mahwahwajr
Member
- Jun 10, 2010
- 18
- 22
Ndugu wanabodi,
Hapana shaka uchaguzi wa mwaka huu tayari umevuta na utaendelea kuvuta hisia za wachunguzi wa maswala ya kisiasa na hata wananchi wa kawaida, pengine kuliko uchaguzi mwingine wowote. Nina imani hali hii itaendelea mpaka Rais mpya wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania atakapopatikana.
Kuna sababu nyingi lakini moja kubwa ni mwamko mkubwa walio nao vijana kushiriki kwenye mchakato huu kama wagombea lakini zaidi sana wakiwa wapiga kura. Lakini sababu ya pili na kubwa zaidi ni SIFA za wagombea wawili; Mheshimiwa Edward Lowassa wa Umoja wa vyama vya Ukawa na Mh Dr John Magufuli wa Chama Tawala CCM. Wawili hawa wanafanana kwa sifa ya utendaji. Hata hivyo, Dr Magufuli anatambulika nchi nzima kutokana na kazi nzuri aliyoifanya akiwa wizara ya Ujenzi ambapo amefanikiwa kusimamia ujenzi wa miundombinu ya barabara nchi nzima.
Pia Dr Magufuli anatambulika kwa rekodi yake safi na kwamba hakabiliwi na TUHUMA ukimlinganisha na mgombea/mpinzani wake. Mh Lowassa anabebwa na kimuhemuhe cha vijana wengi wanaodai kutaka mabadiliko na hivyo kuwa tayari kumchagua yeyote ili tu kuiondoa CCM madarakani. Hili linathibitishwa na kauli za baadhi ya viongozi wa Ukawa walionukuliwa wakisema wanataka kuiondoa kwanza CCM madarakani halafu mengine yatafuata.
Hata hivyo, kitu kimoja ambacho Mhe Lowassa ataingia kwenye uchaguzi huu akiwa nacho kichwani ni kuelewa kwamba atakuwa anapambana na mtu MCHAPAKAZI kwelikweli ambaye yeye mwenyewe (Lowassa) amekiri mara nyingi kuukubali uwezo wake. Uchapakazi huu wa Dr Magufuli (na wala sio madai ya mabao ya mkono kama ambavyo wapinzania wanadai) kwa vyovyote vile lazima unamtia HOFU ya kushindwa mh Lowassa, licha ya sapoti kubwaya vijana ambayo anaonekana kuwa nayo...
Video hizi mbili zinathibitisha na zitakuwa zinalia kichwani kwa Mh Lowassa mda wote atakapokuwa anamkumbuka anayeenda kupambana nae...
Hapana shaka uchaguzi wa mwaka huu tayari umevuta na utaendelea kuvuta hisia za wachunguzi wa maswala ya kisiasa na hata wananchi wa kawaida, pengine kuliko uchaguzi mwingine wowote. Nina imani hali hii itaendelea mpaka Rais mpya wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania atakapopatikana.
Kuna sababu nyingi lakini moja kubwa ni mwamko mkubwa walio nao vijana kushiriki kwenye mchakato huu kama wagombea lakini zaidi sana wakiwa wapiga kura. Lakini sababu ya pili na kubwa zaidi ni SIFA za wagombea wawili; Mheshimiwa Edward Lowassa wa Umoja wa vyama vya Ukawa na Mh Dr John Magufuli wa Chama Tawala CCM. Wawili hawa wanafanana kwa sifa ya utendaji. Hata hivyo, Dr Magufuli anatambulika nchi nzima kutokana na kazi nzuri aliyoifanya akiwa wizara ya Ujenzi ambapo amefanikiwa kusimamia ujenzi wa miundombinu ya barabara nchi nzima.
Pia Dr Magufuli anatambulika kwa rekodi yake safi na kwamba hakabiliwi na TUHUMA ukimlinganisha na mgombea/mpinzani wake. Mh Lowassa anabebwa na kimuhemuhe cha vijana wengi wanaodai kutaka mabadiliko na hivyo kuwa tayari kumchagua yeyote ili tu kuiondoa CCM madarakani. Hili linathibitishwa na kauli za baadhi ya viongozi wa Ukawa walionukuliwa wakisema wanataka kuiondoa kwanza CCM madarakani halafu mengine yatafuata.
Hata hivyo, kitu kimoja ambacho Mhe Lowassa ataingia kwenye uchaguzi huu akiwa nacho kichwani ni kuelewa kwamba atakuwa anapambana na mtu MCHAPAKAZI kwelikweli ambaye yeye mwenyewe (Lowassa) amekiri mara nyingi kuukubali uwezo wake. Uchapakazi huu wa Dr Magufuli (na wala sio madai ya mabao ya mkono kama ambavyo wapinzania wanadai) kwa vyovyote vile lazima unamtia HOFU ya kushindwa mh Lowassa, licha ya sapoti kubwaya vijana ambayo anaonekana kuwa nayo...
Video hizi mbili zinathibitisha na zitakuwa zinalia kichwani kwa Mh Lowassa mda wote atakapokuwa anamkumbuka anayeenda kupambana nae...
Last edited by a moderator: