Mtoa taarifa acha upotoshaji wewe,Kwamba wilaya haina Hospital ya Wilaya huu ni uongo.Ipo Hospital kubwa na yenye hadhi ya hali ya juu pengine tofauti na Wilaya nyinginezo.Sema tu hospital hiyo ni designated kwa maana ni ya Kanisa na inaendeshwa na Serikali.Kwa kifupi Hospital ipo,tena si moja bali ni Mbili zenye utaratibu huo.(Huruma na Ngoyoni).Vituo vya Afya pia vipo kila Tarafa na vyenye uwezo mzuri.Ukarabati wake umekuwa ukifanyika kila mara.
Mahakama ipo tena imekarabatiwa hivi karibuni,Magereza ipo ya kawaida na yenye hadhi kuliko Magereza mengine kama ya Korogwe,Mwanga na kwingineko,
Kituo cha Polis kipo walau hakipo vizuri sana lakini kinakidhi.
Hivyo utoe taarifa zenye uhakika.usitubabaishe.
Toa sifa pia kama shule kuwepo nyingi,na watu kujituma katika uzalishaji.
Tatizo kubwa ni Maji yasiyo ya uhakika kwa hapa Rombo na hasa wakazi wa tambarare wanataabika sana maji.