engmtolera
JF-Expert Member
- Oct 21, 2010
- 5,150
- 1,437
- Thread starter
- #41
arifu suala hili lipo mahakamani halipaswi kuzungumziwa......
duuu
sasa hii ni kali kwa kweli,haya bwana ngoja tuongelee ya kenya ambayo hayapo mahakamani
arifu suala hili lipo mahakamani halipaswi kuzungumziwa......
Waeleze waelewe maana ya ushirikiano wa Afrika mashariki ni nini? hauwezi kuitangaza Tanzania pekee ukapata wageni,kwanza kiwanja kikubwa cha ndege hatuna hizo terminal 2 za Mwl Nyerere Int. airport hazitoshi kurupushani ya ndege Kenyata int. airport zipo terminal kama 100 wageni wanaingia na kutoka kwa wingi,mashirika mengine makubwa ya ndege hayatui Dar kutokana na ufinyu wa uwanja,hiyo hata hao wanaoitangaza TZ wageni wakija wanatua Kenya ndiyo wapande Precision air kuja Tz,haidhuru wakiitangaza serengeti au kilimanjaro wageni hawaishii kenya ni lazima wavuke mpaka kuja Tz tabu iko wapi?,Kenya wana shirika lao Kenya Airways sisi letu liko wapi?unategemea walete wageni mpaka Dar kwa faida ya nani?hiyo Kilimanjaro Airport ndiyo usiseme hata sehemu ya kurukia ndege mashimo matupu bado wanyama kama ndege wadogo wanalala katika sehemu ya kurukia mara nyingi ndege za kimataifa zimepata hititafu kwa ndege kuingia katika turbo power engine za ndege wakati wa kuruka hasa usiku,pia umbali wa kuruka kutoka Nairobi kuja Kilimanjaro kwa ndege kubwa distance ni ndogo sanaaaaa,tunatakiwa kuwekeza katika miundombinu ya kuwezesha wageni kufika nchini siyo mahoteli makubwa na hifadhi nzuri tu,Kenya hawana hifadhi nzuri au mahoteli mazuri kama sisi ndiyo sababu wanatangaza vivutio vyetu nao wapate maslahi kidogo na hayo ndiyo maisha,mpaka hapo nasi tutakaposhituka,tukijaribu tutaweza,Kenya wana ndege inaitwa Tanzanite tena Boeing 787 new,sasa we jiulize hiyo Tanzanite ipo kenya?au ni sisi tumewapelekea?,vikwazo tunajiwekea wenyewe kisha tunalalamika.tena wanaotangaza utalii wa Tz huko Kenya ni wa TZ kutokana na miundombinu yetu mibovu sisi tumekalia siasa tu utendaji 0%.tusilaumu sana serikali yetu....leo naweza kuitetea kidogo sana.....mwaka huu wamejitahidi kuutangaza utalii.....tuna wageni wengi sana nchini kwa sasa....ki ufupi kumefurika....na mkumbuke Kenya kuna al shabab....kufa kufaana.....
source: msiniulize....nyie jueni habari ndo hiyo.....
Waeleze waelewe maana ya ushirikiano wa Afrika mashariki ni nini? hauwezi kuitangaza Tanzania pekee ukapata wageni,kwanza kiwanja kikubwa cha ndege hatuna hizo terminal 2 za Mwl Nyerere Int. airport hazitoshi kurupushani ya ndege Kenyata int. airport zipo terminal kama 100 wageni wanaingia na kutoka kwa wingi,mashirika mengine makubwa ya ndege hayatui Dar kutokana na ufinyu wa uwanja,hiyo hata hao wanaoitangaza TZ wageni wakija wanatua Kenya ndiyo wapande Precision air kuja Tz,(1)haidhuru wakiitangaza serengeti au kilimanjaro wageni hawaishii kenya ni lazima wavuke mpaka kuja Tz tabu iko wapi?,Kenya wana shirika lao Kenya Airways sisi letu liko wapi?unategemea walete wageni mpaka Dar kwa faida ya nani? (2)hiyo Kilimanjaro Airport ndiyo usiseme hata sehemu ya kurukia ndege mashimo matupu bado wanyama kama ndege wadogo wanalala katika sehemu ya kurukia mara nyingi ndege za kimataifa zimepata hititafu kwa ndege kuingia katika turbo power engine za ndege wakati wa kuruka hasa usiku,pia umbali wa kuruka kutoka Nairobi kuja Kilimanjaro kwa ndege kubwa distance ni ndogo sanaaaaa,tunatakiwa kuwekeza katika miundombinu ya kuwezesha wageni kufika nchini siyo mahoteli makubwa na hifadhi nzuri tu,Kenya hawana hifadhi nzuri au mahoteli mazuri kama sisi ndiyo sababu wanatangaza vivutio vyetu nao wapate maslahi kidogo na hayo ndiyo maisha,mpaka hapo nasi tutakaposhituka,tukijaribu tutaweza,Kenya wana ndege inaitwa Tanzanite tena Boeing 787 new,sasa we jiulize hiyo Tanzanite ipo kenya?au ni sisi tumewapelekea?,vikwazo tunajiwekea wenyewe kisha tunalalamika.tena wanaotangaza utalii wa Tz huko Kenya ni wa TZ kutokana na miundombinu yetu mibovu sisi tumekalia siasa tu utendaji 0%.
INA MAANA UNAMSEMA MALIMA? PascoHizo ndizo priorities zetu!. Nilihudhuria Maonyesho fulani ya kukuza Utalii nchini US yaliyoandaliwa na AGOA, banda la Tanzania ilikuwa ni aibu ukilinganisha na Kenya!. Hebu fuatilia timu yetu ya Olympic jijini London ulinganishe na timu ya Kenya!.
Ila tusilaumu, sisi concetration yetu ni kale ka mchezo cha kwenye 6x6!.
No simsemi mtu, hiyo ndio priority ya viongozi wetu walio wengi na mimi nikiwa ni mmoja wa wenye priority hiyo ila mimi sio kiongozi!. Kwa sasa nina six kids, standard number ni 8!.INA MAANA UNAMSEMA MALIMA? Pasco
Vizuri, watatusaidia kutangaza mbuga yetu kimataifa.
Tbc, itv, chanel 10, chanel 5 na wengine mko wapi????
Pasco u can t chill how many kids dou you have?No simsemi mtu, hiyo ndio priority ya viongozi wetu walio wengi na mimi nikiwa ni mmoja wa wenye priority hiyo ila mimi sio kiongozi!. Kwa sasa nina six kids, standard number ni 8!.
Mie nilibahatika mwezi wa tano kuiona hiyo migration ya maasai mara.Kwakweli inavutia sana,wanyama wanakua wamenyoosha mstari mmoja mrefu.nilijaribu kupiga picha yangu ya mchina,haikua poa sana.kesho ntajaribu kupost hizo pic, pamoja na yale niliyoyaona Ngorongoro crater.nilichoshindwa kuelewa,huu utalii ni mzuri sana kuingilia route ya mwanza kuliko arusha.Maana ukiingilia pale Lamadi,ni karibu zaidi na unaanzia Serengeti,ukishaimalina unaingia Ngorongoro Crater,then unatokea Karatu,unakujaingia Manyara.Kwakweli ni bonge la tour.
Kule Crater wamasai wanaishi na wanyama na hawaliwi.
Ni wanyama au ni wale manyumbu? Sidhani kama ni wanyama wote wanaozungumziwa kuhama.
wakiwa masai mara ni upande wakenya na wakivuka kuja serengeti ni watanzania,sinaa hakika zaidi
hao pia ni wanyama bobuu.......kwanza wana kitu kimoja ambacho kinavutia sana......
wale wanazaa kutokana na hali ya chakula ilivyo......kama muda wa kuzaa umefika na bado mvua hazijanyesha.....huwa ana uwezo wa kuzuia kuzaa mpaka mvua zinyeshe ili mtoto wake apate nyasi.....ndio maana huwa anazalia kwenye plain area ili apate majani mapya machanga ya mtoto.....(naweza nikasahihishwa hapa kama nimekosea)..........
hii route pia inatumika.......japo wageni wanatokea Kenya kwa kupitia Isibania.......si wengi kama kutokea Arusha......
kwa mfano ningekuwa mimi ndio kiongozi wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano kati ya Zanzibar na Tanganyika.....ningeboresha uwanja wa Mwanza.......
wallah tusingeamini namna tungepiga bingo.......