Lowassa kachezeshewa "chekundu cheusi"?

Lowassa kachezeshewa "chekundu cheusi"?

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Joined
Mar 10, 2006
Posts
34,095
Reaction score
43,305
Siupendi sana huu mchezo; kwani unaweza kukuaminisha kabisa kuwa utashinda. Unaona kabisa kwa macho yako kuwa karata nyekundu imefunikwa upande wa kushoto na unaona mtu mwingine anaapa kabisa iko pale na anaweka hela zake pale na wewe kwa kuamini "ulichokiona" na "ushawishi" wa mtu mwingine unaamua kuweka fedha zako pale. Unaulizwa una uhakika na wewe unaapa kabisa. Kweli ikifunuliwa unakiona kipo pale na wewe na yule mwingine wote mnalipwa! Unafurahia moyoni, unachekelea kwa sababu macho yako hayajakudanganya.

Raundi nyingine inafuatia; safari hii wewe peke yako una uhakika umeona karata iile na yule mwingine yeye anaweka pale ambapo una uhakika siko. Lakini kwa vile unaona kuwa una uhakika unaongeza na dau lake kusubiria mavuno. Karata zikifunuliwa unakuta umeliwa jumla!! Unataharuki na kuapa kuwa uliona kabisa. Unaamua kuondoka kwa kujikunyata. Umeweka fedha za ada ya watoto na pango la nyumba!

Baadaye unaambiwa kuwa wote wale walikuwa timu moja- yule mchezeshaji na yule shabiki aliyekuwa anakushawishi wewe - unaamua kurudi kwa hasira ili uwafungie kazi. Unakuta wameanua jamvi na wameondoka mahali. Unafikiria utamwambia nini mama wawili ukirudi nyumbani.

Ndivyo ambavyo tunaweza kuelezea jitihada kubwa ya kutikisa NEC na kumtikisa Kikwete. Kwa miaka karibu miwili kulikuwa na tishio la kutaka kutenganisha nafasi za Uenyekiti na ile ya Urais na hata siku chache zilizopita kulikuwa na madai ya kura za vijana ambao wanataka mabadiliko. Mwisho wa siku ni watu 2 tu walithubutu kumpigia kura za "Hapana" Mwenyekiti. Watu 2!

Kwa sababu hawakutegemea CCM kuwapiku kwa kubadilisha mtindo wa kupiga kura ambapo ingekuwa rahisi sana kuweza kujua kura za hapana zimetoka wapi. Hata uhesabuji kura - vyanzo vya ndani vinadokeza na hili litafumuka baadaye - ulifanywa ili kuhakikisha kujua ni kundi gani lilimpigia Rais kura za hapana.

Ni wazi mwisho wa kundi la Lowassa utaanzia leo; hasa tukisubiri uundwaji wa sekretariati mpya ya CCM ambayo itakipeleka chama hicho kwenye uchaguzi mkuu wa 2015. Mtu kaliwa. Lakini atarudi tena na fedha nyingine kujaribu kucheza mchezo ambao uko dhidi yake?
 
Mwanakijiji wewe ni mchambuzi mzuri mfano wa chekundu - cheusi unafurahisha lakini katika muktadha huu ni mfano mfu. Nani alikwambia kuwa Mh. Lowassa na Rais Kikwete ni maadui? Watu wanawekewa maneno nao wanayabeba kama majuha.
Lowassa na Rais Kikwete ni Marafiki wa siku nyingi na hakuna wa kuwatenganisha wala wao hawana sababu za kuwa maadui, wawe maadui kwa lipi???

Anayesema kuwa hawa ni maadui ama atakuwa ana matatizo kwenye ubongo na mfumo wote wa ufahamu wake au atakuwa ni wakala wa kuendelea kupumbaza watu kwa makusudi yao na hapo ndipo wanaokubali na kufikiri kuwa ni maadui ndio wanachezeshwa chekundu- cheusi!!

Hii ni JF watu tuna vichwa vizuri!!
 
Mwanakijiji wewe ni mchambuzi mzuri mfano wa chekundu - cheusi unafurahisha lakini katika muktadha huu ni mfano mfu. Nani alikwambia kuwa Mh. Lowassa na Rais Kikwete ni maadui? Watu wanawekewa maneno nao wanayabeba kama majuha.
Lowassa na Rais Kikwete ni Marafiki wa siku nyingi na hakuna wa kuwatenganisha wala wao hawana sababu za kuwa maadui, wawe maadui kwa lipi???

