Lowassa na Wagombea Wengine Waimarishiwe Ulinzi na Uhuru Wao Usibanwe

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,478
39,998
Suala la Lowassa kutembea kwenye dalala au kwenda Bunju au Maneromango ni suala la hekima za kiongozi. Polisi wameshindwa kutoa sababu ya msingi hasa ambayo inahusiana na usalama wa wagombea wenyewe na watu wengine. Mgombea wa Urais ni mtu mzito kwa wadhifa wake na potential yake kama Rais. Hekima inampasa mtu huyo kucoordinate ziara yake mahali popote pale na vyombo vya usalama vya eneo husika. Kwa mfano, ingetokea tu kuwa msongamano wa watu wenye kumshabikia Lowassa unakanyagana na tunasikia watoto watatu au watu kadhaa wamekufa tutaweza kweli kutetea kuwa ni haki yake kutembea popote? Potential ya disaster ni kubwa sana.

Kwa upande mwingine - na hili ni upungufu mkubwa sana wa serikali - mgombea wa Urais anapotangazwa tu kuwa ni mgombea rasmi na Tume, Vikosi vya Usalama wa Taifa vinapaswa kuchukua majukumu yote ya ulinzi wake siyo majukumu ya kumpangia wapi pa kwenda bali kuhakikisha kila anapokwenda yeye na mgombea mwenza wako salama. Hili ni jukumu la kawaida na la lazima.

Polisi na vyombo vya usalama wanatakiwa wakae pamoja na viongozi wa CCM na CDM na wagombea wengine kulingana na nafasi zao kuwapa ulinzi wa kutosha. Lowassa kwanza kabisa anatakiwa awe na ulinzi wake kama Waziri Mkuu wa zamani (kama haujaondolewa bila sababu ya msingi) na kuongezewa ulinzi kama Mgombea wa Urais. Ulinzi huu wa ziada siyo wa wagombea wa CCM na CHADEMA tu bali wa wagombea wengine wa Urais; ukiwemo ulinzi wa nyumbani kwao.

Hata kwa sisi ambao si waumini au wafuasi wa safari isiyo na lengo suala la usalama wa wagombea linaweza kuepusha sintojua za huko mbeleni. Lakini kusema mtu asiende mahali au kukutana na watu fulani ni dalili moja ya kutokuwa na weledi. Hivi Jeshi la Polisi katika vyuo vyake vyote na mafunzo ya maafisa wake wote hakuna ambaye anaweza kufikiria njiabora ya kuhakikisha usalama na uhuru wa wagombea? Vinginevyo, itaonekana (na zipo sababu za kuona hivyo) kuwa Jeshi la Polisi kwa mara nyingine linaonesha u-policcm wake.

MMM
 
Kiongozi anapo amua kupanda dala dala bila ya kufahamisha authorities unategemea nini? Lowassa bado hajaelewa kuwa anagombea nafasi ya Urais na sio Ubunge.
 
Siku hizi kunatungwa sheria baada ya lowassa kufanya jambo

lowassa kasindikizwa kuchukua fomu siku ya pili wakakataza kusindikizwa na watu (jiji lilisimama shughuli zote)

kaenda kwenye msiba wamenzuia asiende

kapanda daladala inatoka sheria wagombea hawaruhusiwi kupanda daladala japo ukweli aliyepanda daladala nu mgombea mmoja

ameenda sokoni oo mgombea haruhusiwi kwenda sokoni

kanywa maji ya kiroba yamezuiliwa hayo maji (hapa wameniudhi ndio maji yangu haya lofa mimi)

hizi nazitafsiri ni sheria against Lowassa

Nasubiri siku watakayo kataza kunya kisa wamejua Lowassa anakunya

lets wait and see time will tell
 
Tabu ya serikali ya CCM inaongozwa kwa mihemko, hizi marufuku marufuku zinazotoka kwanza hazizingatii sheria na pia hazitoi suluhisho la muda mfupi au kudumu wa hicho kinachodhaniwa kuwa ni tatizo. Lowassa sasa hivi anaonekana kero kisa yupo upinzani.

