Lowassa: Nitamtoa Babu Seya gerezani

Lowassa: Nitamtoa Babu Seya gerezani

Status
Not open for further replies.
alitolewa baraba sembuse babu seya, tunam miss huku kitaa, nguza viking aje aungane na king kikii tupate burudani mambo ya kitambaa cheupe, mwanameka, fungua njia kitoto chaanza tambaaa, le capitano
 
Duh ila hapa tulipofikia kwakweli Watanzania tunahitaji msaada wa Mungu tu,Sisi wenyewe tayari tumeshaharibu mno,nchi imekuwa ya hovyo kabisa.Uchaguzi huu ulipaswa kuwa wa kusisimua sana,ukiwapambanisha wagombea walio na mawazo bora na yenye ubunifu wa hali ya juu,wagombea wenye uwezo mkubwa wa kujenga hoja,wenye CV za kusisimua.Mambo yamekuwa kinyume kabisa,chama kilichopo madarakani tayari kimeshapitisha sheria nyingi mbovu na kandamizi kama ile sheria ya uhalifu wa mtandao, hakika hawapaswi kurudi madarakani kabisa maana maisha ya Watanzania yatakuwa mabaya mno chini ya utawala wao wa miaka ijayo na hasa kama huyu dikteta Dr Magufuli atashinda.
Nikiangalia upande wa pili nako kusema ukweli hakuna kinachonivutia kuhusu mgombea wao wa urais,huyu hawezi kuwa aina ya rais atakayenifanya nitembee kifua mbele.Kwakweli hafikii vile viwango ninavyovitaka mtu yeyote anayetaka kuwa rais wa nchi hii avifikie,hasa uelewa wake juu ya suluhisho zinazohitajika katika kukabiliana na changamoto zitokanazo na ulimwengu tunaoishi leo,sidhani kama Lowassa ana uwezo wa kupambana na complex issues. Halafu mimi na yeye tunatofautiana mno katika suala la bodaboda,natamani apatikane kiongozi mwenye kujielewa akatuondolea hawa bodaboda maeneo ya mijini,wao wamekuwa sababu kubwa ya kutokea kwa ajali mijini kwasababu wengine hawana elimu ya sheria za usalama barabarani.Ni vyema bodaboda zikapelekwa maeneo yaliyo nje ya mji.
All in all katika uchaguzi huu tunaletewa two choices;ni kati ya chama kibovu kabisa kilichopoteza legitimacy ya kuendelea kuongoza nchi yetu kutokana na rekodi zake mbovu kama watawala vs mgombea mbovu ambaye hana msisimko.Ila itakapokuja wapi tupeleke kura zetu,kwakweli itabidi tutumie ile kanuni yetu ya 'the lesser of the two evils'.CCM/Magufuri na Lowassa wote ni evils, ila Lowassa ni evil mwenye afadhali kwakuwa akichaguliwa atafanya kazi kwa kufuata misingi na miongozo ya UKAWA.CCM?watafuata misingi na miongozo yao ya siku zote ambayo ni kuwakandamiza wananchi wa Tanzania.
 
kesi kama ya babu seya adhabu inatakiwa iwe kudeki tu barabara, basi wezi wa mali ya umma ndio wanatakiwa kuwa segerea
 
Babu seya kaonewa hakuna cha kuvunja sheria bali atazifundisha taasisi zinazobaka sheria
 
Lowassa ni mgonjwa anajisemea hovyo. Kinachofanya kazi ni pesa zake na si yeye.

Completely rubbish!!!. Una uhakika? Kasema lini? Na wapi? Kama hauna ushahidi funga hilo bakuli lako. Sijui umekula maharage ya wapi wewe????
 
Sera za Lowassa ni hatari sana, kwahiyo kwa hili nalo watu wakapiga makofi siyo? nilijua atatwambia kwanini Masai wenzie wanahamia mjini kulinda mageti ya watu kumbe ndo yale yale ya kutafuta SIFA ZA KIJINGA ..ndo maana Mwl. Nyerere alituhonya tusiwe na akiri za kijinga kama za Lowassa, asante sana Baba wa Taifa
 
Lowassa ni mgonjwa anajisemea hovyo. Kinachofanya kazi ni pesa zake na si yeye.

