK, ninayeunga mkono migomo ya wafanyakazi, ninayepambana na mchuzi bata kama wewe! Je wewe ni nani ambaye usiye taka tuandamane watanzania kuwandamana , ok ngojea niangalie IP yako
 
Back
Top Bottom