Maamumzi ya Mchakato wa Katiba Mpya ni ya Wananchi au Rais? na pesa anatoa Rais au Wananchi?

Jimmy_Msukuma

Senior Member
Nov 1, 2018
153
181
Wanabodi,

Katika mambo aliyojadili jana Mh. Rais Magufuli ni kwamba, alikiri kuwa Wananchi wanahitaji Katiba mpya, akasema hilo kwasasa sio kipaumbele chake na hatotoa Fedha ili watu wakalale Bungeni.

Kauli hii ina mambo 4:
1. Anakiri kwamba wananchi waliompa Urais wanahitaji Katiba Mpya
2. Maamuzi ya Mchakato wa Katiba Mpya ni yake
3. Pesa anatoa yeye.
4. Hatotoa kwasababu Wabunge hulala (hawafanyi kinachowapeleka Bungeni).


Namba 2 kwakweli sio kweli, maamumuzi ua Mchakato wa Katiba Mpya ni ya Wananchi, Rais ajue anatumikia Wananchi. Namba 3 sio kweli kwamba Pesa za kuendesha mchakato anatoa yeye, Pesa ni kodi za wananchi, hivyo Pesa ni za wananchi wenyewe, yeye ana dhamana tu. Namba 4, kwakweli Rais ameridharau Bunge kwa kupuuza shughuli za wabunge, kwamba muda mwingi wanautumia kulala etc, hivyo hatotoa mwanya huo. Mbona vikao na mambo mengine Bunge hutengewa pesa? Je, wakati wa mchakato uliopita Wabunge walilala?

Hadi sasa nashindwa nimpe hadhi gani Mh. Rais Magufuli: Je, amelewa madaraka? Je, yupo juu ya mihimili mingine? Je, ni kweli hakuna walezi wengine wa Taifa zaidi yake, hadi atoe toe kauli waziwazi za kuashiria yeye ndio mwenye kauli ya mwisho?

Nawasilisha.
 
Haya ndio matokeo ya kufanya maamuzi yaliyojaa ushabiki kupindukia matokeo yake tunapata rais kichaa kama alivyowahi kukiri mwenyewe kwa kinywa chake
 
Achen ujinga. Mwamuzi wa mwisho wa nini kifanyike nchini ni rais. Kesha waambia hicho sio kipaombele kwake. Anasimamia pesa kwenda kwenye mambo ya maendeleo.

Namuunga mkono.
 
Huo ndio ukweli. Uamuzi wa kila kitu katika nchi hii anao yeye na sio wananchi. Pesa zote za hazina ziko chini ya uamuzi wake, zinatumika anavyotaka wala sio kufuatana na bajeti iliyopitishwa na bunge. Neno lake ndio sheria kwa kuwa yeye yupo juu ya sheria. Kulingana na yeye katiba haina umuhimu wowote mradi yupo madarakani, hata kama kuna uharibifu wa kununuliwa wabunge na madiwani na kupoteza pesa za walipa kodi kwa chaguzi feki. Hata hilo haoni linaweza kutatuliwa na katiba mpya?
 
Safi hata kama ni mimi sitoi hela
Waendelee tuu kulala mpaka masiha atakaporud
 
Tatizo wabongo ni wavivu sanaaa wanapenda kunyonga vya kuchinja hawataki sasa dawa ni moja tuu mpaka mnyooke
Speed 150kph ukishindwa ruka dirishan hulazimishwi mzee hili bus ni nooomaa
 
Tanzania na baadhi ya nchi zingine za kiafrica ni ngumu sana kupata maendeleo ni kwasababu tuna amini ktk kupewa na sio kutafta.
Nasema hivi kwasababu wengi wetu hatujui kudai haki zetu
 
Back
Top Bottom