Ludovick Utouh: Hakuna usawa wa Mihimili, Serikali Kuu inafunika Mihimili mingine

BARD AI

JF-Expert Member
Jul 24, 2018
3,377
8,121
Akizungumza katika Mjadala wa Uwajibikaji na Bajeti, Utouh amesema licha Katiba kueleza kuwa Mihimili 3 (Serikali, Bunge na Mahakama) iko sawa, kiuhailisia haiko hivyo na hali hiyo imedhoofisha Uwajibikaji na Utendaji wa Mihimili mingine.

Amesema ili kuwepo kwa Uwajibikaji na Utawala Bora lazima kuwena Vigezo ambavyo ni Mtoa Dhamana anayeiweka Serikali Madarakari (Mwananchi), Mbeba Dhamana (Serikali), Kilichowekewa Dhamana (Madaraka ya Watu na Taasisi), Mtoa Dhamana kumwajibisha Mbeba Dhamana na Matokeo ya Kutowajibika.

Akifafanua zaidi, Utouh amesema Wananchi wanapaswa kujiuliza kwa hali ilivyo Nchini kama wanaweza kuiwajibisha Serikali au Watu waliowapa Madaraka au wanasubiri hadi ufanyike Uchaguzi ndio waoneshe kuwawajibisha waliowapa Dhamana.
 
Back
Top Bottom