Nani anajua Dovutwa yuko wapi leo au anatembelea nn?
 
huuuuu ndio usafiri wa malofa na wapumbavu hahahahahha

na haya ndio maji ya malofa na wapumbavu


najua hawataki kujumuika na malofa
 
Siku hizi kunatungwa sheria baada ya lowassa kufanya jambo

lowassa kasindikizwa kuchukua fomu siku ya pili wakakataza kusindikizwa na watu (jiji lilisimama shughuli zote)

kaenda kwenye msiba wamenzuia asiende

kapanda daladala inatoka sheria wagombea hawaruhusiwi kupanda daladala japo ukweli aliyepanda daladala nu mgombea mmoja

ameenda sokoni oo mgombea haruhusiwi kwenda sokoni

kanywa maji ya kiroba yamezuiliwa hayo maji (hapa wameniudhi ndio maji yangu haya lofa mimi)

hizi nazitafsiri ni sheria against Lowassa

Nasubiri siku watakayo kataza kunya kisa wamejua Lowassa anakunya

lets wait and see time will tell

ha ha ha

sasa hivi wana mpango wa kuzuia watu kula kwa mama ntilie kwa vile Lowasa alikamata kikombe cha uji
 
Haya mnayoyataka hata akiwa yeye Rais hayatowezekana. . . . . . Tusubiri!!!!!!
 
Haya mnayoyataka hata akiwa yeye Rais hayatowezekana. . . . . . Tusubiri!!!!!!

Wagombea wote wapewe ulinzi sawa kuanzia wa ccm hadi act sasa jeshi la polisi limeshindwa kufanya kazi ccm wamezidisha muda wa kampeni walitakiwa hili kova alikemee kwa sababu chama kingine kisirudie sasa na siyo kusubiri upinzani ndio kutoa matamko
 
Mwaka 2012, Rais wa Ufaransa (Hollande) alitangaza kuanza kutumia usafiri wa umma (Treni) ndani ya ufaransa lakini na pia kwenda kwenye vikao vya Umoja wa Ulaya jijini Brussels.

Kuanzia Mwaka 2010 ,Waziri Mkuu wa Uingereza (Cameroon), amekuwa akitumia treni mara kwa mara na akawaagiza Mawaziri wake waanze kutumia vyombo vya usafiri wa umma (Treni) badala ya usafiri binafsi.

Hawa ni viongozi wa nchi, kwanini iwe tatizo kwa mgombea Urais? Zipo faida nyingi kwa Lowassa kufanya hivyo katika muktadha wa nchi yetu, chache zikiwa ni pamoja na:

1. Kujenga imani ya wananchi juu ya mfumo wa usafiri wa umma, mfumo ambao wananchi wengi wanautumia kwa vile tu hawana namna. Matumizi makubwa ya mfumo huu kwa watu wengi zaidi utasaidia sana kupunguza foleni zinazotokana na wingi wa magari.

2. Akiwa kama mgombea urais, kitendo cha Lowassa kutumia usafiri wa umma kunamfanya aone adha na kero zilizopo katika mfumo huo, first hand.

3. Akiwa kama mgombea urais, anapata fursa ya kukutana na wananchi ana kwa ana wakiwa katika shughuli zao za ujenzi wa taifa na kujionea kinachowasibu.

Kwanini tusione faida kubwa katika hili? Aina hii ya uongozi ina fursa kubwa zaidi ya kutunga sera ambazo zinaendana na uhalisia wa maisha ya watanzania.

Wakati haya yakiendelea, mgombea urais wa CCM John Magufuli, Jana (25/08/2015) amewaeleza wananchi wa Rukwa kwamba tofauti na wagombea urais wengine watakaopita mikoani, yeye kwa kampeni nzima, hatatumia usafiri wa anga bali usafiri wa gari kwa hoja kwamba "nataka niteseke nanyi". Hiyo ndio sababu yake ya msingi, "Kuteseka na Wananchi". Suala la ulinzi wake katika ziara ya maelfu ya kilometa nchi nzima, hilo kwa polisi halina shida.

