Maalum kwa wanaume waliolelewa na mama tu

Maalum kwa wanaume waliolelewa na mama tu

stable woman

JF-Expert Member
Joined
Nov 12, 2013
Posts
3,883
Reaction score
4,484
Habari wandugu wa jukwaa hili.

Wajameni nimeambiwa na kusikia tabia walizonazo wanaume wengi waliolelewa na mzazi mmoja hasa Mama.

Kuwa ni wanaume wanaojali na kuthamini wake zao japo sijathibitisha hili.

Wengi wao nimegundua ni watu wakudeka sana, wapo legelege sio wakamavu pia wanasumbuliwa na tabia ya kununa kuna.

Hili nimelithibitisha hata kwa mashemeji zangu.

Naomba nilete hili mezani tuchangie kwa pamoja nifahamu nisiyoyajua mengine.

Asanteni
 
Mimi Nina case 3 za watu Wa dezine hiyo,,, sifa zao ni:-

1.Vitombi aooo!!
2.AF wapo free sana
3. Wana zali la hela sana
Etc.
 
Hii inategemea Ntu na ntu!
Kwani kudeka kukoje?
 
Inategemea na aina ya mzazi mi Nina mamaangu mkubwa analea wanae wakiume watupu wanne.Aaisee hamna kudekeza watt wala nini zamu za kupika km kawa,na deki wanapiga so inategemea sana jinsi walivyolelewa.
 
Pamoja na ukweli kwamba wapo strong women wanao lea watoto vizuri bila kudekeza ila bado huwa upungufu unakuja kuonekana tu. Malezi ya baba yana nafasi yake pia hata mama akiwa smart vipi. Mimi nilishaona tatizo la kutokuwa na msimamo as a man. Mara nyingi hawa watu huyumbishwa na saa nyingine huwa hawawezi kutoa final decision yeye kama yeye bila kushauriana na watu wengine. Na sometimes hawa watu hukosa sauti kama watawala katika familia zao. Ila hii si applicable kwa wote ila wengi wao ambao nimeshawahi ishi nao na kuwashuhudia wana hivyo vi chembe chembe
 
Leo nimeona generalization ya jf, mimi nawafahamu wengi na wapo tofauti na unachoandika hapa.
 
Sidhani,anyway ni tabia ya mtu binafsi. Mimi nimelelewa na mama(mzee alirip nikiwa kwa tumbo),alafu ni last born ila hakukua na kudeka wala nini,maza alitulea kwa mkono wa chuma maana tulikua madume tu vinginevyo tungemshinda.

Niko strong sio lege lege,sinuni nuni ila nina hasira nyingi sana. Hao mashemeji zako ni tabia yao tu. Kuhusu kujali na kuthamini mke sijui maana sijaoa.
 
Habari wandugu wa jukwaa hili!
Wajameni nimeambiwa na kusikia tabia walizonazo wanaume wengi waliolelewa na mzazi mmoja hasa Mama!
kuwa ni wanaume wanaojali na kuthamini Wake zao japo sijathibitisha hili!

Wengi Wao nimegundua ni watu wakudeka sana, wapo legelege sio wakamavu Pia wanasumbuliwa na tabia ya kununa kuna! Hili nimelithibitisha hata kwa mashemeji zangu! Naomba nilete hili mezani tuchangie kwa pamoja nifahamu nisiyoyajua mengine!

Asanteni

Sio wote ila wengi wako hivyo. Na wanaume waliozaliwa peke yao kwenye familia huku wakizungukwa na wadada wengi wakoje?.
 
Kuna ka ukweli...
Uzuri wao hawana mfumo dume...
Wana respect sana wanawake...
Ila wanadeka...hii si kasoro as long as uko tayari kudekeza...
Na kama wataoa (maana wengine wagumu kuoa) basi wana work hard kuhakikisha hawaigi tabia ya baba zao (watoto wao hawalelewi na single parents) - nikiwa na maana hawataki ku repeat mistakes za wazazi wao...

(naongelea expiriensi)
 
Mmmmmmmh! Jamii nayo kwa ubaguzi! Mbona Obama kalelewa na mama tu na hayupo hivo?

Nashauri usome Edwin Mtei's From Goatherd to Governor (Mchunga Mbuzi hadi Gavana wa Benki Kuu) . Mwasisi wa CHADEMA, chama kinachotarajia kuchukua DOLA, naye alilelewa na mama tu. Nimempigia simu kumwaririfu na kumsomea thread hii, akanijibu HAKUNA KULALA MPAKA KIELEWEKE ifikapo Oktoba 2015.
 
We unamjuaje Obama? Michele analalamika, wewe unasema hayuko hivyo, we nani kwa Obama. Acha ujuaji usichokijua.Ungezungumzia watu uliokaribu nao ningeafiki mchango wako, lakini Obama katika social events, family issues. Hapana sio kielelezo kizuri
Mmmmmmmh! Jamii nayo kwa ubaguzi! Mbona Obama kalelewa na mama tu na hayupo hivo?
 
Pamoja na ukweli kwamba wapo strong women wanao lea watoto vizuri bila kudekeza ila bado huwa upungufu unakuja kuonekana tu. Malezi ya baba yana nafasi yake pia hata mama akiwa smart vipi. Mimi nilishaona tatizo la kutokuwa na msimamo as a man. Mara nyingi hawa watu huyumbishwa na saa nyingine huwa hawawezi kutoa final decision yeye kama yeye bila kushauriana na watu wengine. Na sometimes hawa watu hukosa sauti kama watawala katika familia zao. Ila hii si applicable kwa wote ila wengi wao ambao nimeshawahi ishi nao na kuwashuhudia wana hivyo vi chembe chembe

Umefunguka vyema mkuu! Big up
 
Back
Top Bottom