Lowassa mbioni kuinusuru Hoteli ya KKT, Corridor Spring

Lowassa mbioni kuinusuru Hoteli ya KKT, Corridor Spring

OgwaluMapesa

JF-Expert Member
Joined
May 24, 2008
Posts
10,942
Reaction score
437
Wana bodi!!
Hatimaye lile jembe la kaskazini Waziri mkuu mstaafu na mbunge wa Monduli mh. Edward Lowassa aingilia kati mgogoro wa hotel ya KKKT corridor spring isiuzwe.

Hili limejitokeza baada ya hotel hiyo kukopa fedha katika benki ya CRDB na kushindwa kulipa,ina sadikika hotel hiyo miaka ya nyuma ilichukua kiasi kikubwa cha hela na kushindwa kurudisha na kupelekea deni kufikia zaidi ya bilioni moja.

Jana mh. Lowassa alifnya kikao kikubwa na wafanyabiashara wakubwa kuhakikisha wanainusuru hoteli hiyo ambayo iko mbioni kuuzwa.

Katika kikao hicho ambacho kiliongozwa na mh. Lowassa walikubaliana watafanya harambee kubwa ya kufunga mwaka ambayo itakuwa ya kihistoria lengo ni kuhakikisha fedha hizo zinapatikana kuhakikisha hoteli inarudi mikononi mwa KKKT jimbo la Arusha.

Wakazi wa Arusha wamepokea kwa shangwe kubwa na kumpongeza kwa nguvu zote mh Edward Lowassa,wakazi hao wa Arusha hatimaye wamefikia maamuzi ya kutenga siku kwaajili ya kumwombea mbunge wa Monduli ili Mungu aendelee kumpa moyo wa huruma.

Wakaz hao wanasema walishakata tamaa na hawakuwa tena na matumaini kama hoteli ingebaki tena mikononi mwa KKKT.

Wanasema kiasi cha fedha ambacho hotel hiyo ilikuwa ikidaiwa kutokna na mkpo walio chukuwa hakuna mtu mwingine ambaye angeweza kuinusuru hoteli zaidi ya Lowassa kwani amekuwa na ushawishi mkubwa sana wa kushawishi wafanyabishara wakubwa kuchangia michango mbali mbali ya kimaendeleo.
 
Ofcoz lowassa pamoja na kimei wasinge iacha hiyo hotel pamoja selian hsptl ziuzwe. Ingekuwa ni aibu kubwa kwa walutheri wote wa arusha ikiwamo yeye. All in all Waliohusika na huu mchezo wote wakamatwe na kutaifishiwa mali zao. Tukianza na israel karyongi, Emanuel saevie na aliyekuwa mwenyekiti wa mali. Hawa jamaa wameimaliza kanisa kwa ufisadi wao wa kutisha. Wao ndio wamesababisha haya yote kutokea
 
Sisi waumini tupo tayari kabisa kuchangia hizi pesa endapo kweli hawa jamaa watachukuliwa hatua za kisheria.
 
yule mkenya aliyetoroka nchinialiyekuwa manager wa hoteli hiyo ameishia wapi..?

Yule mkenya ni shemeji yake na karyongi na yeye ndio alimweka hapo ili waifisadi hiyo hotel. Kwahiyo anajua mahali alipokimbilia
 
Hiyo hoteli inafaida gani kwa waumini? Na je waimini walishwa elezwa hizo pesa zilizo kopwa zilitumikaje? Na je wakati wa kukopa waumini walishilikiswa?
 
Wazili mkuu aliefukuzwa kwa kashfa ya kuuibia nji milion156 kwa siku, nae sasa amekua na huruma
 
haya sasa waje wale wafihidhina waanze kucrashi manake wao hawanaga jema umbwaaaa kabs
 
mi mwenyewe nilisha kata tamaa na hii hoteli,nilijuwa imesha potea mazma!!Lowassa!!Lowassa!!Lowassa!Mungu ampe maisha marefu mzee wa mamvi
 
Hiyo hoteli inafaida gani kwa waumini? Na je waimini walishwa elezwa hizo pesa zilizo kopwa zilitumikaje? Na je wakati wa kukopa waumini walishilikiswa?

haya maswali unapaswa umuulize kariongi!
 
Juzi tu tulilipa riba peke yake milioni 600, bado awamu nyingine.

Hoteli ya kanisa hairuhusu wazinzi, walevi, wavuta sigara kulala pale, na hakuna lounge kwa ajili ya kupata vinywaji vikali ndiyo maana hoteli haifanyi vizuri.

USHAURI WANGU;
Hoteli ya Corridor Spring iuzwe, fedha zitakazopatikana zielekezwe kujenga shule au hospitali ya kanisa
 
Juzi tu tulilipa riba peke yake milioni 600, bado awamu nyingine.

Hoteli ya kanisa hairuhusu wazinzi, walevi, wavuta sigara kulala pale, na hakuna lounge kwa ajili ya kupata vinywaji vikali ndiyo maana hoteli haifanyi vizuri.

USHAURI WANGU;
Hoteli ya Corridor Spring iuzwe, fedha zitakazopatikana zielekezwe kujenga shule au hospitali ya kanisa


Hapo umenena.
 
Juzi tu tulilipa riba peke yake milioni 600, bado awamu nyingine.

Hoteli ya kanisa hairuhusu wazinzi, walevi, wavuta sigara kulala pale, na hakuna lounge kwa ajili ya kupata vinywaji vikali ndiyo maana hoteli haifanyi vizuri.

USHAURI WANGU;
Hoteli ya Corridor Spring iuzwe, fedha zitakazopatikana zielekezwe kujenga shule au hospitali ya kanisa
pamoja na ufisadi kuwa mojawapo ya sababu ya kufilisika kwake ila
umetoa sababu nyingine ya maana sana!
 
Poor management why mnajiingiza kwny biashara msizoweza kizisimamia na kuanza kutembeza bakuri la ombaomba. It's much better kufocus ktk ujenzi wa matawi mengine ya kanisa na kuvuna waumini wengi zaidi ili kueneza injiri mana hiyo ndo main theme ya kanisa kuliko kujiingiza kwny biashara kwa manufaa ya wachache na kuleta aibu na usumbufu kwa waumini.!!
 
Weka taarifa iliyokamilika jamaa.Na ni kiasi gani sio mambo ya kusema "kiasi kikubwa cha fedha"
 
Back
Top Bottom