Deadbody
JF-Expert Member
- May 30, 2015
- 4,276
- 6,585
- Thread starter
- #521
Dah jamaa alikuwa level zingine kabisa.Sylivester nimebahatika kusoma naye. Tumekaa wote bweni moja scandia. Sijawahi kuona mtu anayejua Maths kama yule. Siku moja katika mtihani wa Maths aliomba karatasi ya ziada baada ya saa moja na nusu huku Mtihani ukiwa ni wa masaa mawili na nusu. Mwalimu Majala wa Maths ndo alikuwa msimamizi akamletea karatasi kucheck akaona jamaa ameshamaliza mtihani wote na hata hajafuta chochote.Mwalimu akamuuliza ile karatasi ameomba ya nini ? Sylivester akamjibu ni ya kuprove majibu yake Mwl Majala akamnyima karatasi na kuchukua zile answer sheets zake na kutukana kwambs watu wengine bana unaomba karatasi wakati umemaliza mtihani wote akamwambia akusanye atoke nje. Majibu yalipokuja ana 99% Kumbuka mtihani ulikuwa umetungwa na Mwl Urio mtaalam wa hesabu na siyo mwl majala
Mwl majala alikuwa mvivu alikuwa anasema atafundisha topic mbili tu za Maths form five na form six. Ila kama unataka kumkomoa feli na anaongezea kuwa ila ukifaulu na kuwa wa kwanza kitaifa ni yeye atakayeenda bungeni kuchukua zawadi kama mwl wako
Sylivester tunaye udsm anachukua Masters of science in structural engineering