Ludewa, Njombe: RC asema wasiolima mazao ya biashara kuwekwa rumande

Influenza

JF-Expert Member
Jul 1, 2018
1,445
3,403
Mkuu wa wilaya ya Ludewa mkoani Njombe Andrea Tsere ametangaza kumuweka lumande “Lock up” mwananchi yeyote atakayeshidwa kuwa na zao la biashara kutokana na uhamasishaji mkubwa unaoendelea wilayani humo ili kukuza uchumi wa wilaya na wananchi wa wilaya hiyo.

Mkuu wa wilaya hiyo amesema uamuzi huo katika kikao cha hamasa cha wadau/wanaLudewa wanaoishi nje ya wilaya kilichofanyika mjini Njombe, na kutokana na sheria ndogo walizojiwekea ili kuhakikisha kila mtu anakuwa na zao la biashara kwa kuwa wilaya hiyo imekuwa ikikubali mazao mbali mbali ya kibiashara ikiwemo zao la korosho,chai na kahawa hivyo sheria kali zitachukuliwa kwa mwananchi ambaye hataweza kushiriki katika mazao hayo.

“Akiwa Lock up tutakuwa tunamuelimisha umuhimu wa kupanda korosho,akielewa akiahidi kwamba atapanda tutamuachia aende kupanda korosho,lakini kwasababu tumetunga sheria kama ataendelea kuwa mkaidi tutampeleka mahakama ya mwanzo kwasababu kuto kupanda zao la biashara ni ukiukwaji kwa mujibu wa sheria ndogo ya halmashauri na kama watakuwa wengi tutawachukuwa kwa viwango”anasema Andrea Tsere

Amesema mkuu wa wilaya amepewa mamlaka na Rais kwa mujibu wa sheria ya kumuweka mtu yeyote masaa 24 hakutakuwa na swali lolote ni lazima mkaidi apelekwe Lumande kwakuwa ajenda iliyopo kwa sasa ni kujenga uchumi huku mazao hayo yakiwa ni mali yao wananchi
 
Common law ukiangalia mabadiliko yake mengi yalitokana na questioning from citizens. Leo imekua ni source of law kwa mataifa mengi yaliyopo commonwealth. Kila mwaka tunazalisha wasomi LLB/M ila sijui huwa wanajificha wapi. Zile mbwembwe za campus ni tofauti na huku mtaani.
 
NI WAZO ZURI SANA KAJA NALO HUYO Mh. DC ILA PIA TUNASHAURI PAWEPO NA MKAZO ZAID NA ZAID KTK KUDHIBITI MBEGU NA MBOLEA ZISIZO NA UBORA.

Tupo pamoja Mh. DC
 
Huwa inaudhi pale MTU umezaliwa na kukulia zako ludewa alafu analetwa MTU toka mbulu huko anakuletea ujinga wake ukiukataa anakutia kizuizini!!! Nikama yule wa hai anayemzuia lema kwenda kijijini kwao eti aombe kibali maana yeye ni wa arusha!!?!?? Yaani umetoka makondeko huko unamzuia MTU asiende kwao na asikutane na watu wakwao?? Asee....
 
Huwa inaudhi pale MTU umezaliwa na kukulia zako ludewa alafu analetwa MTU toka mbulu huko anakuletea ujinga wake ukiukataa anakutia kizuizini!!! Nikama yule wa hai anayemzuia lema kwenda kijijini kwao eti aombe kibali maana yeye ni wa arusha!!?!?? Yaani umetoka makondeko huko unamzuia MTU asiende kwao na asikutane na watu wakwao?? Asee....
Hana historia ya wanyasa wabena wapangwa wakinga ataamka siku moja ajikute yupo Lake Nyasa anavua samaki
 
RC kama bwana shauri hawa akina Nyerere kazi yao imeisha thamani, tumepiga return.
 
Back
Top Bottom