zomba
JF-Expert Member
- Nov 27, 2007
- 17,240
- 3,910
Kweli Chadema hawafanyi makosa! Nilimcheki kamanda akihitimisha baraza la M4C jana huko Ndanda pale alipowakumbusha kuwa CCM ni marehemu na wawe makini kung'amua hilo. Niliachwa hoi na art aliyotumia na kuwaacha hoi halaiki iliyokuwa inamsikiliza. Kwa maneno yake mwenyewe alisema:
"Kupe; si mnamjua kupe? Kupe akishamndandia ng'ombe yeye basi keshamaliza safari. Ng'ombe anapelekwa gulioni kupe yupo; ng'ombe anauzwa kupe yupo; ng'ombe anachinjwa kupe yupo tu; ng'ombe anachunwa ngozi kupe yupo tu; ngozi ikianza kuchomwa ndo kupe anazinduka, 'alaa, huyu jamaa kumbe kachinjwa!'
Waosha magamba mpooo?
Sasa ndio nini hicho?