kanga
JF-Expert Member
- Jan 13, 2011
- 1,025
- 494
Nimejaribu kuangalia watangaza nia karibu wote wanawapambe wao wa karibu na wengine ni viongozi waandamizi wa serikali iliyopo au zilizopita. Tofauiti na wengine Team Lowassa wapambe wake wengi ni majeruhi wa mfumo au serikali ya Kikwete iliyopo madarakani kwa wakati huu.Jambo muhimu la kujiuliza je imetokea kwa bahati mbaya au wana malengo sawa na nia moja au wana ajenda ya siri?.Hebu angalia orodha fupi kwa watu maarufu au viongozi majeruhi waliojitokeza siku ya kutangaza nia yake hapo Amri Abeid stadium Arusha.-Karamagi, Tibaijuka,Mulugo, Ngansongwa,Maige,Mathayo n.k kwa uchache. Je kwa nini isiaminishwe kuwa Team Lowassa kule kwetu tuliopita mafunzo ya usalama ameanza gwaride na mguu wa kushoto kuanguka kwake kuko wazi?.