Lizaboni
JF-Expert Member
- Feb 21, 2013
- 33,901
- 20,416
Mheshimiwa Lukuvi kwa mara nyingine amesema maneno yanayochoma sana bungeni muda huu. Amesema kuwa wabunge wa UKAWA wanasema kuwa wana mkanda wa video unaomuonesha Lukuvi akileta uchochezi wa kidini kanisani.
Amesema kuwa kama wao wana video moja, yeye anazo zaidi ya 20 (amezionesha) ambazo zinawaonesha viongozi mbalimbali wa upinzani wakileta uchochezi kwenye nyumba za ibada. Anasema kuwa viongozi wa CUF ndio wameasisi wa siasa za udini nchini kutokana na kauli zao na matendo yao.
Amewaonya wabunge wa upinzani kwa kitendo chao cha kuendelea kudodosa mambo wasiyoyajua kwa vile yeye anao ushahidi wa kutosha juu ya uchochezi wa viongozi wa UKAWA. Anasema kuwa baadhi ya viongozi wa UKAWA wamemuomba asiseme sana ili wasiumbuke hivyo na yeye ameheshimu maombi hayo ili asiharibu hali ya hewa.
Amesema kuwa ndani ya UKAWA kuna usaliti wa hali ya juu kiasi ambacho ni vigumu tena kujiaminisha kuwa wanasimamia matakwa ya wananchi.
Amesema kuwa bunge la bajeti halipo kwa malengo ya kuvurugana kutokana na itikadi za kisisa. Amewaomba wabunge wa UKAWA kurudi kwenye bunge la Katiba huko ndiko mambo yatawekwa hadharani.
Hakika wakati Lukuvi anaongea, nimewaona wabunge wa UKAWA wakiinamisha macho chini kwa aibu. Viva Lukuvi
Amesema kuwa kama wao wana video moja, yeye anazo zaidi ya 20 (amezionesha) ambazo zinawaonesha viongozi mbalimbali wa upinzani wakileta uchochezi kwenye nyumba za ibada. Anasema kuwa viongozi wa CUF ndio wameasisi wa siasa za udini nchini kutokana na kauli zao na matendo yao.
Amewaonya wabunge wa upinzani kwa kitendo chao cha kuendelea kudodosa mambo wasiyoyajua kwa vile yeye anao ushahidi wa kutosha juu ya uchochezi wa viongozi wa UKAWA. Anasema kuwa baadhi ya viongozi wa UKAWA wamemuomba asiseme sana ili wasiumbuke hivyo na yeye ameheshimu maombi hayo ili asiharibu hali ya hewa.
Amesema kuwa ndani ya UKAWA kuna usaliti wa hali ya juu kiasi ambacho ni vigumu tena kujiaminisha kuwa wanasimamia matakwa ya wananchi.
Amesema kuwa bunge la bajeti halipo kwa malengo ya kuvurugana kutokana na itikadi za kisisa. Amewaomba wabunge wa UKAWA kurudi kwenye bunge la Katiba huko ndiko mambo yatawekwa hadharani.
Hakika wakati Lukuvi anaongea, nimewaona wabunge wa UKAWA wakiinamisha macho chini kwa aibu. Viva Lukuvi