Tukirudi kwenye hoja ya magufuli na matumizi ya barabara, kwa maana hiyo, matumizi ya usafiri wa barabara kwa viongozi huwa ni mateso. Ndio maana siku ya kwanza kwenda Mwanza kujitambulisha baada ya kuteuliwa kuwa mgombea Urais, alipanda ndege ya serikali (walipa kodi), na hakwenda na gari. Pia, kwa maana hiyo, zaidi ya wananchi 90% ambao hutumia usafiri wa ardhini, wananchi hao wanaishi kwa mateso makubwa sana.

Ukiyashangaa ya MKAPA, utayaona ya MAGUFULI.
 
Ni ukweli usiopingika mkuu, Obama alianza kula protection ya secret service hata kabla hajawa Democrat nominee, but then ilikua ni nchi ya utawala wa haki na sheria.
 
Suala la Lowassa kutembea kwenye dalala au kwenda Bunju au Maneromango ni suala la hekima za kiongozi. Polisi wameshindwa kutoa sababu ya msingi hasa ambayo inahusiana na usalama wa wagombea wenyewe na watu wengine. Mgombea wa Urais ni mtu mzito kwa wadhifa wake na potential yake kama Rais. Hekima inampasa mtu huyo kucoordinate ziara yake mahali popote pale na vyombo vya usalama vya eneo husika. Kwa mfano, ingetokea tu kuwa msongamano wa watu wenye kumshabikia Lowassa unakanyagana na tunasikia watoto watatu au watu kadhaa wamekufa tutaweza kweli kutetea kuwa ni haki yake kutembea popote? Potential ya disaster ni kubwa sana.

Kwa upande mwingine - na hili ni upungufu mkubwa sana wa serikali - mgombea wa Urais anapotangazwa tu kuwa ni mgombea rasmi na Tume, Vikosi vya Usalama wa Taifa vinapaswa kuchukua majukumu yote ya ulinzi wake siyo majukumu ya kumpangia wapi pa kwenda bali kuhakikisha kila anapokwenda yeye na mgombea mwenza wako salama. Hili ni jukumu la kawaida na la lazima.

Polisi na vyombo vya usalama wanatakiwa wakae pamoja na viongozi wa CCM na CDM na wagombea wengine kulingana na nafasi zao kuwapa ulinzi wa kutosha. Lowassa kwanza kabisa anatakiwa awe na ulinzi wake kama Waziri Mkuu wa zamani (kama haujaondolewa bila sababu ya msingi) na kuongezewa ulinzi kama Mgombea wa Urais. Ulinzi huu wa ziada siyo wa wagombea wa CCM na CHADEMA tu bali wa wagombea wengine wa Urais; ukiwemo ulinzi wa nyumbani kwao.

Hata kwa sisi ambao si waumini au wafuasi wa safari isiyo na lengo suala la usalama wa wagombea linaweza kuepusha sintojua za huko mbeleni. Lakini kusema mtu asiende mahali au kukutana na watu fulani ni dalili moja ya kutokuwa na weledi. Hivi Jeshi la Polisi katika vyuo vyake vyote na mafunzo ya maafisa wake wote hakuna ambaye anaweza kufikiria njiabora ya kuhakikisha usalama na uhuru wa wagombea? Vinginevyo, itaonekana (na zipo sababu za kuona hivyo) kuwa Jeshi la Polisi kwa mara nyingine linaonesha u-policcm wake.

MMM

Mzee Mwanakijiji, naweza kuungana na wewe. Lakini ni kweli serikali inataka wawe na ulinzi, unaweza kuamini kweli walinzi wa CCM kwa mtu ambaye ana high potential ya kuiondoa CCM madarakani? To be more realistic serikali inataka Magaufuli awe rais, and they will do whatever they can to that end. Upolisi wa CCM ni wazi na utaendelea kuwa hivyo. Wanachojali sasa ni urais, usalama wa watu hakuna anayeujali.
 