HON. MP, acha ku cream. Hawa mabwana siyo marafiki tena take it from me. Inawezekana wewe hauko karibu na yeyote kati ya hao. Si uliona juzi EL alimkacha JK alivyokwenda Monduli
 
Mkuu Mzee Mwanakijiji
Tangu juzi jumamosi kulikuwa na makundi mawili yenye mvutano mkali pale dodoma,kundi la Mh.Lowasa na wengine watiifu kwa JK walibakia uande huo,lakini JK alipoarifiwa kuwa kuna mpango wa kumpigia kura za HAPANA nae akaamua kuhakikisha kila sehemu anapata za chini ya kapeti na misimamo yao,watu wakagawanyika ndipo akapata jeuri ya kuwapiga mkwara kwenye ufunguzi na kubadilisha ratiba ya kupiga kura za Wajumbe wa Nec-CCM Taifa hapo akawa kisha wachanganya kwa kuwa aliarifiwa kuwa Mh.Lowasa anataka kuandalia watu wake chakula cha jioni.
Nadhani kama ni mtu wa kukoma Mh.Lowasa atakuwa amekoma maana watu alioamini ni wake si wake bali ni wa wenzao na kwa kweli mpango wake hauwezi kutimia na kwenye hili natumai atarejea Ujerumani kwenye matibabu...!!
 
Ingawa Kikwete ni balaa, Lowassa ni zaidi. Kikwete karibu ataondoka. Nisingependa aje Kikwete mwingine kupitia Lowassa. Kwa hili nawapongeza CCM ingawa ningependa waendelee kuboronga ili tuwachape goli la kisigino hapo 2015.
 
HON. MP, acha ku cream. Hawa mabwana siyo marafiki tena take it from me. Inawezekana wewe hauko karibu na yeyote kati ya hao. Si uliona juzi EL alimkacha JK alivyokwenda Monduli

Sote tuko karibu na rais Kikwete maana ni rais wetu wote Tanzania nzima!

Kukacha wapi? kwa hiyo mtu asipokuwepo mahala alipo mwingine ndio uadui? Mbona Rais kaenda na kugawa ng'ombe kwa Lowassa na Lowassa alikuwepo na akimtambulisha kwa furaha ya kutimiza aliloahidi! Je tukio hilo tu moja unaweza kuweka conclusion ya mahusiano ya watu!

Ni nani kati yao aliwahi kumsema mwenzake kwa ubaya, wapi? Zaidi ya wapambe tu wanaozusha hayo. Pili uadui wao ni wa nini sasa. Hawa watu hawagombei urais pamoja, Rais Kikwete anamaliza kipindi chake na ni marafiki wa siku nyingi. Wewe unaweza kuwa mmoja wa mawakala wa kusambaza uongo, danganyeni wasiofikiri!
 
kikwete siku zote hutaka kuonekana ni super star, kama unabisha angal;ia matukio, ooh pinda anasema angekuwa yy angemtimua yule katibu mkuu, kikwete anam..., ooh mawaziri wapeleka barua za kujiuzuru, anazikataa then anabadili baraza..., ooh kikwete kuongea na madaktai..sorry na wazee..inaahirishwa anapima upepo, anaonekana superstar..chezea JK wewe, tungoje tuone, kama lowassa anampinga...JK will win, he always does
 
kuna kitu kimoja wengi kitawasumbua kwa mda kidogo na wengi wanaweza wasikifahamu kabisa
 
Siupendi sana huu mchezo; kwani unaweza kukuaminisha kabisa kuwa utashinda. Unaona kabisa kwa macho yako kuwa karata nyekundu imefunikwa upande wa kushoto na unaona mtu mwingine anaapa kabisa iko pale na anaweka hela zake pale na wewe kwa kuamini "ulichokiona" na "ushawishi" wa mtu mwingine unaamua kuweka fedha zako pale. Unaulizwa una uhakika na wewe unaapa kabisa. Kweli ikifunuliwa unakiona kipo pale na wewe na yule mwingine wote mnalipwa! Unafurahia moyoni, unachekelea kwa sababu macho yako hayajakudanganya.

Raundi nyingine inafuatia; safari hii wewe peke yako una uhakika umeona karata iile na yule mwingine yeye anaweka pale ambapo una uhakika siko. Lakini kwa vile unaona kuwa una uhakika unaongeza na dau lake kusubiria mavuno. Karata zikifunuliwa unakuta umeliwa jumla!! Unataharuki na kuapa kuwa uliona kabisa. Unaamua kuondoka kwa kujikunyata. Umeweka fedha za ada ya watoto na pango la nyumba!

Baadaye unaambiwa kuwa wote wale walikuwa timu moja- yule mchezeshaji na yule shabiki aliyekuwa anakushawishi wewe - unaamua kurudi kwa hasira ili uwafungie kazi. Unakuta wameanua jamvi na wameondoka mahali. Unafikiria utamwambia nini mama wawili ukirudi nyumbani.

Ndivyo ambavyo tunaweza kuelezea jitihada kubwa ya kutikisa NEC na kumtikisa Kikwete. Kwa miaka karibu miwili kulikuwa na tishio la kutaka kutenganisha nafasi za Uenyekiti na ile ya Urais na hata siku chache zilizopita kulikuwa na madai ya kura za vijana ambao wanataka mabadiliko. Mwisho wa siku ni watu 2 tu walithubutu kumpigia kura za "Hapana" Mwenyekiti. Watu 2!

