Niliichukia CCM long time kutokana na kutokuwa na utendaji wa kutuvusha na uadilifu. Lakini wakati nikijaribu kutathmini watia nia wote CCM niliona ni Lowassa pekee alikuwa na merites za kuwasumbua ukawa katika uchaguzi huu kutokana na utendaji wake. The man always walk the talk, and not merely talking the walk.
Kimsingi nilivutiwa sana na utendaji wa Lowassa kwa kipindi kifupi alichofanya katika awamu ya nne kama waziri mkuu. Hata hivyo, baada ya kutia nia kupitia chama chake cha awali cha kijani, nisingeweza kumpa kura kutokana na kupoteza imani na chama hicho kitambo. Kwa bahati nzuri amanipa fursa, kwa kukikimbia chama chenye kelele nyingi bila vitendo na kuja huku aliko ambapo nasi tupo. Ni wakati wa kutimiza ndoto yangu, ya kumchagua kwa kuwa ninaamini atatuvusha. Amekuja tulipo kwa dhati kabisa, alipo nipo, alipo tupo.
"Nitaendesha serikali kwa speed ya ajabu", hii ni kauli yake ambayo sina mashaka nayo kabisa. Inanipa matumaini ya Tanzania mpya isiyo na uzembe na taarifa za mkaguzi mkuu zilizojaa wizi wa rasilimali zetu. Na hii ni tahadhari kwa wale wanaofanya kazi kwa mazoea, kwa uzembe bila malengo, siku zao zinahesabika. Lowassa ni mtendaji, na si mtu wa maneno.
Ukombozi mpya ni sasa. Jibu tayari tunalo, jibu ni Lowassa. Na kama huamini juu ya ubora wa kiongozi huyu, muda utakujibu, na utakuja kunishuhudia haya niyasemayo kama ndoto yangu hii itatimia.