Lutheran Primary School Moshi ilivyokuwa 1958 na sasa

Mohamed Said

JF-Expert Member
Nov 2, 2008
20,847
30,189
LUTHERAN PRIMARY SCHOOL MOSHI KAMA ILIVYOKUWA 1950s NA SASA

Nilianza darasa la kwanza mwaka wa 1958 kwenye jengo hilo hapo chini lililokuwa ni Kanisa la Kilutheri.

Baada ya miaka mingi nilifika Moshi kuangalia pale nilipoanza shule.

Ilikuwa siku ya Jumamosi tarehe 20 December, 1986 na nikapiga picha hiyo ya kwanza nimesimama kwenye mlango wa kuingilia kanisani ambako ndiko nilipoanza kusoma.

Ile piano ambayo Mwalimu Paul alikuwa akipiga na sisi wanafunzi tukiimba ''hyms,'' ilikuwa pale pale ilipokuwa mwaka wa 1958.

Piano ile ilirejesha kwangu kumbukumbu nyingi pamoja na nyimbo nilizojifunza pale na zote nikizikumbuka kama vile niliziimba jana ---''Damu ya Kondoo,''Ni Nani Aliyetuumba ni Mungu Mwenyewe,'' ''Ewe Mwezi ni Rafiki Yangu,'' ''Tunamsifu Baba Marehemu Kingi George.''

Kuzunguka kanisa kulikuwa na bustani nzuri ya maua ya rangi tofauti na kulikuwa na ukoka uliopandwa kiasi huoni ardhi.

Mwalimu Paul alikuwa mtu mzima na ndiye aliyeniandikisha shule nikiwa na miaka sita.

Alikuwa siku zote akivaa pama hata darasani.

Alikuwa akitufundisha kuwa watu wakifa wanakwenda mbinguni.

Miaka miwili tu mama yangu alikuwa amefariki na ndiyo sababu ya mimi kuchukuliwa na mama yangu mdogo na kujanae Moshi alipokuwa akifanya kazi katika Nursing Home ya Mgiriki Dr. Georgedis nianze shule.

Hospitali hii ilikuwa makhsusi kwa Wazungu tu.

Kwa kuwa Mwalimu Paul alikuwa akitufunza kuwa watu wakifa wanakwenda mbinguni nilikuwa na kawaida ya kukaa kwenye ukoka kwenye bustani peke yangu na wakati mwingine nikilala chali kuangalia juu mawinguni nikitegemea kumuona mama yangu.

Namkumbuka mwanafunzi mwenzangu umri sawa na mimi akiitwa Njuguna wakati mwingine akija kukaa na mimi pale bustanini.

Njuguna alikuwa mzuri na nikipenda sana awe karibu yangu.

Miaka ilisogea na pamoja tukawa wakubwa kiasi miaka miaka 12 hivi.

Siku moja kwenye fete alipewa microphone akaambiwa aimbe nyimbo yoyote aitakayo.

Junguna akaimba, "Oh Carol," ya Neil Sedaka kwa ustadi mkubwa sana.

Kila niisikiapo nyimbo hii humkumbuka Njuguna.

Njuguna ametangulia mbele ya haki miaka mingi iliyopita.

Namkumbuka Hidaya yeye tukifuatana pamoja kwenda shule.

Siku moja nikauliza kama Hidaya yuko mjini.

Nikafahamishwa kuwa amefariki miezi michache iliyopita.

Alikuwa nurse Hospitali ya Mawenzi.

Majonzi yalinijia ingawa tulipoachana sote tulikuwa watoto wadogo labda wa miaka 10.

Miaka imekwenda wapi?

Picha hiyo ya pili nimeipiga tarehe kama hii ya leo mwaka jana nikapiga sehemu ile niliyosimama mwaka wa 1986 miaka 36 iliyopita.

Kanisa ambalo ndani yake ndiko lilipokuwa darasa langu la kwanza pamebadilika sana kama inavyoonekana kwenye picha.

Screenshot_20220324-233058_Facebook.jpg
 
Kumbe Mzee tulikuwa wote bana!!....... unamkumbuka Wambura chacha??meno kuoza??!!..safi san umenikumbusha mbali sana itabidi nikapatembeleee!!.....Shule ya Msingi KIbumaye niliendaga huko baada ya hapo!

lkn weye unaonekana ulikuwa na marafiki wachache sana kwa nini??......halafu wamekufa!! mie sasa nilikuwa na marafiki darasa zima walikuwa wana nizimia tena hao hao wakanichagua kuwa Monitor wao Kwa nguvu!!

Miaka yote mie nikawa Kiongozi!......kuuumbe tabia huanzia utotoni bana weee!! mpaka leo nina mavyeo karibu yooote !!
 
Mungu amekufanyia makubwa sana mzee wangu na dunia umeizunguka sana,sana sisi vijana wako tufanye nini tufanikiwe hivyo Mr.Mohammed said?
Classic...
Naweza kusema ni mipango ya Mwenyezi Mungu, bahati na nyakati zetu fursa zilikuwa nyingi.
Jambo moja linazua jingine hivyo, hivyo mambo yanakwenda.
 
Alaah! Kumbe mzee Mohamed ulipata elimu kwenye shule za "kikafiri"
Ndiyo elimu utumiayo sasa kwenye makala zako za "historia ya tanganyika"
 
LUTHERAN PRIMARY SCHOOL MOSHI KAMA ILIVYOKUWA 1950s NA SASA

Nilianza darasa la kwanza mwaka wa 1958 kwenye jengo hilo hapo chini lililokuwa ni Kanisa la Kilutheri.

Baada ya miaka mingi nilifika Moshi kuangalia pale nilipoanza shule.

Ilikuwa siku ya Jumamosi tarehe 20 December, 1986 na nikapiga picha hiyo ya kwanza nimesimama kwenye mlango wa kuingilia kanisani ambako ndiko nilipoanza kusoma.

Ile piano ambayo Mwalimu Paul alikuwa akipiga na sisi wanafunzi tukiimba ''hyms,'' ilikuwa pale pale ilipokuwa mwaka wa 1958.

Piano ile ilirejesha kwangu kumbukumbu nyingi pamoja na nyimbo nilizojifunza pale na zote nikizikumbuka kama vile niliziimba jana ---''Damu ya Kondoo,''Ni Nani Aliyetuumba ni Mungu Mwenyewe,'' ''Ewe Mwezi ni Rafiki Yangu,'' ''Tunamsifu Baba Marehemu Kingi George.''

Kuzunguka kanisa kulikuwa na bustani nzuri ya maua ya rangi tofauti na kulikuwa na ukoka uliopandwa kiasi huoni ardhi.

Mwalimu Paul alikuwa mtu mzima na ndiye aliyeniandikisha shule nikiwa na miaka sita.

Alikuwa siku zote akivaa pama hata darasani.

Alikuwa akitufundisha kuwa watu wakifa wanakwenda mbinguni.

Miaka miwili tu mama yangu alikuwa amefariki na ndiyo sababu ya mimi kuchukuliwa na mama yangu mdogo na kujanae Moshi alipokuwa akifanya kazi katika Nursing Home ya Mgiriki Dr. Georgedis nianze shule.

Hospitali hii ilikuwa makhsusi kwa Wazungu tu.

Kwa kuwa Mwalimu Paul alikuwa akitufunza kuwa watu wakifa wanakwenda mbinguni nilikuwa na kawaida ya kukaa kwenye ukoka kwenye bustani peke yangu na wakati mwingine nikilala chali kuangalia juu mawinguni nikitegemea kumuona mama yangu.

Namkumbuka mwanafunzi mwenzangu umri sawa na mimi akiitwa Njuguna wakati mwingine akija kukaa na mimi pale bustanini.

Njuguna alikuwa mzuri na nikipenda sana awe karibu yangu.

Miaka ilisogea na pamoja tukawa wakubwa kiasi miaka miaka 12 hivi.

Siku moja kwenye fete alipewa microphone akaambiwa aimbe nyimbo yoyote aitakayo.

Junguna akaimba, "Oh Carol," ya Neil Sedaka kwa ustadi mkubwa sana.

Kila niisikiapo nyimbo hii humkumbuka Njuguna.

Njuguna ametangulia mbele ya haki miaka mingi iliyopita.

Namkumbuka Hidaya yeye tukifuatana pamoja kwenda shule.

Siku moja nikauliza kama Hidaya yuko mjini.

Nikafahamishwa kuwa amefariki miezi michache iliyopita.

Alikuwa nurse Hospitali ya Mawenzi.

Majonzi yalinijia ingawa tulipoachana sote tulikuwa watoto wadogo labda wa miaka 10.

Miaka imekwenda wapi?

Picha hiyo ya pili nimeipiga tarehe kama hii ya leo mwaka jana nikapiga sehemu ile niliyosimama mwaka wa 1986 miaka 36 iliyopita.

Kanisa ambalo ndani yake ndiko lilipokuwa darasa langu la kwanza pamebadilika sana kama inavyoonekana kwenye picha.

View attachment 2163433
Karibu tena kundini mkuu
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom