M45
JF-Expert Member
- Aug 20, 2015
- 1,461
- 2,321
Kura za Rais nazo zinabandikwa kituoni. Wanachokataa NEC ambacho mimi sikubaliani nacho ni kwamba huruhusiwi kujumlisha kura za Rais kutoka vituo mbali mbali na kutangaza.
Ila kubandika, mbona hata 2010 walibandika ?
Kwa hiyo hapo sioni chochote alichoagiza, amekumbushia tu utaratibu wa siku zote ambao hata 2010 ulikuwepo
Vizuri
Kama kura zote mpaka za Rais zitabandikwa itakua vyema sababu tutakua tumeiona picha mapema kabla ya kupelekwa Makao Makuu ya Nec ili kumtangaza mshindi.
Kinachotakiwa Vyama vya Ukawa Viwaandae Mawakala ambao ni Halisi sio Pandikizi wa Vyama vingine.
Ambao hawatakubali chochote kifanyike nje ya Utaratibu.
Tanzania Mpya inakuja.