nkongu ndasu
JF-Expert Member
- Jan 19, 2013
- 22,532
- 6,628
naunga mkono wabunge aina ya lusinde wanaliaibisha bunge, wanaliaibisha taifa! Poleni wana mtera.CCM wanadhani jimbo la Mtera limekosa mwakilishi makini na hivyo juhudi zinafanyika ili wamng'oe, na mimi sina hakika kama wakati kama huu mwakani tutakuwa naye maana CCM wakimkosakosa nina hakika UKAWA hawatamwacha, lazima atamumwaga. Hatuwezi kuwa na wabunge ambao kkazi yao kubwa ni vijembe na halafu akafikiria atachaguliwa tena kwa vijembe vyake. Tundu Lissu alipodai apewe dakika zaidi ya dk tatu ambazo spika alizokuwa ameamua zitumike alikuwa amefuata kanuni na taratibu za bunge na ndiyo maana spika alikubaliana naye, sasa mbunge ambaye siku zote yuko bungeni lakini hajui hata hizi taratibu rahisi anakaaje bungeni. Wabunge wote wa aina yake lazima wawapishe wenye uwezo wakatufanyie kazi.
haa haaa mbavu zangu mie!Wagogo Mungu ndiye wakuwasaidia tu.
haa haa duh.Mkuu yule ndio msomi wa juu pale mtera.... My foot hii nchi inaongozwa na vilaza wa kila aina
Wagogo Mungu ndiye wakuwasaidia tu.
Mimi nitaamini kwamba sasa Watanzania wameelimika endapo watawapiga chini wabunge wote mizigo na vihiyo. Hatuwezi kuwa na wabunge aina ya joti wanaokwenda kufanya komedi na kuchekesha watu bungeni. Tunataka wabunge serious ndani ya bunge na siyo comedians.
haa haa lusinde awe waziri! Toba!! Hapo wizarani muda wote vitapigwa vichekesho na komedi za nguvu badala ya kuwatumikia watanzania!Kilichopwaya ni kiti cha Lusinde! Ndiyo maana na kujikomba kwake kote, hata JK ameona kwamba hamfai katika Baraza lake dhaifu la mawaziri.
haa haaa...yaani jimbo zima wamekosa mtu wa kuwawakilisha bungeni wakampata lusinde! Kama taifa kwenye elimu tumekwama kama wabunge wenyewe ndo hawa"Wana mtera mkirudisha hiki kiazi mwaka huu itabidi jimbo Zima mkapimwe akili tena uzuri hospitali ya magonjwa ya akili iko hapo hapo mkoani kwenu dodoma.
Lusinde amesema makinda anapwaya kwa kuwa sasa hivi halindi maslahi ya ccm, anafuata pressure ya UKAWA, na kwa kufanya hivo CCM inaumizwa kwa kuonekana hamna wanalolifanya.
CCM wanadhani jimbo la Mtera limekosa mwakilishi makini na hivyo juhudi zinafanyika ili wamng'oe, na mimi sina hakika kama wakati kama huu mwakani tutakuwa naye maana CCM wakimkosakosa nina hakika UKAWA hawatamwacha, lazima atamumwaga. Hatuwezi kuwa na wabunge ambao kkazi yao kubwa ni vijembe na halafu akafikiria atachaguliwa tena kwa vijembe vyake. Tundu Lissu alipodai apewe dakika zaidi ya dk tatu ambazo spika alizokuwa ameamua zitumike alikuwa amefuata kanuni na taratibu za bunge na ndiyo maana spika alikubaliana naye, sasa mbunge ambaye siku zote yuko bungeni lakini hajui hata hizi taratibu rahisi anakaaje bungeni. Wabunge wote wa aina yake lazima wawapishe wenye uwezo wakatufanyie kazi.
kwa hiyo wanakoboana na kusagana!!! dah kazi ipo!!!!Na ndio Mume wa Lizaboni
Watu wa mtera ndivyo walivyo,refer Le Mutuz.
Wabunge wote wagogo ni bure kabisa.
Pro-Chadema wengi uwa wanafiki sana hawajui wanachotaka wala wanachokipigania.
Juzi walikuwa wanaungana na Lusinde kuhusu ushahidi wake kuwa Zitto Kabwe aliongwa milioni 10 na PAP.
Tukaambiwa kuwa anafuatiliwa na TAKURU, leo tena pro-Chadema mnapingana na Lusinde.