Bartazar
JF-Expert Member
- Oct 4, 2011
- 1,043
- 565
Katika kile kinachoonekana kwa wananchi kuipokea nguvu ya mabadiliko kwa hamasa kubwa, wanakijiji 150 wa kijiji cha Mnavira Masasi wamejiunga na chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA). Wanabodi mnaweza kupata picha juu ya idadi hiyo, kijiji hicho hakina idadi kubwa sana ya watu, hivyo kupata idadi hiyo ya wanachama, ni kama robo tatu ya kijiji. Viongozi wa wilaya wanaendelea kupokea mialiko kwa ajili ya kupokea wanachama wapya na kufungua matawi!
Katika hali nyingine, mbunge wa Masasi Mariam Kasembe alijikuta kwenye wakati mgumu alipokuwa akitembelea jimbo, kwenye kijiji cha Mpanyani baada ya kushindwa kujibu Maswali kutoka kwa wanakijiji na wanakijiji wakaanza kuzomea! Aliishia kupanic na kupanda gari lake kurudi mjini! Baada ya hiyo sintofahamu habari za uhakika ni kwamba aliimwagiza mtendaji aorodhesha majina ya waliomzomea,na alipelekewa hayo majina na mtendaji huyo. Kisha alilipeleka suala hilo polisi na kuwapakazia vijana hao kuwa walimtishia kumuua!
Vijana hao waliwekwa ndani na sasa hivi wapo nje kwa dhamana!
Majuma kadhaa yaliyopita Makamanda wa CDM Masasi walitembelea kijiji hicho katika vuguvugu hili na kuwapa wananchi mbinu za kuwahoji viongozi wao kuhusu uwajibikaji wao kwao na utekelezaji wa ahadi walizozitoa wakati wa kampeni...!
Katika hali nyingine, mbunge wa Masasi Mariam Kasembe alijikuta kwenye wakati mgumu alipokuwa akitembelea jimbo, kwenye kijiji cha Mpanyani baada ya kushindwa kujibu Maswali kutoka kwa wanakijiji na wanakijiji wakaanza kuzomea! Aliishia kupanic na kupanda gari lake kurudi mjini! Baada ya hiyo sintofahamu habari za uhakika ni kwamba aliimwagiza mtendaji aorodhesha majina ya waliomzomea,na alipelekewa hayo majina na mtendaji huyo. Kisha alilipeleka suala hilo polisi na kuwapakazia vijana hao kuwa walimtishia kumuua!
Vijana hao waliwekwa ndani na sasa hivi wapo nje kwa dhamana!
Majuma kadhaa yaliyopita Makamanda wa CDM Masasi walitembelea kijiji hicho katika vuguvugu hili na kuwapa wananchi mbinu za kuwahoji viongozi wao kuhusu uwajibikaji wao kwao na utekelezaji wa ahadi walizozitoa wakati wa kampeni...!