Mwaka 2012, Rais wa Ufaransa (Hollande) alitangaza kuanza kutumia usafiri wa umma (Treni) ndani ya ufaransa lakini na pia kwenda kwenye vikao vya Umoja wa Ulaya jijini Brussels.

Kuanzia Mwaka 2010 ,Waziri Mkuu wa Uingereza (Cameroon), amekuwa akitumia treni mara kwa mara na akawaagiza Mawaziri wake waanze kutumia vyombo vya usafiri wa umma (Treni) badala ya usafiri binafsi.

Hawa ni viongozi wa nchi, kwanini iwe tatizo kwa mgombea Urais? Zipo faida nyingi kwa Lowassa kufanya hivyo katika muktadha wa nchi yetu, chache zikiwa ni pamoja na:

1. Kujenga imani ya wananchi juu ya mfumo wa usafiri wa umma, mfumo ambao wananchi wengi wanautumia kwa vile tu hawana namna. Matumizi makubwa ya mfumo huu kwa watu wengi zaidi utasaidia sana kupunguza foleni zinazotokana na wingi wa magari.

2. Akiwa kama mgombea urais, kitendo cha Lowassa kutumia usafiri wa umma kunamfanya aone adha na kero zilizopo katika mfumo huo, first hand.

3. Akiwa kama mgombea urais, anapata fursa ya kukutana na wananchi ana kwa ana wakiwa katika shughuli zao za ujenzi wa taifa na kujionea kinachowasibu.

Kwanini tusione faida kubwa katika hili? Aina hii ya uongozi ina fursa kubwa zaidi ya kutunga sera ambazo zinaendana na uhalisia wa maisha ya watanzania.

Wakati haya yakiendelea, mgombea urais wa CCM John Magufuli, Jana (25/08/2015) amewaeleza wananchi wa Rukwa kwamba tofauti na wagombea urais wengine watakaopita mikoani, yeye kwa kampeni nzima, hatatumia usafiri wa anga bali usafiri wa gari kwa hoja kwamba "nataka niteseke nanyi". Hiyo ndio sababu yake ya msingi, "Kuteseka na Wananchi". Suala la ulinzi wake katika ziara ya maelfu ya kilometa nchi nzima, hilo kwa polisi halina shida.

Tukirudi kwenye hoja ya magufuli na matumizi ya barabara, kwa maana hiyo, matumizi ya usafiri wa barabara kwa viongozi huwa ni mateso. Ndio maana siku ya kwanza kwenda Mwanza kujitambulisha baada ya kuteuliwa kuwa mgombea Urais, alipanda ndege ya serikali (walipa kodi), na hakwenda na gari. Pia, kwa maana hiyo, zaidi ya wananchi 90% ambao hutumia usafiri wa ardhini, wananchi hao wanaishi kwa mateso makubwa sana.

Ukiyashangaa ya MKAPA, utayaona ya MAGUFULI.

Hakika. Jana Nilimsikiliza Magufuli,ati anataka ateseke na malofa wa huko maporini kwa kutopanda Helicopter,badala yake atatumia VX V8 yake.
Lakini nilitegemea atasema," Nataka nitembee kwa miguu au nipande baskeli" ili nioneshe ushirika wa mateso nanyi malofa. Vinginevyo ....
 
Tutaelewana tu na itafahamika kati ya sisi malofa aka wapumbavu na wale wenye matumbo mapana ni yupi anayemuweka mtu madarakani..
 
Kiongozi anapo amua kupanda dala dala bila ya kufahamisha authorities unategemea nini? Lowassa bado hajaelewa kuwa anagombea nafasi ya Urais na sio Ubunge.
Kwani akigombea uraisi anatakiwa atengane na wapiga kura?
 
Back
Top Bottom