Maadhimisho ya miaka 35 ya CCM live Star tv

Maadhimisho ya miaka 35 ya CCM live Star tv

hao sio wanachama wapya. ni wao kwa wao waliketwa jana kwa maroli.
 
Nimeyaona malori yakisomba watu kutoka Misungwi, Sengerema na MAGU Vijijni pia, maana kuna ndugu zangu wamenipigia wakisema wapo njiani na malori ya ccm angalabu walione jiji na msosi wa bure.

SHAME ON CCM LEADERS
 
Ahhaahah hao wamenunuliwa hakika tena tusubiri ukweli utajulikana!!!kiboko yao wale chipukizi maana wale ndio waliopiga kura kuwadondosha ccm uchaguzi leo wamepata cha juu na wali na kusepa!!JK amekubali kuwasikiliza kilio chao cha kutopewa sehemu nzuri ya biashara....ndicho kisa kikuu cha ccm kuchukiwa mwanza mjini na ubabe wa kandoro!!!!
 
Heche alisema walikuwa wamejiandaa kuwarubuni viongozi wa chadema lakini nafurahi hawajafanikiwa. Kwanza hatuna hakika kama ni idadi hiyo lakini pia hakuna chadema hata mmoja aliyerudisha kadi. Safi sana watu wa mwanza hawanunuliki
 
Kwa nini CCM wanaendeleza hizi mbinu za kizamani? Kakabidhi kadi is purely cosmetic haitasaidia chochote. Uanachama uko moyoni.

CHADEMA fanyeni mkutano wa nguvu kusafisha jiji la mwanza baada ya hizi fuso za CCM kuondoka. Mara baada ya bunge kuisha, viongozi wote wakuu wa CHADEMA nendeni mwanza na muwaeleze wamachinga wasikubali kurubuniwa. Hela wanazopewa na ccm sasa hivi ni haki yao. Kama hawakuwatema ccm 2010 leo hii ccm isingekuwa inawasikiliza. Ni kupitia CHADEMA wamachinga wamewafundisha adabu hawa wazee wa posho.
 
udhalilishaji hapo uko wapi? hao ni watu wazima na akili zao, wewe endelea na mishemishe zako tu
 
hiyo bwana taarifa tumeipata ya kuwa ccm watanunua kadi feki na kuzichapa na kuwagawia wanachama wa ccm kisha waseme ni wanachadema wamerudisha kadi zao na kujiunga na ccm taariza za kiintelijensia tunazo kaka hilo lisiwape hofu peopleeeeeeeeeezzzzzz....
 
mfumuko wa bei na ugumu wa maisha ndio vimewavutia? au nipilau na nyama choma uwanjani zimewafanya wasahau shida zao.......hatudanganyiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiki?
 
Najaribu kufanya estimation ya gharama za zile tshirt na kofia na mapambo pale uwanjani, najaribu pia kupiga hesabu kama hawa watu wa kokodi wanapewa sh. 10,000 kila mmoja ni shillingi ngapi zimeteketea pale uwanjani wakati madaktari wanaendelea na mgomo na watu wanazidi kufa mahospitali. Na gharama hizo au sherehe hizo zinafanywa na chama chenye serikali, kwa kweli kuna ombwe kubwa la kiungozi Tanzania...
 
Wakinamama kibao na vizee! kama kuna kijana basi ni yule mwenye mapungufu ya akili.
 
wanachama 1847 wamejiunga na CCM wakitokea upinzani
nani kakwambia kwamba wametoka upinzani, kama wametoka upinzani mbona kadi walizokuwa nazo awali hawakuzionesha. hawa ni walewale CCM ila walikuwa hawana kadi kama wewe.
 
kazi hii ya kukijenga chama iwe ni ya kila siku.sio kusubiri matukio.mwanachama akiwa mchafu tumuondoe

Mwambie aache unafiki wa kijinga. Anasema chama kiwaondoe wachafu, mbona yeye kashindwa kuwaondoa serikalini Ngeleja na malima, Hosea na Utouh, ni wasafi hao? Mbona kashindwa kuwawajibisha Jairo na Luhanjo... Mbona anawachekeachekea Nyoni na Mponda, ni wasafi hao? &&@@@$ zake....
 
[h=3]JK AONGOZA MATEMBEZI MIAKA 35 YA CCM[/h]

Kikwete akimsalimia Katibu Mkuu wa CCM mstaafu, Philip Mangula kabla yamatembezi kuanza Ofisi ya CCM mkoa wa Mwanza. Kulia ni Katibu Mkuu Mstaafu Yussuf Makamba.
Rais Kikwete akimsalimia Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi Nape Nnauye kabla ya matembezi hayo.
Wananchi kutroka maeneo mbalimbali ya mkoa wa Mwanza wakiwa kwenye Ofisi ya CCM mkoa huo tayari kushiriki matembezi hayo.

Katibu Mkuu wa CCM Wilson Mukama akiwa na Makatibu wastaafu wa CCM, Yussuf Makamba na Philip Mangula kabla yamatembezi kuanza.
Vijana wa Sungusungu wakijifua kabla ya matembezi kuanza.
 
hiyo nitakwimu tu 1847 ili kujifurahisha na hao 30 ni walewale wanachama
 
Back
Top Bottom