Njoka Ereguu
JF-Expert Member
- Apr 7, 2012
- 821
- 336
Kama ingefanyika tathmini duniani, Tanzania inaongoza kwa viongozi wenye fikra za njozi kuliko matendo. Wewe umepewa mamlaka ya kuwezesha wananchi kuwa na maisha bora halafu unakuja taarifa ambazo ni njozi. Kauli hii inafaa kutolewa na wahubiri makanisani na watabiri siyo kiongozi mwenye mamlaka ambaye tayari tumeona utendaji kazi na uwongo wake. Si kosa kwa yeye kubadili kazi na kutangaza sasa kuwa amekuwa mtabiri.
Mwaka 2015 uwe wenye mafanikio makubwa sana. Taifa letu linaingia kwenye Uchumi wa Gesi Asilia. Dira yetu ya Maendeleo inatulazimisha kufanya kazi kwa bidii zaidi na kwa ubunifu mkubwa kwa kutumia sayansi na teknolojia ili ifikapo Mwaka 2025 Tanzania iwe nchi ya kipato cha kati (uchumi imara). Umeme mwingi, wa uhakika, wa bei nafuu na unaopatikana kiurahisi vijijini na mijini ndiyo injini kubwa ya upatikanaji wa ajira mpya kwa vijana wetu. S Muhongo