jack;
unasema wazazi wote wanajua kinacho endelea tangu uchumba!! Ni mzazi yupi aliyekufundisha kwenda kutoa pichu yako kabla ya ndoa??
Nakusihi, usimruhusu mzazi yeyote akushauri tena hapo. Wazazi wanangojea ushushe mzigo tu waangalie. Omba sana Mungu, mtoi awe salama, wajua ninachokisema, akija na katatizo kidogo tuu, ni mzigo wako weye na mamako tu. Hutamwona mtu hapo.
Ushauri; Kama anakujali, anakutunza na siku moja moja anamwongezea mtoto sikio.... we wajua nisemalo. Tulia tuli, ukijifungua, asikujue tena mpaka pete ya ndoa hadharani. Mwambie Bahati mbaya huja mara moja tu hairudii ikirudia ni mazoea. Niliwahi kumshauri binti mmoja akadhani miye naota tu. Leo ana watoi 4 na pete bado. Juzi kati kaja kwangu, jamaa kampandishia zogo kweli kweli mpaka likawa timbwili. Jamaa kakomaa kuwa alimkuta mtu ndani ya nyumba mchana peupe. Kumbe uongo ni mtu anataka kukwepa majukumu.
Usiwalete wazazi wala marafiki hapo. Uamuzi unao weye tu