Lugha ya Kiafrikana (Africaans)

Nyanidume

JF-Expert Member
Oct 24, 2012
2,364
1,023
Afrika ya Kusini ni nchi yenye historia ya ajabu ambapo ubaguzi wa rangi ndiyo ulichukua nafasi kubwa katika maisha ya kila siku. Historia hiyo inakwenda mbali hadi mwaka 1852 wakati ambao walowezi wa Kiholanzi walipowasili nchini humo ikiwa ni sehemu ya ukoloni wa wazungu katika bara la Afrika. Wakoloni hao wamekuwepo Afrika kusini kwa muda mrefu huku wakiikuza lugha yao ya Kiafrikana na baadaye wakaja kujurikana kama makaburu (boers) yaani wakulima. Wakuu, baada ya maelezo hayo mafupi ninayoyajuwa kuhusu hao makaburu pia ningependa kujuwa zaidi kwani ndiyo msingi wa kuanzisha uzi huu, je hii lugha ya Kiafrikana ilikuwepo huko Uholanzi kabla ya kulowea huko kusini mwa Afrika? na je inaendelea kutumika huko kwenye asili yao (Uholanzi)? Na vipi inaitwa Kiafrikana (Africaans) jina ambalo linafanana na jina la bara letu (Africa)?
Kwa hayo machache natumai nitapata jibu la maswali yangu. Ahsanteni.
 
!
!
hii nadhani itakuwa ni pijini ambayo imezaliwa huku afrika. Kwa hiyo hata kama ina asili ya huko uholanzi basi itakuwa imetofautiana na ile ya asili tu
 
!
!
hii nadhani itakuwa ni pijini ambayo imezaliwa huku afrika. Kwa hiyo hata kama ina asili ya huko uholanzi basi itakuwa imetofautiana na ile ya asili tu

Ahsante mkuu, kwa jibu lako naanza kupata pa kuanzia katika kuifahamu lugha hii!
 
Lugha hiyo inaunganisha lugha ya asili za asili za Afrika kusini hasa ya kabila la kina bushmen na lugha ya kiholanzi. Makaburu walifanya vile ili iwe rahisi kuwasiliana na watu weusi na kuwatawala kwa urahisi zaidi. Kimsingi hii lugha ya kiafrikana haipo Uholanzi na inasemekana kuwa ukiongea kiafrikana ukiwa Uholanzi hakuna mholanzi atakayekuelewa kabisa kwa sababu lugha ya kiholanzi yenyewe ilishatoholewa sana hadi lugha mpya ya kiafrikana ikazaliwa na mholanzi mwenyewe wa Afrika kusini akiamua kuongea lugha yake tupu bila kuongea kiafrikana,anayejua kiafrikana hawezi kung'amua chochote kile kilichoongelewa. Hivyo makaburu walipokuwa wanataka kuwateta watu weusi walikuwa wanaongea kiholanzi origino na wanafanya mambo yao. Lugha ya kiafrikana inasemekana ni ngumu sana kujifunza tofauti na lugha zingine za Afrika ya kusini.

Source: Kwa msaada wa vijana wa kitanzania wanaokimbilia Afrika kusini kutafuta maisha
 
Lugha hiyo inaunganisha lugha ya asili za asili za Afrika kusini hasa ya kabila la kina bushmen na lugha ya kiholanzi. Makaburu walifanya vile ili iwe rahisi kuwasiliana na watu weusi na kuwatawala kwa urahisi zaidi. Kimsingi hii lugha ya kiafrikana haipo Uholanzi na inasemekana kuwa ukiongea kiafrikana ukiwa Uholanzi hakuna mholanzi atakayekuelewa kabisa kwa sababu lugha ya kiholanzi yenyewe ilishatoholewa sana hadi lugha mpya ya kiafrikana ikazaliwa na mholanzi mwenyewe wa Afrika kusini akiamua kuongea lugha yake tupu bila kuongea kiafrikana,anayejua kiafrikana hawezi kung'amua chochote kile kilichoongelewa. Hivyo makaburu walipokuwa wanataka kuwateta watu weusi walikuwa wanaongea kiholanzi origino na wanafanya mambo yao. Lugha ya kiafrikana inasemekana ni ngumu sana kujifunza tofauti na lugha zingine za Afrika ya kusini.

Source: Kwa msaada wa vijana wa kitanzania wanaokimbilia Afrika kusini kutafuta maisha
Mungu akubariki mkuu, hakika ufafanuzi wako umenitoa tongotongo
 
Back
Top Bottom