Lowassa: Tuko tayari kuingia vitani na Malawi...

Lowassa: Tuko tayari kuingia vitani na Malawi...

Suala hili la uvamizi liko mahakamani, si vema sana kulizungumzia tutaingilia uhuru wa mahakama. Wazambia wanadai mambo makubwa sana ambapo taifa Kwa Sasa haliwezi kuwatimizia..

ha! Ha! Ha! Ha! Ha! Da! Maisha ya kibongo bana,raha mostarehe.huenda chadema wanahusika.
 
Mimi nashangaa chain of command yetu iko wapi. Lowassa yeye ni nani kuzungumza kwa niaba ya JWTZ? Kamanda in Chief yuko wapi? Yaani Tanzania yetu imeshaparaganyika kiasi kwamba yeyote tu anaweza kuzungumza kwa niaba yake? Suala la vita au kuwa tayari kwa jeshi letu ni kamanda in chief peke yake anayeweza kulizungumzia. When was the last time you saw Lowassa inspecting a guard of honour?
Mwenye kustahili kutoa kauli ya vita au amani yupo kwenye ngoma akitoka huko anaandaa safari kutembelea malawi.Hata kwenye histoa ushajifunzanza kwamba wakware walipigana vita?Wao hupiga ngoma
 
Tunaomba juhudi za kutatua mgogoro huu kwa njia ya kidiplmasia utumike.

Zikishindikana zipigwe tu.

Kitendo cha Malawi kuanza kufanya utafiti wa gesi na mafuta na kutangaza kuwa hilo ziwa ni lao, huku wakijuwa kuwa hilo ziwa lina migogoro tangu uhuru.

Badala ya kukaa chini na watz kwanza ili kuumaliza kwanza huo mgololo. Wao wanaamuwa kuingia kwenye ziwa hilo kwa nguvu na kuwafukuza watz wanao litegemea hilo ziwa. Ni sawa na kusema liwalo na liwe. Ni sawa na kusema kuwa malawi wameshatangaza vita na wako tayari kwa lolote na wameshapanga majeshi yao kivita wanasubili majibu kutoka Tz.

Kinachochelewesha hapa ni busara tu ya watz ambao wanataka kwanza kutumia busara za kidiplomasia na hii inatokana na watz wenyewe kutokuwa na hulka ya kupigana na majirani, mbona ingekuwa nchi zingine zingekuwa zimeshapigwa tayari.
 
huyu mtu ananipa maswali sana

hili sakata anataka apate 'nitoke vipi'

au hata huu mvurugano ni pandikizi??
Kama mtera maji yalikuwa yanamwaga ili mgao uwepo hakuna la ajabu kwa 'movie star' huyu.

Tunaweza kuwa tunatoka povu kumbe movie tupu.
 
jmushi1, unaamini huu mgogoro?
Mie naanza kuutilia mashaka, japo sina evidence kwa sasa.
 
Last edited by a moderator:
huyu mtu ananipa maswali sana

hili sakata anataka apate 'nitoke vipi'

au hata huu mvurugano ni pandikizi??
Kama mtera maji yalikuwa yanamwaga ili mgao uwepo hakuna la ajabu kwa 'movie star' huyu.

Tunaweza kuwa tunatoka povu kumbe movie tupu.


Umeona eeeh?
Mwenyewe nilikuwa nawaza the same.
 
Nikikumbuka Mwl Nyerere kabla ya kuanza Vita Uganda alitumia mbinu na fursa zote za kidiplomasia lakini akashindwa. Alikwenda OAU sasa AU, alikwenda UN, alikwenda SADC na kwingineko. Kote huko Id Amin alikaidi. Mwisho Mwalimu akatangaza vita. Sisi Viongozi wetu wamefanya nini? Je tumeomba Mgogoro huu usuluhishwe Kimataifa?? Lazima tujadili mambo haya kwa busara zaidi. Wana JF, matamko haya yanafaa kwa sasa?? Tafakari!
 
Vita baina ya nchi na nchi uleta umoja katika wananchi husika[tanzania vs watanzania] na uadui kati ya raia wanchi na nchi[tanzania vs malawi] njia za kidipromasia uleta umoja baina ya nchi na nchi na raia pia [malawi vs tanzania] chezyea vita wewe?
 
Zipigwe tu. Mbabe aanze kumchokoza mwenzie aone.
 
