Lowassa na siasa za makanisani?

Lowassa na siasa za makanisani?

atoaye kwa wingi pesa za wajenzi huru na ziada au kwa Moyo acha ujinga wewe.Anatoa zake au za watz alizokwisha fyonza sana

Mkuu hujui hata Shetani (Freemason) hubariki kutokana na utoaji?
 
mkuu asafishike kivipi? Kwani ni mchafu? Hebu weka hapa uchafu wake...usifuate mkumbo! God bless u El.

We jipe moyo tu lakini huyo mtu wako uraisi haupati. Hakuna anae taka Lowasa asibarikiwe na Mungu, watu hawamtaki tu kama raisi wao. Kwa hiyo usihofu hizo baraka atazipata tu.
 
bora hela zake anazirudisha kufanyia kazi ya mungu...ningewaomba akina ngeleja,mkulo na maige wafanye hivyo hivyo na wao...watabarikiwa na bwana!!
 
Tangia anyofelewe kwenye Uwaziri mkuu kwa kashfa kubwa ya kuliingiza taifa gizani kwa mikataba ya kilaghai Bw E Lowasa amekuwa akionekana kwenye madhehebu mbalimbali na kitita cha fedha kuwasaidia ama kununua vinanda, madirisha, matofali, redio, viwanja, sherehe nk huku akiaambatana na kundi kubwa kumsaidia kuchangia hizo harambee.

Ameifanya ili kujitakasa na kile alichokifanya akiwa madarakani.

JK alitumia nyumba za ibada kuingia ikulu madhara yake wote tunayaona. E Lowassa kajikita kwenye nyumba za ibada kujitakasa na kuomba kura.

Madahara yake ni makubwa sana, viongozi wote wa dini wanaoshabikia haya nao ni majanga ya kitaifa. Huwezi kumsafisha mchafu kwa fedha. Tanzania tufike mahali tumuogope Mungu. Hili swala la watu kutaka kuonekana wasafi wakati hawataki kutubu dhambi zao na kurudisha vyote walivyopata kwa ulaghai kwa masikini ndio wamfuate Mungu ni kebehi sio tu kwa madhehebu husika bali kwa viongozi wote wa dini wenye tamaa ya fedha chafu.

Kiongozi wa dini wajibu wake ni kukemea maovu na kufundisha kuhusu toba na kuwa mfuasi wa Mungu kwa matendo. Sidhani kama ni kazi yao kushamirisha matendo maovu kwa kupokea vipande vya dhahabu vya Yuda baada ya kumuuza Yesu.

Kesho watu hawa wanaotumia nyumba za ibada wakiingia Ikulu watakuwa viongozi wa nani?

Matumizi ya nyumba za ibada kwa vipande vya dhahabu ni dhihaka kwa Mungu. Kuhonga kanisani/Msikitini ni dhambi kubwa sana. Naomba wote wenye tabia hii chafu waache mara moja.

Udini ni zao la umasikini, wizi wa mali ya umma siasa chafu na tamaa ya madaraka. Viongozi wabovu duniani kote wanatumia kete ya kutenga na kutawala kwa gharama hata ya machafuko ya kidini, kikabila nk.

Ni wajibu wa viongozi na waumini wa dini zote kujua mbinu chafu za wanasiasa mufilisi. Nyumba za ibada sio sehemu ya kumtakasa mchafu kisiasa ili akubalike, kumbukeni wengi wamevaa ngozi ya kondoo na sio kondoo.
 
Tangu lini kuabudu kumeanza kubagua?

Tangu lini kushiriki shughuli za ibada imekuwa kosa?

Kazi ya kumhukumu mwanadamu ni ya Mungu tu...
 
Lowassa ana haki ya kwenda kanisani na kufanya afanyayo PROVIDED HAKUNA KAMPENI ZA KISIASA ANAZOFANYA.Lakini hata asiposema kitu kwa anayofanya tu tayari siku akitangaza kugombea urais au cheo chochote serikalini kuna watu wengi ndani ya UKRISTO watakuwa ktk hatari ya kumuona MTU WAO!nawaasa sana wakristu na watz kwa ujumla,TUSIDANGANYIKE.Tumpime kwa yale aliyofanya akiwa serikalini.tumpime kwa taarifa sahihi kuhusu yeye na sio PROPAGANDA.Haya ya kanisani tumuachie tu mwenyewe!tumuone ni muumini wa kawaida tu mwenye majukumu kwa dini yake kama wengine!
 
Hakika udini ni zao la umasikini kama unavyokiri ndugu yangu na wewe ni mdini namba moja. Imeandikwa usihukumu usije ukahukumiwa, EL huwa anaalikwa unataka akatae? Kama wewe au nyinyi hamumwaliki hawezi kuvamia kwenye ibada za machangizo yenu. Kiongozi anayependa kujali mambo ya watu wake hujitoa na nikudokeze kitu kimoja, Mungu huwabariki na kuwazidishia mpaka pasiwepo pa kuweka wote wamtoleao kwa moyo wa dhati hii ni siri na kama una imani itakusaidia. Leo hii nikikuuliza unajitoa vipi kwa Mungu huwezi kuniambia la maana maana najua ukitoa unafikiri unamtolea mwanadamu badala Mungu.
 
Lowassa ana haki ya kwenda kanisani na kufanya afanyayo PROVIDED HAKUNA KAMPENI ZA KISIASA ANAZOFANYA.Lakini hata asiposema kitu kwa anayofanya tu tayari siku akitangaza kugombea urais au cheo chochote serikalini kuna watu wengi ndani ya UKRISTO watakuwa ktk hatari ya kumuona MTU WAO!nawaasa sana wakristu na watz kwa ujumla,TUSIDANGANYIKE.Tumpime kwa yale aliyofanya akiwa serikalini.tumpime kwa taarifa sahihi kuhusu yeye na sio PROPAGANDA.Haya ya kanisani tumuachie tu mwenyewe!tumuone ni muumini wa kawaida tu mwenye majukumu kwa dini yake kama wengine!

Sasa wewe ndio umeanza kampeni.

Mtu anaenda kwenye nyumba ya bwana kutoa sadaka, hayo mabo ya siasa yametoka wapi tena?

Inaamana akienda sokoni nako mtasema kaenda kufanya siasa? sasa yeye ajifungie ndani tu?
 
Sasa wewe ndio umeanza kampeni.

Mtu anaenda kwenye nyumba ya bwana kutoa sadaka, hayo mabo ya siasa yametoka wapi tena?

Inaamana akienda sokoni nako mtasema kaenda kufanya siasa? sasa yeye ajifungie ndani tu?

kapumzike na uchukue ujira wako hapo lumumba ZeMarcopolo
 
Last edited by a moderator:
Wadau naomba mnijuze labda mimi sifahamu! Nimekua namfuatilia sana Ndugu yangu Edward wa Monduli nikagundua kuwa huenda kuna kitu kimejificha nyuma ya pazia. Kama mtakubaliana na mimi Mh Edward amekuwa akienda sana kwenye nyumba za Ibada na kutoa mamichango makubwa makubwa! kwanza sijui pesa zote hizo anatoa wapi? Afu mbona anachanga sana kuna nini kimejificha? Kuna wakati alikuja kwetu Tabora akatoa karibu milioni mia (100) je ni upendo wake kwa dini au kuna siri hapa! naomba mnijuze labda mimi namuhisi vibaya.....Nakutegemea sana ndugu yangu ukombozi katika hili.
 
Back
Top Bottom