Lowassa: Rushwa ni kansa inayoitafuna nchi

Lowassa: Rushwa ni kansa inayoitafuna nchi

ipad

Member
Joined
Jan 25, 2013
Posts
21
Reaction score
2
Aliyepata kuwa Waziri Mkuu wa Tanzania,Edward Lowassa amesema rushwa nchini ni kansa inayoitafuna nchi,amesema hayo mchana huu akihojiwa na idhaa ya kiswahili ya DW, Pamoja na hayo amesisitiza kuwa hana kundi ndani ya CCM.

Mahojiano;


  • Haya ni dondoo za mahojiana ya Lowassa na mtangazaji wa DW yaliorushwa ktk matangazo ya leo mchana

    Mtangazaji: Maoni yako hukusu rushwa
    Lowassa: "Rushwa ni canser ndani ya jamii ", yanazungumzwa mengi ila nikwambie mtangazaji tuna TAKUKURU inafanya kazi nzuri na pia nina
    imani na bosi wake anafanya kazi nzuri ila kazi hiyo ni ngumu sana inahitaji ushirikiano wa jamii na pia kuna dosari za kisheria.

    Mtangazaji: Je ni dosari gani za kisheria
    Lowassa: Wenyewe PCCB wamedai kuna dosari ktk sheria waulize wenyewe watakueleza zaidi

    Mtangazaji:Inaelezwa kunamakundi ndani ya CCM na ww ni mmojawapo, je una kundi?
    Lowassa: Hapana, unajua wakati wa uchaguzi kila mmoja huwa na kundi lake ila kwa CCM baada ya kumpata mshindi basi makundi yote yanaishia hapo na tunakua kitu kimmoja. na kama ni kuwa nakundi basi kundi langu ni "CCM"

    Mtangazaji: Je utagombea urais 2015
    Lowassa: bado kuna miaka 3, unajiandaaje kuvuka daraka kabla hujalifikia! basi nikishavuka daraja ndio nitasema kama nitagombea

    Mtangazaji: Sauti inapazwa umefika wakati Rais ajaye awe Mwanamke
    Lowassa: sipendi kulizungumzia kwa sasa subirini hadi muda utakapofika

    Mtangazaji: Unazungumziaje Muungano uliopo na je zipo kero
    Lowassa: Muungano unaendlea uzuri ila zipo kero lakini hata kwny ndoa kero zipo muhimu ni kwavipi mnazishuhulikia hizo kero

    Mtangazaji: je maoni yako juu ya muundo wa muungano wakati huu wa utungaji wa katiba mpya
    Lowassa: Mimi niachie mjadala uendelee na baadae nitatoa msimamo wangu

    Mtangazaji: Je ikiamuliwa uwe muungano wa serikali 3 au wa mkataba
    Lowassa: Watakavyoamua wananchi ndio sawa na nitaunga mkono​


 
sasa kazi ipo hapa naona ndio yale yale ambayo mkuu wa kaya alisema yeye mwenyewe anashangaa kwamba wakina mama nao wanapokula rushwa ahahaha kweli haya mambo magumu
 
Na yeye ndiye one of the waasisi maana ile ya Richmond hajakanusha hadi leo.lol!
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Pia amesema,suala hili la Rushwa linamsononesha sana.
 
Haya ni dondoo za mahojiana ya Lowassa na mtangazaji wa DW yaliorushwa ktk matangazo ya leo mchana

Mtangazaji: Maoni yako hukusu rushwa
Lowassa: "Rushwa ni canser ndani ya jamii ", yanazungumzwa mengi ila nikwambie mtangazaji tuna TAKUKURU inafanya kazi nzuri na pia nina
imani na bosi wake anafanya kazi nzuri ila kazi hiyo ni ngumu sana inahitaji ushirikiano wa jamii na pia kuna dosari za kisheria.

Mtangazaji: Je ni dosari gani za kisheria
Lowassa: Wenyewe PCCB wamedai kuna dosari ktk sheria waulize wenyewe watakueleza zaidi

Mtangazaji:Inaelezwa kunamakundi ndani ya CCM na ww ni mmojawapo, je una kundi?
Lowassa: Hapana, unajua wakati wa uchaguzi kila mmoja huwa na kundi lake ila kwa CCM baada ya kumpata mshindi basi makundi yote yanaishia hapo na tunakua kitu kimmoja. na kama ni kuwa nakundi basi kundi langu ni "CCM"

Mtangazaji: Je utagombea urais 2015
Lowassa: bado kuna miaka 3, unajiandaaje kuvuka daraka kabla hujalifikia! basi nikishavuka daraja ndio nitasema kama nitagombea

Mtangazaji: Sauti inapazwa umefika wakati Rais ajaye awe Mwanamke
Lowassa: sipendi kulizungumzia kwa sasa subirini hadi muda utakapofika

Mtangazaji: Unazungumziaje Muungano uliopo na je zipo kero
Lowassa: Muungano unaendlea uzuri ila zipo kero lakini hata kwny ndoa kero zipo muhimu ni kwavipi mnazishuhulikia hizo kero

Mtangazaji: je maoni yako juu ya muundo wa muungano wakati huu wa utungaji wa katiba mpya
Lowassa: Mimi niachie mjadala uendelee na baadae nitatoa msimamo wangu

Mtangazaji: Je ikiamuliwa uwe muungano wa serikali 3 au wa mkataba
Lowassa: Watakavyoamua wananchi ndio sawa na nitaunga mkono
 
Ameshindwa kutoa maoni yake juu ya utendaji kazi wa wanawake licha ya kushika nyadhifa kubwa serikalin.Kwa tafsiri yangu ni kwamba ameogaopa kuwapaisha wanawake
 
Kama ndiyo alivyosema , basi sawa , bali atambue kwamba hiyo kansa ni pamoja na kuwanunulia Wamasai pombe na nyama choma ili aendelee kuwa juu , kansa hiyo pia ni pamoja na yale mahela ( 3 bill ) zilizomwagwa kwenye uchaguzi wa UWT peke yake ! Lakini anapaswa kujua kwamba kila siku siyo jumapili !
 