Maneno ya kujifurahusha hayo! Vijana wa JWTZ hawana morali hata kidogo ! Nani anaenda kupigana vita wakati dhuluma imetapakaa kila sehemu? Hata JWTZ kwenyewe kunafukuta moshi ndani kwa ndani kwa muda mrefu sasa.. Vijana wanaonewa , wanahujumiwa nafasi za masomo, posho halali Na mengine mengi.. Kwa maoni yangu kuingia vitani kipindi hiki imekula kwetu..

hayo ni maoni yako.kama ingekua hivyo wasingeenda kulinda amani nchi za watu.
na kama wangeenda basi wangeharibu nchi ikapata aibu..
NB. japo mie si afande,wakianzisha na-join..navyopenda hizo move!!
nataka kitu 'live',lowasa lianzishe..dhaifu hawezi
 
Haya ndio maneno aliyoshindwa kusema MEMBE juzi Bungeni. Sielewi nani alimwambia Membe awaite wa Malawi ''WENZETU'' wakati wao wanajiandaa kutupiga kivita.

Tangu lini adui akawa mwenzako?

mwenzie Lowassa amesoma mood ya nchi na ameamua ku grab the headlines vilivyo

so far as far as national security is concerned: LOWASSA 1 MEMBE 0

game inaendelea

Niliwahi kusema humu katika uzi mmoja unaohusu hili jambo kuwa tunahitaji viongozi wasiomun'gunya maneneo kama Edwars Lowasa nikirejea alichowajibu wamisri walipoanza kupigia kelele kitendo cha Tanzania kutumia maji ya ziwa victoria kwa kisingizio cha mikataba ya wakoloni nikabezwa...Sikujua kwa nafasi yake atachomoza...when it come to territorial integrity tunahitaji kauli za namna hii hopefully vikosi viko mpakani kumshughulikia yeyote atakayeleta chokochoko....hata ndege inayoruka upande wetu ni kuishusha.... Mazungumzo yaendelee kusisitiza hilo ili wayapate kwenye meza ya mazungumzo...
 
Tunajua viongozi hawapo kwa maslahi ya utaifa; inapotokea maslahi ya Taifa yanatishiwa utaifa daima unawekwa mbele lakini kwa sababu viongozi wapo kimaslahi ya binafsi zaidi wanakuwa kimya, hivi unategemea viongozi kesho tutakawapa dhamana ya kulinda mipaka yetu wataweza? Lakini sishangai sio ndio mbunge alisema Arusha itajitenga? au watu Mbinga sio watanzania.

Chama
Gongo la mboto DSM
Chama tumia brain ndugu yangu, kutoa tamko sio kuonyesha uzalendo/utaifa kama unavyotaka tuamini! Kuvamiwa mipaka yetu ni jambo linalomtaka amiri jeshi mkuu kulitolea tamko, lakini ajabu mpaka sasa matamko yanatolewa na watendaji wake - ni sawa diplomasia kuchukua nafasi yake lakini kilichofanywa na kamati ya EL kilipaswa kufanywa na mkuu wa kaya.
 
vijana waliopelekwa mpakani wengi ni new comerz kwenye jeshi, bado hawana uzoefu hao ndio watakuwa frontliners
 
Suala hili la uvamizi liko mahakamani, si vema sana kulizungumzia tutaingilia uhuru wa mahakama. Wazambia wanadai mambo makubwa sana ambapo taifa Kwa Sasa haliwezi kuwatimizia..
eng,hivi kweli upo dunia hii? JK KAINGILIA MAHAKAMA,mgomo wa walimu.
serikali ya tz imeipuuza mahakama kwa kuvunja sheria ya kuhukumu na kulifungia mwanahalisi.
wakati chombo kinachotafasili sheria ni mahakama.
sasa ukisema jambo lipo mahakamani cha ajabu nini..
kwa tuna mahakama sisi,au magenge ya magambaz!
 
Nikikumbuka Mwl Nyerere kabla ya kuanza Vita Uganda alitumia mbinu na fursa zote za kidiplomasia lakini akashindwa. Alikwenda OAU sasa AU, alikwenda UN, alikwenda SADC na kwingineko. Kote huko Id Amin alikaidi. Mwisho Mwalimu akatangaza vita. Sisi Viongozi wetu wamefanya nini? Je tumeomba Mgogoro huu usuluhishwe Kimataifa?? Lazima tujadili mambo haya kwa busara zaidi. Wana JF, matamko haya yanafaa kwa sasa?? Tafakari!
Mkuu ni vyema kuweka msimamo wako dhahiri ili uende kwenye meza ya mazungumzo ukiwa na msimamo huo.....Fanya yote usichezee mipaka ya nchi.
 
Hata status ya jeshi letu si Lowassa mwenye mamlaka ya kulizungumzia. It is simply cheap politics. Where is our commander in chief? Hivi, wakati wa chokochoko za Idd Amin mlimsikia Kawawa au mbuge yeyote yule akizungumzia juu ya utayari wa jeshi letu? Hiyo ilikuwa kazi ya Commander in Chief. Na as long as we have one, unless you want to tell me we do not have one, no one else can speak on behalf of the readiness of our JWTZ.

How if the commander in chief is weak??
 
Back
Top Bottom