Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,461
- 39,928
Watawala wetu walioshindwa wamejaribu kutengeneza siasa ambayo si siasa tena; wanajaribu kuichakachua na kufanya siasa isiwe vile ilivyo. Siasa ni pamoja na kejeli, utani, kebehi, uchokozi na hata kurushiana madongo na vijembe.
Leo hii wamejaribu kubadilisha siasa na kutaka kuleta kitu kinachoitwa "lugha ya kiistaarabu" katika kampeni za kisiasa. Kimsingi wanachokitaka ni "lugha zisizowaudhi watawala". Jaribio hili ni la hatari katika demokrasia na uhuru wa maoni. Demokrasia hujengwa kwa kutumia ushawishi na ushawishi wa maneno hutumia nyenzo mbalimbali za lugha katika kufikisha ujumbe.
Kumbe vijembe, utani, kebehi, kejeli na hata utani ni nyenzo mbalimbali za lugha ambazo hutumiwa kufikicha ujumbe wa kisiasa. Watawala wetu walioshindwa wameanza kukosa uvumilivu. Wanataka wote tuanza kuzungumza kwa lugha moja ya "kistaarabu" lugha ambayo haipo kwenye siasa mahali popote duniani.
Ili kufikicha ujumbe unaokusudiwa mwanasiasa ni lazima awe huru kujitofautisha na mwanasiasa mwingine na ni lazima awe na wigo mpana zaidi wa kufikisha ujumbe wake kwa hadhara.
Sasa, nyenzo hizo mbalimbali mara kwa mara hubeba ujumbe uliofichika ambao wakati mwingine haunogi kusemwa vinginevyo. Kama vile katuni zinavyoweza kutumika kuelezea ukweli fulani kuliko picha tu basi lugha nayo yaweza kutumiwa kwa namna mbalimbali kuelezea ukweli fulani vile vile.
Ni kutokana na ukweli huo nimeamua kuruhusu matumizi ya kejeli, utani, dhihaka, vijembe na madongo ya kisiasa. Hii ina maana kuwa vyombo vya habari visijikute kuwa ni polisi wa maoni kwa kuangalia ni maoni gani yasiruhusiwe hasa kama yanaonekana kuwa ni ya vijembe, kejeli au utani au ambayo yanaweza kuwafanya watawala walioshindwa kujisikia kuwa wanaonewa.
Vinginevyo kama wanaona demokrasia ni ngumu sana kuweza kuvumilia maoni yenye kuudhi basi wajaribu udikteta.
Leo hii wamejaribu kubadilisha siasa na kutaka kuleta kitu kinachoitwa "lugha ya kiistaarabu" katika kampeni za kisiasa. Kimsingi wanachokitaka ni "lugha zisizowaudhi watawala". Jaribio hili ni la hatari katika demokrasia na uhuru wa maoni. Demokrasia hujengwa kwa kutumia ushawishi na ushawishi wa maneno hutumia nyenzo mbalimbali za lugha katika kufikisha ujumbe.
Kumbe vijembe, utani, kebehi, kejeli na hata utani ni nyenzo mbalimbali za lugha ambazo hutumiwa kufikicha ujumbe wa kisiasa. Watawala wetu walioshindwa wameanza kukosa uvumilivu. Wanataka wote tuanza kuzungumza kwa lugha moja ya "kistaarabu" lugha ambayo haipo kwenye siasa mahali popote duniani.
Ili kufikicha ujumbe unaokusudiwa mwanasiasa ni lazima awe huru kujitofautisha na mwanasiasa mwingine na ni lazima awe na wigo mpana zaidi wa kufikisha ujumbe wake kwa hadhara.
Sasa, nyenzo hizo mbalimbali mara kwa mara hubeba ujumbe uliofichika ambao wakati mwingine haunogi kusemwa vinginevyo. Kama vile katuni zinavyoweza kutumika kuelezea ukweli fulani kuliko picha tu basi lugha nayo yaweza kutumiwa kwa namna mbalimbali kuelezea ukweli fulani vile vile.
Ni kutokana na ukweli huo nimeamua kuruhusu matumizi ya kejeli, utani, dhihaka, vijembe na madongo ya kisiasa. Hii ina maana kuwa vyombo vya habari visijikute kuwa ni polisi wa maoni kwa kuangalia ni maoni gani yasiruhusiwe hasa kama yanaonekana kuwa ni ya vijembe, kejeli au utani au ambayo yanaweza kuwafanya watawala walioshindwa kujisikia kuwa wanaonewa.
Vinginevyo kama wanaona demokrasia ni ngumu sana kuweza kuvumilia maoni yenye kuudhi basi wajaribu udikteta.