Lowassa: Kikwete Ameharibu Uchumi

CASTRO PEMBA

Member
Jul 29, 2015
85
50
Katika mkutano wa kihistoria, mh" rais mtarajiwa amesema JK ameharibu uchumi, watu weng wamekua maskini, bidhaa juu, hoi

Akizungumza na wafuasi wa Chadema na UKAWA katika ofisi za Chadema mara baada ya kuchukua fomu ya kuwania urais kupitia chama hicho amesema, "rafiki yangu Jakaya Kikwete ameuharibu uchumi wa nchi yetu," ameongeza: "Wakati Rais Mkapa anaondoka madarakani kilo ya sukari ilikuwa Sh. 600 leo ni Sh. 2,300. Mchele ulikuwa Sh. 550 leo ni Sh. 2,300. Sembe ilikuwa Sh. 250 leo ni Sh. 1,200."

Aidha Lowassa amesema, katika kipindi cha utawala wa Rais Kikwete ndipo Tembo na kila aina ya wanyama wameuwawa kuliko kipindi chochote katika historia ya Tanzania.

"Katika utawala wa Rais Kikwete, Tembo wameuawa kuliko kipindi chochote katika historia duniani kote. "Kila aina ya mnyama ameuawa kuliko kipindi chochote katika historia ya nchi yetu.

Nitaijenga serikali yenye uchumi kwa speed (kasi), ambaye hawezi akae pembeni," amesema Lowassa.

Chanzo: MwanaHalisi Online
 
Huyo lowassa alikuwa wapi? Unafiki huu wa kiwazimu kweli, Halafu hana cha kusema ila tu ntawafanya Watanzania matajiri kwa njia ipi? Holaa hakuna anachojua zaidi ya ajira ni bomu na ntawafanya watz matajiri, nyumbu hata hawawazi utajiri huo utatoka wapi
 
Aliyoyasema yako wazi hayahitaji ushahidi, mpaka chumvi imepanda bei kwenye huu utawala dhalimu. Watakaobisha ni wale walioshiriki kutuharibia uchumi.

Liwike, lisiwike Lowassa all the way to the white house.
 
Lowassa kachoka sana, kwani tunamchagua JK ama tunamchagua JPM? alafu mbona yeye alikuwa ni mmoja wa watumishi katika serikali anayoilaumu? kama ilishindwa na yeye tunamhesabu ni mmoja wao
 
Back
Top Bottom