Maajabu ya Mji wa Chato

Maajabu ya Mji wa Chato

Kila kiongozi angekuwa anafanya hivyo home kwake nadhan tz ingekuwa kama Kwa Trump vile

Viongozi hawajazaliwa mijini,wamezaliwa vijijini,lakn,ukienda hata barabara ya kuingilia kijijin kwake hakuna

Hongera mjomba

Sent using Jamii Forums mobile app
Naunga mkono hoja yako..... maana mkataa kwao ni mtumwa.

Sent from my Siemens kidole juu using JamiiForum mobile app.
 
Wa-Tz bana, mtu akijenga kwao anasemwaaa, asipojenga anasemwaaa!!!

Lipi bora?

Bora tule wote, kujenga home ndo uwajibikaji! Viongozi wapuuzi na wabinafsi hawakumbuki kwao.

JPM, has done well. Wengine waige kwao. Nilipitaga jimbo la aliyekuwa waziri wa kilimo Eng Chiza huko Kakonko, pabayaaaaaa utafikiri ni njia ya kuelekea jalalani huku jamaa linaishi Dar! Nikapita jimbo la Lukuvi, nako hovyo tu....

Sasa lipi bora???

Sent using Jamii Forums mobile app
Shangaaa wewe.
kweli kuongoza Tz ni sawa na kubeba gunia la misumari na vipande vya chupa....
lol

Sent from my Siemens kidole juu using JamiiForum mobile app.
 
Jamani picha mbona zipo nyingi tu page ya kwanza ya huu uzi.
 
Katika pilika za hapa na pale, basi nikafanikiwa kufika chato baada ya muda mrefu toka mara ya mwisho nlivyofika mahala hapa. Yafuatayo nimepata kuyaona kidogo:

Kati kati ya mji huu kuna mataa ya kuongozea magari barabarani, taa hizi ni kituko kidogo maana zinakusubirisha wakati hakuna magari mengine au watu wanaopita, yaan unaweza kujikuta uko tu mwenyewe na unasubiria tu taa zi ruhusu. Naam wale wa mikoa kama morogoro pamoja na umaarufu wa mkoa wake ila mataa kwao ni habari nyingine, hakuna kabisa kwaio hapa wanaweza wasinielewe.

Mitaa yote ya mji huu ina barabara za lami, ni karibu asilimia 90 mkeka tu, kuanzia za kati ya mji mpaka mitaani.

Wakazi wa huku kama nao wanajiona waTanzania namba moja, yaani kiburi kiburi hivi.

Barabara nzuri ila baiskeli zimetawala kweli kweli, anyway nyie wa rorya hapa mnaweza msinielewe au nyie we marinyi barabara mbovu wilaya nzima, kwaio naombeni utulivu wenu hapa.

Hospitali za mji huu ni full air conditions tu, kipupwe safi kabisa, na sijaona vihospitali kama sinza, Sijui temeke au wapi huko bado sanaa, kimiundo mbinu kwa hospital za chato.

Majengo ya serikali ni nadhifu na mazuri sanaa, yanavutia ata kuyatazama tu.

Kuna ulinzi mzuri tu, migambo wamejaa kila mtaa na wanachokera wanajifanya ni matrafic wanakamata hadi magari, sijui mamlaka haya wameyatoa wapi.

Kuna airport karibuni itaanza kutumika, japo ukiwaangalia wananchi tu walio wengi kwa kweli labda nauli zishushwe.

Wakuu tukumbuke kujenga vijijini kwetu ni muhimu sanaa. Ni haya machache tu na ndio nliyoyaona kwaio nisije kupangiwa vya kuona na kusema.
nyumbani kwa rais na waziri wa muda mrefu serikalini miaka ya nyuma. Tujifunze kujenga kwetu tupatapo fursa
 
jamaa anatumia vibaya sana pesa zetu anaweka mataa kuongoza baiskeli barabarani

mwisho wa siku pia atawasafirisha bure kwa ngege
 
Watu waongo! Dah! Eti zahanati na hospital in full kiyoyozi, lami ya mjini hata Km 3 hazifiki, anyway n mawaza na maono yako.
 
Barabara nzuri ila baiskeli zimetawala kweli kweli, anyway nyie wa rorya hapa mnaweza msinielewe au nyie we marinyi barabara mbovu wilaya nzima, kwaio naombeni utulivu wenu hapa.



Basi hizo ndizo ziwekewe utaratibu wa kutumia hayo mataa ili nishati isikwishe bure
 
jamaa anatumia vibaya sana pesa zetu anaweka mataa kuongoza baiskeli barabarani

mwisho wa siku pia atawasafirisha bure kwa ngege

Waende wapi tena na ndege? Ila Tanzania ni moja, hamia chato mkuu
 
chuo cha afya chato.
CHATO_INDEX.jpg
 
Back
Top Bottom