Kwa sababu hawakutegemea CCM kuwapiku kwa kubadilisha mtindo wa kupiga kura ambapo ingekuwa rahisi sana kuweza kujua kura za hapana zimetoka wapi. Hata uhesabuji kura - vyanzo vya ndani vinadokeza na hili litafumuka baadaye - ulifanywa ili kuhakikisha kujua ni kundi gani lilimpigia Rais kura za hapana.

Ni wazi mwisho wa kundi la Lowassa utaanzia leo; hasa tukisubiri uundwaji wa sekretariati mpya ya CCM ambayo itakipeleka chama hicho kwenye uchaguzi mkuu wa 2015. Mtu kaliwa. Lakini atarudi tena na fedha nyingine kujaribu kucheza mchezo ambao uko dhidi yake?

Inapokuja suala la kuongelea masuala ya CCM na hasa kumhusu lowassa huwa simuamini mwanakijiji hata kwa sekunde moja kwa sababu zifutazo,
1. kwanza mwanakijiji kwa kila dalili ya maandiko yake humu ni mfuasi wa Bernard Membe , hilo halina ubishi na hawezi muandika vibaya mfuasi wake.

2. kuhusu kutenganisha uenyekiti wa ccm na urais imebainika dhahiri kuwa walioandaa vipeperushi hivyo walifadhiliwa na membe na vyombo vya usalama vimethibitisha , zaidi walitaka aonekane ni lowassa wapate la kumsema, fuatilia tweets za serukamba utajua nini kiliendelea.


3. Nguvu ya lowassa nec ipime kwa wagombea wafuasi wake katika viti kumi vya NEC bara na Visiwani, hapo utaelewa bila kura za itifiki , kipenzi chako membe asingefurukuta.


mwisho niwaase wana JF kuwa linapokuja suala la Lowassa kupitia kwa MMKJJ litizameni mara mbili mbili kwa kuwa mara nyingi anaandika with a pre concluded assumptions . Kwa membe huwa hawezi kuficha hisia zake.
 
Kwa Tanzania wapiga kura hawawezi kukupa ushindi - bali wanaohesabu kura ndio wanaoamua mshindi. Na Kikwete na wenzie wanajua hivyo!
 
Huyu kijana anaejiita Mzee Mwanakijiji, anaonesha kwa dhati kabisa kuwa ni fataani kwelikweli na anataka kuwaaminisha watu yasiyokuwepo.

Humjui Kikwete humjui Lowassa, unawasikia tu.

Mtakufa navyo vijiba vya roho!
 
Jay Kay mjuzi wa kujinyumbua kimwili na kifikra kama ajuavyo kucheza. He is smart on that.
 
Mkuu Mzee Mwanakijiji
Tangu juzi jumamosi kulikuwa na makundi mawili yenye mvutano mkali pale dodoma,kundi la Mh.Lowasa na wengine watiifu kwa JK walibakia uande huo,lakini JK alipoarifiwa kuwa kuna mpango wa kumpigia kura za HAPANA nae akaamua kuhakikisha kila sehemu anapata za chini ya kapeti na misimamo yao,watu wakagawanyika ndipo akapata jeuri ya kuwapiga mkwara kwenye ufunguzi na kubadilisha ratiba ya kupiga kura za Wajumbe wa Nec-CCM Taifa hapo akawa kisha wachanganya kwa kuwa aliarifiwa kuwa Mh.Lowasa anataka kuandalia watu wake chakula cha jioni.
Nadhani kama ni mtu wa kukoma Mh.Lowasa atakuwa amekoma maana watu alioamini ni wake si wake bali ni wa wenzao na kwa kweli mpango wake hauwezi kutimia na kwenye hili natumai atarejea Ujerumani kwenye matibabu...!!

Mh. Lowasa atapoteza fahamu safari hii, jiulize mkuu, kama yeye ana watu anaowaamini, kwa nini alikimbia kundi lakifo? Hakuna kitu tena pale! Ngoja tusubiri kama bado atakuwa na nguvu ya kwenda kwenye makanisa, mashule na misikiti kutoa vijisenti eti michango! Mwizi tu!
 
With CCM so much is speculation
hujui nini ni nini
nani ni nani
Mara Mangula adui wa Kikwete
mara sasa washkaji
mara Nape adui wa Mkama mara sasa washkaji
mara huyu ataondolewa .mara kapandishwa cheo...
Aliekuwa anaweza kuielewa CCM alikuwa Sheikh Yahya peke yake.....
sisi wengine mpaka tujifunze elimu ya utabiri na majini hatuwezi
 
Back
Top Bottom