NAAMINI
JF-Expert Member
- Oct 14, 2013
- 672
- 235
Mwaka 2015 uwe wenye mafanikio makubwa sana. Taifa letu linaingia kwenye Uchumi wa Gesi Asilia. Dira yetu ya Maendeleo inatulazimisha kufanya kazi kwa bidii zaidi na kwa ubunifu mkubwa kwa kutumia sayansi na teknolojia ili ifikapo Mwaka 2025 Tanzania iwe nchi ya kipato cha kati (uchumi imara). Umeme mwingi, wa uhakika, wa bei nafuu na unaopatikana kiurahisi vijijini na mijini ndiyo injini kubwa ya upatikanaji wa ajira mpya kwa vijana wetu. S Muhongo