Lowassa: Kikwete Ameharibu Uchumi

Ni kweli kabisa, maisha ni magumu sana na mbaya zaidi yanazidi kuwa magumu..Kila kitu kiko juu, hakuna unafuu.
Ni wakati wetu sasa Watanzania kuitumia hii turufu kuchagua viongozi bora watakaotumia madaraka yao vyema.
#PamojaTutashinda

achana nayo fanya mambo mengne.
maisha magumu unakesha j.miii forum ??
maisha magumu soko la kina iphone. samsung na magar ya bei yamejazanaa foren??
mnataka maisha gan nyinyi ???
unadhan chadema itakuja kutatua matatizo yak ya familia.????
hahahah nifah beiby
 
achana nayo fanya mambo mengne.
maisha magumu unakesha j.miii forum ??
maisha magumu soko la kina iphone. samsung na magar ya bei yamejazanaa foren??
mnataka maisha gan nyinyi ???
unadhan chadema itakuja kutatua matatizo yak ya familia.????
hahahah nifah beiby

Hahahaaaaa, mwanzo nilitaka nikujibu hovyo ila nimeona haina maana.
Kwani kutokushinda JF ndio maisha yatakua marahisi ilhali gharama za maisha zinapanda kila siku?
Jaribu kutumia akili basi kujenga hoja, sio unakuja na hoja nyepesi ambayo hata mtoto wa darasa la 3 atakushangaa.
Hayo ma iPhone n.k ni swali la kuuliza? Hujui kwamba tabaka kati ya matajiri na masikini linazidi kukua siku hadi siku?
Mwisho kabisa ndio nimekuona kilaza kabisa hata sikustahili kukujibu basi tu nimeamua kukupa darsa la bure.
Huwezi kuikwepa siasa katika maisha yako, leo hii kila kitu kiko juu kutokana na haohao wanasiasa wanaosaini mikataba mibovu huku wakiweka maslahi yao mbele zaidi ya taifa.
Leo hii umeme uko juu na kila kitu kimepanda....jaribu kujiongeza.
Hata kama ufanye kazi zaidi ya punda, mchana na usiku huku gharama za maisha ziko juu sahau kupata mafanikio kwa wakati.
 
Maisha yamekuwa magumu, vijana wanakosa fursa za kuajiriwa na kujiajiri, viwanda vimekufa, kila sekta ya uchumi ipo hoi.
Ichagueni CCM muangukie pua.
 
Huyu jama ni kweli kaharibu uchumi. Aliingia Ikulu akakuta nchi ina akiba ya kutosha ya fedha alizoacha Mkapa basi akaanza kutumbua hela. Mara mabilioni ya JK, zilipoisha hakuongelea tena mikopo ya mabilioni ya JK kwa sababu ulikuwa uamuzi wa mhemko baada ya kuona furushi la hela. Akaja na Kilimo Kwanza na kugawa pembejeo za kilimo, baada ya muda na yenyewe ikapotea. Ikaja Big Results now, ikapiga hela na kelele kwa miezi kadhaa. Na yenyewe kimya sasa. Ameingia deni la taifa ni trilion 8, anaondoka deni ni trilion 40, alichofanya cha maana hakuna.

Kwa kifupi, Kikwete hakuwa na maono ya kiuchumi. Hakuna sera hata moja ya uchumi iliyofanikiwa. Mbaya zaidi eti ana shahada ya uchumi. Ameshindwa kujenga uchumi kama alivyofanya mwandishi wa habari (Mkapa). Tunahitaji Rais mwenye maono ktk uchumi, mtu ambaye atakuwa tayari kuteua wataalamu kwa ueledi na sio kwa kujuana na kulipana fadhila kama Kikwete. NI kwa kufuata utaalam wa kiuchumi tu ndo tutaondoka hapa tulipo.
 
Hahahaaaaa, mwanzo nilitaka nikujibu hovyo ila nimeona haina maana.
Kwani kutokushinda JF ndio maisha yatakua marahisi ilhali gharama za maisha zinapanda kila siku?
Jaribu kutumia akili basi kujenga hoja, sio unakuja na hoja nyepesi ambayo hata mtoto wa darasa la 3 atakushangaa.
Hayo ma iPhone n.k ni swali la kuuliza? Hujui kwamba tabaka kati ya matajiri na masikini linazidi kukua siku hadi siku?
Mwisho kabisa ndio nimekuona kilaza kabisa hata sikustahili kukujibu basi tu nimeamua kukupa darsa la bure.
Huwezi kuikwepa siasa katika maisha yako, leo hii kila kitu kiko juu kutokana na haohao wanasiasa wanaosaini mikataba mibovu huku wakiweka maslahi yao mbele zaidi ya taifa.
Leo hii umeme uko juu na kila kitu kimepanda....jaribu kujiongeza.
Hata kama ufanye kazi zaidi ya punda, mchana na usiku huku gharama za maisha ziko juu sahau kupata mafanikio kwa wakati.

tukutane october
vyote unavyolilia avina maana.
 
Hivi wakati lowasa yupo PM kwenye senate walikua hawafuati ushauri wake?

Hawakufuata ushauri wake, ukitaka kuthibitishiwa hilo kuhusu RICHMOND baada ya kuona magumashi aliita kikao cha makatibu wajadili na kuvunja mkataba lakini likatoka AGIZO KUTOKA MAMLAKA YA JUU kuruhusu mchakato uendelee.

Mwaka 2008 umeme uniti 72 tulipata kwa tsh.10,000/- lakini mwaka 2015 umeme unit 64 unazipata kwa tsh.30,000/-.
Kwa nini gharama za uzalishaji bidhaa, huduma zisipande?

Sukari, Sabuni, Ndala, Biki, Daftari, Ream Paper, Mafuta ya kula, Ngano, Kiberiti, Pipi, Biskuti vyote vimepanda bei hata uongezewe mshahara hakuna unafuu.

Tumegundua gesi ilipaswa ipatikane kwa bei nafuu ili kusaidia kupunguza matumizi ya mkaa na kuni na upatikanaji wa umeme lakini ni kucheka cheka tu.
 
Lowassa hawezi na hana uwezo wa kuhubiri mapungufu ya CCM. Kakuwa ndani ya chama kile. Hoja zingine jamvini hazina mashiko. Mtu anasema alinunua shati elfu 12 na sasa elfu 20. Shati ni lilelile? Amenunua palepale?
Licha ya tatizo la mfumuko wa bei, kiuhalisia nchi hasa sekta binafsi zinapanuka. Nchi inakuwa na viashiria vya kiuchumi vinaonekana. Hili inawezekana yasiwe mafanikio ya CCM bali ni ya wakati.
Lowassa hawezi kuikosoa CCM na wala hawezi kubadilisha mfumo. Ni CCM imeamua kuchukua UKAWA
 
Hawakufuata ushauri wake, ukitaka kuthibitishiwa hilo kuhusu RICHMOND baada ya kuona magumashi aliita kikao cha makatibu wajadili na kuvunja mkataba lakini likatoka AGIZO KUTOKA MAMLAKA YA JUU kuruhusu mchakato uendelee.

Mwaka 2008 umeme uniti 72 tulipata kwa tsh.10,000/- lakini mwaka 2015 umeme unit 64 unazipata kwa tsh.30,000/-.
Kwa nini gharama za uzalishaji bidhaa, huduma zisipande?

Sukari, Sabuni, Ndala, Biki, Daftari, Ream Paper, Mafuta ya kula, Ngano, Kiberiti, Pipi, Biskuti vyote vimepanda bei hata uongezewe mshahara hakuna unafuu.

Tumegundua gesi ilipaswa ipatikane kwa bei nafuu ili kusaidia kupunguza matumizi ya mkaa na kuni na upatikanaji wa umeme lakini ni kucheka cheka tu.

mkuu bila kupiga injili ya mabadiliko kuanzia sasa mpaka oct 25 hakita eleweka,

kila mtu kwapamoja iwe kanisani,misikitini,baa,misibani,kwenye sheree,kwenyw dala dala,maofisini,

nikuamshana kila mtu akapige kura oct 25 tumuondoe huyu mnyonyaji ccm, wameharibu kila kitu,

mimi nilikua mwaka 2000 - 2005 nyumbani nilikua naacha 3,500 kuanzia chai chakula cha mchana na usiku, tena mboga 3 menu ya ukweli,

leo ihi hata elf 20,000 haitoshi hawa jamaa mimi sitaki hata kuwaona,
 
Wenzake waadilifu hawatekelezi amri zisizoeleweka
Kama mwadilifu yupi mkuu...si unaona bandari isiyo na tija inajengwa Bagamoyo wakati ya Dar ipo mita chache kutoka hapo...hiyo ni amri ya mkubwa kwa mwadilifu Mwakyembe kupitia baraza la mawaziri ambalo halikupinga. Lowassa nani apinge mamlaka ya juu
 
Kama mwadilifu yupi mkuu...si unaona bandari isiyo na tija inajengwa Bagamoyo wakati ya Dar ipo mita chache kutoka hapo...hiyo ni amri ya mkubwa kwa mwadilifu Mwakyembe kupitia baraza la mawaziri ambalo halikupinga. Lowassa nani apinge mamlaka ya juu
Suala la utendaji wa Lowassa halipimiki kwa muda ambao Kikwete amekuwa madarakani. Lowassa anahistoria ndefu saana. Anaweza kutuambia ana mali kiasi gani na amezipataje? Anaweza kutuambia ule msafara kwa kura za maoni mpaka kuchukua fomu ni nani alimfadhili? Tunafanya kosa hapa. Alichofanya yule bwana ni kutafuta nguo za khaki na kuvaa juu ya suruali nyeusi na shati la kijani. Hali ya hewa ikibadilika na jua kuzidi tutamuona akivua nguo za khaki.
 
Kuna jamaa yangu hampendi Lowasa kwa sababu alisababisha picha na video ya harusi yake ziharibike.

Kipindi Lowasa PM alipita halmashauri moja akatikisa mbaya, mkurugenzi mtendaji wa halmashauri aliachwa hana uhakika wa ajira yake.
Sasa sehemu ya pili kwenda ilikuwa kwa mshkaj ambaye yeye alikuwa District Treasury, alikaliwa kooni wiki nzima kuweka mambo sawa hadi siku moja kabla ya harusi. Alikuwa anakesha kuziba mapengo na viporo, siku ya harusi alikuwa na usingizi mbaya
 
Kuna jamaa yangu hampendi Lowasa kwa sababu alisababisha picha na video ya harusi yake ziharibike.

Kipindi Lowasa PM alipita halmashauri moja akatikisa mbaya, mkurugenzi mtendaji wa halmashauri aliachwa hana uhakika wa ajira yake.
Sasa sehemu ya pili kwenda ilikuwa kwa mshkaj ambaye yeye alikuwa District Treasury, alikaliwa kooni wiki nzima kuweka mambo sawa hadi siku moja kabla ya harusi. Alikuwa anakesha kuziba mapengo na viporo, siku ya harusi alikuwa na usingizi mbaya

Hakika Lowassa ni mchapa kazi na hana utani na wazembe.
 
Yeye anajifanya watanzania sasaiv wana maisha mazuri, baba gari, mama gari, mtoto gari.. Sijui anamzungumzia nani?
 
Suala la utendaji wa Lowassa halipimiki kwa muda ambao Kikwete amekuwa madarakani. Lowassa anahistoria ndefu saana. Anaweza kutuambia ana mali kiasi gani na amezipataje? Anaweza kutuambia ule msafara kwa kura za maoni mpaka kuchukua fomu ni nani alimfadhili? Tunafanya kosa hapa. Alichofanya yule bwana ni kutafuta nguo za khaki na kuvaa juu ya suruali nyeusi na shati la kijani. Hali ya hewa ikibadilika na jua kuzidi tutamuona akivua nguo za khaki.
Tusubiri tuone...acha tumpe benefit of the doubt
 
Back
Top Bottom