Wala msiwapunje watu vitu vyao, wala msifanye jeuri kwa ufisadi. (Ash-Shu'araa: 183)

Na katika watu yupo yule ambaye maneno yake kwa maisha ya kidunia hukufurahisha; naye humshuhudisha Mwenyezi Mungu kwa yaliyomo moyoni mwake, na hali yeye ndiye mkubwa wa ukhasimu. [2:204]

Na anapo tawala hufanya juhudi katika nchi kwa kufisidi humo na kuteketeza mimea na viumbe. Na Mwenyezi Mungu hapendi ufisadi. [2:205].

Na akiambiwa: Mwogope Mwenyezi Mungu, hupandwa na mori wa kutenda madhambi. Basi huyo inamtosha Jahannam. Paovu mno hapo kwa mapumziko. [2:206]

Na kumbukeni alivyo kufanyeni wa kushika pahala pa A'adi na akakuwekeni vizuri katika nchi, mnajenga majumba ya fakhari katika nyanda zake, na mnachonga majumba katika milima. Basi zikumbukeni neema za Mwenyezi Mungu wala msitende uovu katika nchi kwa ufisadi[7:74]
Na utafute, kwa aliyo kupa Mwenyezi Mungu, makaazi ya Akhera. Wala usisahau fungu lako la dunia. Nawe fanya wema kama Mwenyezi Mungu alivyo kufanyia wema wewe. Wala usitafute kufanya ufisadi katika ardhi. Hakika Mwenyezi Mungu hawapendi mafisadi. (Al-Qasas: 77)

Dah maneno mazito haya ya M.Mungu kumbe ndio maana nchi yetu watu wameanza kupigana na police na kuichukia serikali
 
Eti huyu awe Raisi, raisi gani hawezi hata jibu maswali redioni kwa kiswahili
 
Jamani kilaza mwingine huyo anakuja, hivi kasoma huyu? au ndio nyakati za mwisho Mungu anatuonesha mtu mfu? Ubarikiwe Yahweee,.... aende akachunge ng'ombe huyu
 
Rais asiyetaka kusoma: Hajui sheria gani Takukuru inawapa shida bali amesikia kunatatizo la kisheria! huyu ndo aje awe rais na ameshindwa kutambua jambo dogo tu ambalo sio lazima uende shule au upitie makabrasha ya takukuru!!.
 
Wala msiwapunje watu vitu vyao, wala msifanye jeuri kwa ufisadi. (Ash-Shu'araa: 183)

Na katika watu yupo yule ambaye maneno yake kwa maisha ya kidunia hukufurahisha; naye humshuhudisha Mwenyezi Mungu kwa yaliyomo moyoni mwake, na hali yeye ndiye mkubwa wa ukhasimu. [2:204]

Na anapo tawala hufanya juhudi katika nchi kwa kufisidi humo na kuteketeza mimea na viumbe. Na Mwenyezi Mungu hapendi ufisadi. [2:205].

Na akiambiwa: Mwogope Mwenyezi Mungu, hupandwa na mori wa kutenda madhambi. Basi huyo inamtosha Jahannam. Paovu mno hapo kwa mapumziko. [2:206]

Na kumbukeni alivyo kufanyeni wa kushika pahala pa A'adi na akakuwekeni vizuri katika nchi, mnajenga majumba ya fakhari katika nyanda zake, na mnachonga majumba katika milima. Basi zikumbukeni neema za Mwenyezi Mungu wala msitende uovu katika nchi kwa ufisadi[7:74]
Na utafute, kwa aliyo kupa Mwenyezi Mungu, makaazi ya Akhera. Wala usisahau fungu lako la dunia. Nawe fanya wema kama Mwenyezi Mungu alivyo kufanyia wema wewe. Wala usitafute kufanya ufisadi katika ardhi. Hakika Mwenyezi Mungu hawapendi mafisadi. (Al-Qasas: 77)

Dah maneno mazito haya ya M.Mungu kumbe ndio maana nchi yetu watu wameanza kupigana na police na kuichukia serikali

Nakugongea ' Like '
 
Nakugongea ' Like '

umeona eeh nami numekugongea aisee maana leo nilisema hebu niangalie hiki kitabu kunanini kwanini watu wanachukia serikali yao hivi kumbe hata Mungu anachukia

na anawachukia hata wale wa weka mbali na tembo hebu ona hii

Na anapo tawala hufanya juhudi katika nchi kwa kufisidi humo na kuteketeza mimea na viumbe. Na Mwenyezi Mungu hapendi ufisadi. [2:205].
 
Back
Top Bottom