Lizaboni
JF-Expert Member
- Feb 21, 2013
- 33,894
- 20,372
Wakati ninakuwa wazazi wangu walinifundisha penda kusikia zaidi na kusema kidogo, ndani ya machache kuna hekima zaidi kuliko maneno mengi, Mtela tumekusikia ila kuwa makini kuna siku utakuwa peke yako unatetea ushahidi wako. Mimi ni mwanachama hai wa Chadema na hakuna mtu anayenijua hapo makao makuu, na ni mpenzi wa chadema zaidi ya miaka kumi sasa, na haya unayoyaona wewe sasa ni mapito ya kawaida sana katika chama chochote cha siasa. Karume alipo uwawa usidhani watu walikaa kimywa walisema, Kolimba ndugu yangu alipo uwawa siyo kuwa tulikaa kimywa tuliumia, lakini CCM bado ipo na wale ndugu zangu anakotoka Kolimba hawaambiliki juu ya CCM hata baada ya Kolimba kufa, jua CHADEMA ipo na haitakufa, fanya lolote kaka na hata ukaloge CHADEMA haitakufa. Ukidhani unaongea point leo tutaonana 2015 Vwawa, mimi nitakusikia.
Umetumwa na chama chako kuomba msamaha kwa MWAMPAMBA nini? mkuu ukumbuke Mwampamba anawafungua watanzania waelewe kinachoendelea ndani ya vyama vyetu vya siasa, hana lengo na sidhani ana uwezo kukiua CHADEMA lakini ukweli ni kwamba kupitia post zake watanzania watakuwa wamejifunza na hata wanapokurupuka kuvishabikia vyama hivi wajue wakabisa ni majanga na havina nia njema kwa msatakabali wa taifa letu ambalo amani yake mwasisi wake ni CHAMA CHA MAPINDUZI