Watanzania tunakutambua kama moja ya matajiri wakubwa hapa nchini. Lakini katika gazeti la Mwananchi la Ijumaa 19/6/2015 umenukuliwa ukikana utajiri wako. Nanukuu:
Haya madai (ya utajiri) hayana hata chembe ya ukweli hata
kidogo, isipokuwa mimi nadhani wananitakia
mema kwa sababu ukiona jumba zuri wanasema
la Lowassa, gari nzuri la Lowassa, kitu chochote
kizuri wanasema cha Lowassa,
Kwa kauli hii unajaribu kutushawishi kuwa na wewe ni maskini mwenzetu. Kama basi wewe ni maskini, unatupaje matumaini ya kutuondolea umaskini watanzania wakati wewe mwenyewe umeshindwa kuondoa umaskini wako na familia yako? Na kama wewe ni tajiri (kama wengi tunavyokujua), kuna nini nyuma ya pazia kinachokutia hofu kukiri utajiri wako hadharani. Watanzania tunahitaji kiongozi muwazi na mkweli, na kwa maoni yangu umekosa sifa hizi mbili muhimu! Naomba kuwasilisha.