Maajabu ya Magomeni Mapipa

Maajabu ya Magomeni Mapipa

pilau

JF-Expert Member
Joined
Aug 16, 2012
Posts
1,595
Reaction score
450
Haya ni maajabu ambayo wengi wetu hatujayaona.

Kama umekuwepo maeneo ya Magomeni Mapipa nyumba zoooote za za zamani zilizojengwa miaka ya '60 na '70 foundation ya nyumba hizo ni ndefu sana.

Sasa fikiria Magomeni Mapipa wazee wa kizaramo waliona athari za maji na mafuriko ndio maana nyumba nyingi zimejengwa kwa tahadhari kubwa sana na kuwa na misingi iliyonyanyuka.

Nilipomuuliza mmoja wa wazee wa Kizaramo alinijibu kwamba wao maeneo mengi ya Dar walikuwa wanaona kuwa ni mashamba ya kulima mpunga na kuvua samaki lakini hao waliotoka huko walikotoka wakalazimisha kujenga maeneo ambayo hayakustahili kujengwa nyumba bali ni mashamba ya mpunga na sehemu ya mabwawa ya kuvulia samaki aina ya kamambare leo huko kote ni majumba... mafuriko kede kede.

Haya ndio maajabu ya magomeni mapipa na hutasikia mafuriko.
 
Maajabu au ajabu la Magomeni msingi mirefu ya nyumba.?

Nahisi Tanzania tumeishiwa Maajabu Maana hata Magari ya mwendo kasi wataita Maajabu
 
Na ikumbukae nyumba za Magomeni hazikujengwa na mtu binafsi, zilijengwa na National Housing Corporation. Ndio maana ziko imara na zimedumu zaidi ya miaka 40 sasa, tena bila kufanyiwa ukarabati wowote. Zilijengwa kitaalam sana zile
 
Bwana pilau, hayo ndo maajabu? Wazaramo kujenga nyumba za msingi mrefu? Kwamba wazaramo hamna kitu?
 
Hata sinza wakati mzee mwinyi anaibgia madarakani palikua panalimwa mpunga
 
si mzaramo wala msukuma mwanza au mnyakyusa wa mbeya au mmasai wa arusha hakuna tofauti na duniani kote miji au inchi zilizoendelea ni matokeo ya mchanganyiko
 
Hivi Magomeni Mapipa inaanzia wapi na kuishia wapi.
 
..... Haya ni maajabu ambayo wengi wetu hatujayaona ... kama umekuwepo maeneo ya magomeni mapipa nyumba zoooote za za zamani zilizojengwa miaka ya '60 na '70 foundation ya nyumba hizo ni ndefu sana.... sasa fikiria Magomeni mapipa wazee wa kizaramo waliona athari za maji na mafuriko ndio maana nyumba nyingi zimejengwa kwa tahadhari kubwa sana na kuwa na misingi iliyonyanyuka.... nilipomuuliza mmoja wa wazee wa Kizaramo alinijibu kwamba wao maeneo mengi ya Dar walikuwa wanaona kuwa ni mashamba ya kulima mpunga na kuvua samaki lakini hao waliotoka huko walikotoka wakalazimisha kujenga maeneo ambayo hayakustahili kujengwa nyumba bali ni mashamba ya mpunga na sehemu ya mabwawa ya kuvulia samaki aina ya kamambare leo huko kote ni majumba... mafuriko kede kede.. haya ndio maajabu ya magomeni mapipa na hutasikia mafuriko

Kwamba Magomeni Mapipa walikaa Wazaramo watupu!! Besides hayo ndiyo umeona maajabu?
 
Na ikumbukae nyumba za Magomeni hazikujengwa na mtu binafsi, zilijengwa na National Housing Corporation. Ndio maana ziko imara na zimedumu zaidi ya miaka 40 sasa, tena bila kufanyiwa ukarabati wowote. Zilijengwa kitaalam sana zile

pia ilikuwa ni ramani na plan ya mkoloni iliyokuja kutekelezwa na nyerere chini ya NHC,lakini pia zipo zilizojengwa na watu binafsi ambazo zilikuwa ni ghali kuliko NHC na zingine ni za mawe na udongo na zipo mpaka leo na ni imara.Halafu M.Mapipa kuna mtaa wa kipekee ambao Tanzania nzima hakuna mtaa kama huo.Magomeni ndio sehemu alipopokelewa nyerere wakati wa kutafuta uhuru na barabara nyingi za magomeni zilikuwa za kisasa zilijengwa enzi ya mkoloni lakini tangu tupate uhuru hazijakarabatiwa ila leo naona wanajaribu kujenga zile za halmashauri.tena ni tatu ile ya mikumi i kama unaenda kwa sh.yahya ,ya mzimuni kupitia mnymkuu kuelekea njia ya jangwani na idrisa kutokea moroco hotel.lakini sehemu zote zimegeuka mashimo ila maji hayaingii ndani ya majumba sababu ya ujenzi wa kisasa wa nyumba za magomeni.ni miongoni mwa miji ya kisasa ila cha ajabu magomeni hakuna shule ya kata ya sekondari wanatumia kwa pamoja na kata ya ndugumbi.kiwanja cha wazi cha pekee wakazi waliomba kujengea shule magamba wamekataa wamepageuza BAR na wana mpango wa kujenga club,watu wanakunywa na kulikuwa na kelele za music wananchi wakaja juu siku hizi haman makelele kuna pombe mwanzo mwisho ndo hiyo garden breeze upande wa kushoto ukitoka kinondoni kituo cha hospital
 

3344567.jpg
 
Du umeniwahi mleta mada hili halijui na aliemuuliza sio mwenyeji wa magomeni asante mkuu.
Na ikumbukae nyumba za Magomeni hazikujengwa na mtu binafsi, zilijengwa na National Housing Corporation. Ndio maana ziko imara na zimedumu zaidi ya miaka 40 sasa, tena bila kufanyiwa ukarabati wowote. Zilijengwa kitaalam sana zile
 
Back
Top Bottom