Completely rubbish!!!!. Kasema lini? Na wapi? Una ushahidi? Kama huna ushahidi funga hilo bakuli lako. Sujui umekula maharage ya wapi wewe. Wewe una chuki binafsi na Lowassa, hakuna jingine. Ni chuki tu inakusumbua, na hakuna lingine.Poleeee!!!
 
Huyu mzee hovyo kabisa kumtoa babu seya kunawahusu nn watanzania wanaotaka maendeleo?? Au ndo mabadiliko yenyewe haya??!!!
 
Anajua kwann alifugwa c aliyekuwa rafk yake ndio kamuweka ndan
 
Lowassa ni mgonjwa anajisemea hovyo. Kinachofanya kazi ni pesa zake na si yeye.

Rubbish!!! Una uhakika? Kasema lini? Na wapi? Kama una ushahidi nakushauri ukae kimya tu. Wewe ni chuki tu binafsi dhidi ya Lowassa inakusumbua. Polee!!!
 
Ni mtanzania gan asiyejua kua Babu seya alidhulumiwa, kafungwa kisa alikua anamega kisela mzigo wa kiwete! BIG UP LOWASA

Ha ha ha ha ha aaaaaa! Kak kuna sheria ya makosa ya mtandao inaanza tarehe mosi september
 
Tutasikia na sera zisizo na mashiko kama hizi. Who is Babu Seya to the livelihood of people? We need concrete policies and strategies to alleviate the people and nation to middle income level. It is possible just use your brain to sort them out
 
huyu kasoma kichwa cha habari fedha ya kununua gazeti la kufungia anzaji na vitumbua uhuru hakuwa nazo.
 
Kila mzazi anajua uchungu wa mototo na mahangaiko anayopata mazazi katika kumlea mwanae, halafu anatokea "Mario" mwenye akili timamu anaanza kuchezea watoto wa wenzie anakamatwa anafikishwa katika vyombo vya sharia anahukumiwa anakata rufaa anashindwa nayeye anaridhika.

Halafu anatokea mtu mmoja kwa sababu anazozijua yeye anasema atamwachia huru mtu aliyepatikana na hatia ya kunajisi watoto, hapana kabisa huo upumbavu siwezi kuungana nao hata kama kwa namna gani.

Sote tunajua uchafu unaofanywa na hawa akina "Mario" sasa wanadhibitiwa mtu mmoja kwa njaa yake ya madaraka anataka kuwaachia huru, tutawatia kiberiti labda akiwaachia awarudishe makwao.

Wapo waliopatikana na hatia wakitetea haki zao, mfano fransis cheka, mbona hasemi atamwachia? wapo wanaohangaika jela kwa kutetea imani za dini yao kama sheikh Ponda na wapo walioko jela kutetea maslahi yao kama sheikh Farid hao kwake sio kitu ila huyu mbakaji tu.

Zipo NGO nyingi zimehangaika kutetea haki za watoto kama kuzuia ukeketaji, mimba za utotoni na haki ya elimu. Zimetumia fedha nyingi na rasilimali nyingi kupambana na matatizo ya watoto, leo mtu aliyewahi kushika nafasi za juu serikalini hili kwake sio hoja, anaona wabakaji ni watu wanaofanyiwa fitina tu, hapana.

Wakati wa sakata la Richmond bungeni, Niliwahi kumsikia mama kilango akilalamika kuletewa ki memo na chifupa kutoka kwa mheshimiwa sasa naamini hapa sio bure kwa huyu mwenzetu, tuchukue tahadhari.
 
Nimestuka Lowassa kudharau utawala wa sheria. Babuseya alikata rufaa mahakama kuu ya Tanzania na kushindwa kwa kosa la ubakaji na udhalilishaji watoto.

Je Lowassa hautambui mhimili wa mahakama? Je utaachia wafungwa wote?

Lowassa ataleta mgongano wa kidola.

Chanzo: Raia Tanzania

Ni moja ya utawala bora rais mpya anapoingia madarakani kuwasamehe wafungwa ili aanze ukurasa mpya ni moja kati ya kujenga upendo na raia hilo mbona lipo wazi mkuu
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom