Lowassa hajawahi kukataliwa na CCM!!

Lowassa hajawahi kukataliwa na CCM!!

Nashukuru angalau kwa kunijibu zuzu mimi. Lakini swali la udadisi tu, jee kwenye hii mada uzuzu wangu uko kwenye eneo gani hasa??
Uzuzu wako uko maeneo mengi sana hasa kwa kutokubali na kuelewa kwamba Lowassa hakuja CDM kwa hiyari yake bali kwa KUKATWA! Pili CCM kama haina ubavu wa kumkataa basi wangemteua kuwa mgombea Urais na tatu ni kwamba kutomteua Lowassa maana yake ni KUMKATAA!! Kutokana na sababu hizo ndio umethibitisha ulivyo lofa na bwege mtozeni!!
 
kwa hiyo Pinda alikataliwa,Mwungulu alikataliwa,Membe alikataliwa,Kinwangala alikataliwa,Wasira alikataliwa,Makamba alikataliwa, na wote waliokatwa walikataliwa
Hao wote uliowataja ni rahisi tu kufaham kuwa lengo ilikua mlengwa ni lowasa maana ndo alikua zigo lisilobebeka ndani ya ccm
 
Wanyoa vipara siku zote huwa na akili za makengeza.
 
Hapo ndiyo hoja yangu ilipo. CCM haikuwa na ubavu wa kumfukuza Lowassa na hata alipotoka si wao waliomtoa bali ni yeye mwenyewe alitoka. Kwa maana nyingine ile hoja kwamba CCm ndiyo ilimkataa Lowassa kutokana na ufisadi wake ni uzushi wa kina Nape na hao "List of 46".
Lowasa alikataliwa au ww kukataliwa ukitakaje?. Kama alisema kuwa jina lake haliwez kukatwa halafu likakatwa au kukatiliwa ukitaka kuwe vip?
 
Kuna Propaganda zinazoenezwa na CCM na humu JF na "List of 46" wako bize kwa hilo, kwamba Lowassa alijiunga na CHADEMA baada ya kukataliwa na CCM kutokana na "Ufisadi" wake jambo ambalo si la kweli kwa asilimia mia moja. Lowassa alijiunga na CHADEMA baada ya kukataa kuwa Kondoo wa kafara kama walivyofanya kina John Malecela na Gharib Bilal walipoonewa na CCM.

Malecela na Bilal walikubali kukaa kimya hata pale taratibu za chama chao zilipopindwa ili kuwazuia kugombea Urais,lakini Lowassa alijua kuwa "Once beaten twice shy" ni heri kufa umesimama unapigania haki yako kuliko kufa umepiga magoti kwa kusubiria makombo!! Kama kuna mtu ataleta ushahidi hata wa kimazingira kwamba Lowassa aliwahi kukataliwa na CCM kutokana na "Ufisadi" wake naweza kubadili msimamo wangu kuhusu uhalali wa CHADEMA kumpokea Lowassa na kumfanya awe mgombea wake Urais!!
Mkuu Allen,ni kweli hakufukuzwa aliamuwa kutimka ili kuendeleza safari ya matumaini....ila kwasasa nikueleze "EL ni project ya CCM"..hauwezi kuona kwa macho yako hadi uwe na uzoefu wa chaguzi angalau 4 za tanzania au uwe unafuatilia siasa za TZ kwa miaka 20 mfululizi....ni mtego ulionasa chadema na kwa taarifa tu Edward haipendi chadema kwani ndiyo iliyomsababishia kuzongwa na kuitwa gamba...kwa "first time voter" itamchukuwa miaka angalau 10 kugundua hili.
 
Vijana wa mafisadi mnakazi kweli kumtetea fisadi wenu poleni.
 
Lowasa alikataliwa au ww kukataliwa ukitakaje?. Kama alisema kuwa jina lake haliwez kukatwa halafu likakatwa au kukatiliwa ukitaka kuwe vip?
Mkuu huyu mleta mada kachanganyikiwa kweli anadhani kukataliwa mpaka amwagiwe maji ya moto?
 
Kitendo cha kukataliwa kupeperusha nafasi ya juu kabisa ya CCM ilikuwa salamu tosha kwamba hawamtaki na wale wote ambao hawakukubaliana na maamuzi ya chama wakamfata akiwemo kingunge ila ningekuelewa zaidi kama ukisema Lowasa hakuwahi kukubalika chadema maana tunajua maneno waliyokuwa wakimvurumishia kabla hajajiunga na chama chao ndio maana alitumia mbinu ya kuonga viongozi wa juu ili wampitishe kiasi cha kumfanya katibu ambaye ni mtendaji mkuu wa chama kujiondoa na mpaka sasa mmeshindwa kujaza nafasi yake na wewe mwenyewe ni miongoni mwa watu mliokuwa mnapinga asipokelewe CHADEMA baada ya kukatwa CCM
 
Anaelala na choo chumbani ,na mtu anaelala chooni ni yupi afadhali???
 
Nilimaanisha anaelala na kinyesi na anaelala chooni ni yupi afadhali,l am sory
 
Kuna Propaganda zinazoenezwa na CCM na humu JF na "List of 46" wako bize kwa hilo, kwamba Lowassa alijiunga na CHADEMA baada ya kukataliwa na CCM kutokana na "Ufisadi" wake jambo ambalo si la kweli kwa asilimia mia moja. Lowassa alijiunga na CHADEMA baada ya kukataa kuwa Kondoo wa kafara kama walivyofanya kina John Malecela na Gharib Bilal walipoonewa na CCM



ALIKATALIWA kuwa mgombea, HAKUKATALIWA kuwa mwanachama.
 
lowasa aliondoka ccm kama dr slaa alivyoondoka cdm, wote hawakukubaliana na maamuzi ya KAMATI KUU ya vyama vyao, sasa ndo ujiulize hyo kamati kuu ni nn na kazi yake nini katka vyama.
 
lowasa aliondoka ccm kama dr slaa alivyoondoka cdm, wote hawakukubaliana na maamuzi ya KAMATI KUU ya vyama vyao, sasa ndo ujiulize hyo kamati kuu ni nn na kazi yake nini katka vyama.
Kuna tofauti kimamlaka kati ya Kamati Kuu ya CHADEMA na Kamati Kuu ya CCM linapokuja suala la mgombea Urais!
 
Lowassa alikuwa campaign manager wa rais wa awamu ya nne, alikuwa na influence kubwa sana. Nadhani hiyo ni sababu hata JK alikuwa anatumia ule mtindo wa "handle with care", kwa sababu kwa kumgusa mtu ambaye ametumia maisha yake yote katika kujenga networks za watu, unakuwa umekitingisha chama. JK alikuwa leo anakula huku, kesho anakula kule. Leo anakwenda Butiama na kucheka na Mama Maria Nyerere, kesho anakaa na wafanyabiashara wapigaji watoto wa mjini. Hivyo pamoja kuwa alikuwa ni rafiki na Lowassa alikuwa anahakikisha hawaudhi wazee wa Nyerere (ambao ukweli ni kwamba alishawaudhi siku nyingi).

Hivyo Lowassa kuondoka mwenyewe ni sawa na kuondolewa kwa sababu aliyemuwekea zengwe mpaka akaondoka, alihakikisha kuondoka kwake hakuwezi kuigharimu CCM kiasi cha kushindwa uchaguzi mkuu. Lowassa alianza kutengeneza mazingira ya kuwa mtu fulani mkubwa baadae tangu enzi za ujana wake, tangu enzi za awamu ya kwanza alishaanza kuwafuata watu kwa nia ya kuwataka wawe upande wake. Hivyo kumuondoa kwa kumfukuza isingewezekana. Ilibidi utafutwe wakati muafaka wa kumvunja kabisa moyo, kwa kutegemea mikakati ya kisiasa ili hasira zake mwenyewe ziwe ndio kiongozi wa maamuzi yake.
 
Back
Top Bottom